Alhamisi, 2 Juni 2016

BARAZA LA VIJANA CHADEMA MKOA WA IRINGA[BAVICHA] NA SHIRIKISHO LA VYUO VIKUU CHADEMA IRINGA [CHASO] WATOA TAMKO KUHUSU WABUNGE WALIOSIMAMISHWA



SHIRIKISHO la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Chadema (CHASO)  Mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na baraza la vijana chadema Mkoa huo (BAVICHA) wameitaka serikali kupitia Wizara ya elimu kuwarudisha haraka wanafunzi wa vyuo kikuu ha Dodoma (UDOM) ambao walirudishwa nyumbani juzi ili waweze kuendelea kupata haki yao ya msingi ya kuendelea kupata elimu ili wakawahudumie wananchi kama ilivyokusudiwa.

Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu wa baraza la vijana Chadema (BAVICHA) Mkoa wa Iringa Jackson Mnyawami wakati akizungumza na wanahabari mjini hapa na kusema kuwa endapo serikali haitowarudisha wanafunzi hao chuoni hapo wapo tayari kufanya maandamano nchi nzima kwa kushinikiza wanafunzi hao kurudi chuoni kwa sababu kitendo cha kuwarudisha majumbani ni kuwanyima haki zao za msingi.

Katibu huyo pia ameitaka serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Magufuli kutafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali katika sekta za umma ili kuepuka kutokea matatizo kama hayo katika nchi yetu.

Mnyawami alisema kuwa mgogoro wa walimu na serikali katika chuo kikuu cha Dodoma ni matokeo ya kupuuza madai ya watumishi wa umma kwa muda mrefu na hivyo kupelekea kuzorotesha utoaji wa huduma katika sekta za umma,kwani watumishi wa umma wamekuwa wakilalamikia serikali kwa miaka mingi uboreshwaji wa maslahi yao ikiwamo mishahara inayokidhi na kuwaboreshea mazingira mazuri ya kazi lakini serikali meonekana kuziba masikio.

Alisema kuwa Wanafunzi waliofukuzwa chuo kikuu cha Dodoma ni wanafunzi halai,waliopelekwa na serikali kwa mpango wa maalumu kwa ajili ya kupunguza adha  ya uhaba wa walimu wa sayansi  kwa shule za msingi na sekondari ,serikali ilifanya vyema namna ya kukabiliana na changamoto hiyo ambapo ilikuja na program ya kuwapeleka walimu waliofaulu vizuri  kidato cha nne upande wa sayansi  kwenda kuchukua mafunzo ya ualimu kwa muda wa miaka mitatu (specia program).

Pia alisema kuwa wanafunzi hao waliendelea kusoma chini ya udhamini wa bodi ya miopo kwa mujibu wa maelekezo ya serikali lakini jambo la kushangazwa Mei 25 mwaka huu serikali hiyo ilitoa tamko kupitia waziri wa elimu Prof.Joyce Ndalichako kuwataka wanafunzi hao kuondoka kwenye eneo la chuo kwa kile alichodai kwamba kumekuwa na mgomo wa walimu usiopungua mwezi mmoja mgomo ambao umepelekea walimu kutoingia madarasani kwa muda mrefu.

Awali akizungumza mwenyekiti wa chaso Iringa Paschal Sulley alisema kuwa  chaso na bavicha Iringa wamepatwa na wasiwasi mkubwa juu ya utendaji wa mhimili wa bunge katika utekelezaji wa majukumu yake ya kuisimamia na kuishauri serikali katika awamu ya tano ambapo imeonekana dhahiri bunge linasimamiwa na serikali.

Sulley alisema kuwa wachaso na bavicha wamelaani vikali ofisi ya spika kupitia kamati ya bunge haki na madaraka kuwasimamishwa wabunge wa upinzani kushiriki vikao vya bunge kwani maamuzi hayo yana hasara nyingi  ikiwamo kuwanyima wananchi haki ya uwakilishi ndani ya bunge hasa katika vikao vya bajeti.

 Alisema kuwa kitendo hicho kinadumaza ukuaji wa demokrasia  yetu changa.

Aliongeza kuwa  kuondoa sehemu ya bunge hususani upinzani  kunapelekea kulifanya bunge la serikali kukosa meno kwani hapatakuwapo ka mawazo mbadala katika vikao vya bunge hivyo kupelekea kupitisha vitu visivyo na tija katika nchi yetu.


0 maoni:

Chapisha Maoni