MAKAMO Mwenyekiti wa CCM
Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein amesema yeye siyo kiongozi Dikteta
kwani hajawani kumfukuza kiongozi yeyote wa kisiasa ndani ya Chama chake
kwa ajili ya kulinda maslahi binafsi.
Alimtaja Katibu Mkuu wa Chama cha
CUF,Maalim Seif Sharif Hamad kuwa amekuwa akizua na kuzusha uongo kwa
wafasi wake kwa kuwaaminisha kwamba Dkt. Shein ni kiongozi Dikteta
anayetawala Zanzibar kwa mabavu jambo ambalo sio la kweli.
Ufafanuzi huo Dkt.Shein ameutoa
wakati akizungumza na Mabalozi (wajumbe wa nyumba kumi) , Wenyeviti na
Makatibu wa matawi, vijana na Wazee wa CCM katika ziara zake alizofanya
hivi karibu huko katika Wilaya ya Mfenesini Kichama kwenye Ukumbi wa
Chuo cha Kumbukumbu za Mwl. Nyerere Tawi la Zanzibar Bububu.
Katika ziara hizo zlizokuwa na
lengo la kuwashukru wafuasi wa Chama na wananchi kwa ujumla walioichagua
CCM kwenye uchaguzi Mkuu wa Marudio uliofanyika Machi 20 mwaka huu
pamoja na kuimarisha kuongeza kasi za kiutendaji ndani ya Chama, Dkt.
Shein aliwataka wananchi kupuuza kauli na misimamo ya wapinzani hasa
Maalim Seif kwani hoja zao hazina nia ya kuwaunganisha wananchi bali ni
za utengano.
Dkt. Shein alisema bango
lililobebwa na Maalim Seif lililokuwa likimtangaza Rais wa Zanzibar kuwa
ni Dikteta ni moja ya siasa zilizopitwa na wakati na kupingana na
dhamira ya kuanzishwa kwa Mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, ulioasisiwa
kwa nia ya kufanya siasa za uchumi na maendeleo kwa wananchi wote bila
ya ubaguzi.
“Mimi sio Dikteta kwani sijaingia
madarakani kwa ubabe na mabavu kilichoniweka madarakani ni nguvu ya
umma kupitia Uchaguzi wa Kidemokrasia na kupata ushindi wa zaidi ya
asilimia 91.
Sasa huyo anayenitangaza eti mimi
ni Dikteta kweli maana ya neno hilo anayajua ama anasema kuwaridhisha
wafuasi wake, akae akijua kwamba hawezi kunichafua kwa njia hiyo kwani
kinga yangu ni Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 niliyoapa kuilinda na
kuwatumikia wananchi kwa uadilifu.”, alifafanua Dkt. Shein.
0 maoni:
Chapisha Maoni