Kwa Habari za kitaifa na kimataifa

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za michezo na burudani

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za afya

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za Kilimo

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za uchumi na biashara

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za elimu

Tembelea Kali ya habari

Jumanne, 31 Januari 2017

MANISPAA YA ILALA YAWATAKA WANANCHI KULIPA KODI YA MABANGO

Posted by Esta Malibiche on JAN 31,2017 IN NEWS

MAW2
Afisa Uhusiano wa Manisapaa ya Ilala Bi Tabu Shaibu akifafanua kwa waandishi wa Habari Leo Jijini Dar es salaam kuhusu mikakati ya manispaa hiyo katika kuwaletea wananchi maendeleo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari MAELEZO bi Zamaradi Kawawa.
MAW1
Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Ilala Bi Tabu Shaibu akizungumza wakati wa mkutano wa waandaishi wa Habari Leo Jijini Dar es salaam kuhusu umuhimu wa wananchi kulipa kodi ya mabango  ili kuchochea maendeleo katika manispaa hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Sehemu ya Usalama barabarani na mabango Manispaa ya Ilala Bw. James Batinagwa.
MAW3
Mkuu wa Sehemu ya Usalama barabarani na mabango Manispaa ya Ilala Bw. James Batinagwa (kushoto)akisisitiza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) umuhimu wa kutii sheria bia shuruti kwa kulipa kodi ya mabango kwa mujibu wa sheria na kanuni.katikati ni Afisa Uhusiano wa Manispaa hiyo Bi Tabu Shaibu na kulia ni Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari MAELEZO bi Zamaradi Kawawa.
MAW4
 Baadhi ya waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa manispaa ya Ilala na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam ulioenga kueleza mikakati ya Manispaa hiyo katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Azam FC Bocco, Kingue, Sure Boy ni Majeruhi

Posted by Esta Malibiche on JAN 31,2017 IN MICHEZO

BAADA ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, kuanza rasmi mazoezi jana jioni kujiandaa na mchezo ujao dhidi ya Ndanda, daktari wa timu hiyo, Mwanandi Mwankemwa, amezungumzia hali za kiafya za baadhi ya wachezaji waliokuwa majeruhi.
Wachezaji wa Azam FC waliokuwa majeruhi ni nahodha John Bocco ‘Adebayor’, Stephan Kingue waliopata majeraha ya misuli ya paja kwenye mchezo uliopita wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) dhidi ya Simba, ambao matajiri hao walishinda bao 1-0 lililofungwa na Bocco.
Wengine wanaouguza majeraha, ambao waliukosa mchezo huo ni kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’, kipa Mwadini Ally (nyama za paja) na beki Shomari Kapombe, ambaye ni mgonjwa lakini hivi sasa akiendelea vema.
Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz mara baada ya mazoezi ya jana, Mwankemwa alisema kuwa Bocco na Kingue watakaa nje ya dimba kwa muda wa wiki mbili tokea jana, huku Sure Boy akitarajiwa kuanza rasmi mazoezi leo na Mwadini akipumzishwa kwa siku tatu kuanzia jana.
“Bocco hali yake inaonekana kuimarika vizuri tokea alipopata majeraha hayo ya kuchana msuli wa nyuma ya paja, Stephan (Kingue) kwa upande wake naye amechana msuli wa mbele ya paja, hivyo wote watakaa nje ya dimba kwa muda wa wiki mbili kutoka sasa (jana) na wataanza mazoezi mepesi baada ya wiki moja,” alisema.
Daktari huyo bingwa mzoefu, alisema hali za wachezaji wengine ziko vizuri kabisa kuendelea na mikikimikiki ya maandalizi kuelekea mechi zijazo za ligi pamoja na michuano mingine.

Wanaotengeneza vyombo feki vya muziki, matangazo vya Candy wabainika


Posted by Esta Malibiche on JAN 31,2017 IN BURUDANI

kibo1
Mkurugenzi wa Kampuni ya Uhuru Music (T) Ltd, Maneno Sanga (kulia), akiwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Hualang Electric ambao ndio watengenezaji wa vyombo vya muziki vya Candy, Yang Hongwei wakati wa kusaini mkataba wa kibiashara wa kusambaza vyombo vya muziki na matangazo vya kampuni hiyo kwa nchi za tano za Afrika Mashariki.
kibo2
Baadhi ya vyombo vya muziki na matangazo vya Candy ambavyo vinasambazwa nchini na kampuni ya Uhuru Music (T) Ltd.
kibo3
……………………………………………………………………………
Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Kampuni ya kusambaza vifaa vya muziki na matangazo ya Uhuru Music (T) Ltd, ya jijini Dar es Salaam, imewaonya matapeli wanaoghushi nembo ya vyombo vya muziki na matangazo vya Candy kuwa siku zao zinahesabika na wakati wowote watakumbana na nguvu za dola baada ya mbinu wanazotumia kufanya utapeli huo kubainika.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Maneno Sanga ilisema kuwa kikosi kazi cha kampuni hiyo kimegundua njia wanazotumia matapeli hao ambao ni pamoja na kutengeneza vyombo vya muziki na matangazo nchini kwa kutumia teknolojia duni na kubandika nembo bandia ya Candy.
Alibainisha kuwa maharamia hao ambao wana karakarana zao katika maeneo ambayo wameisha yabaini, wamekuwa wakiharibu sifa ya bidhaa hizo ambazo zinatengenezwa na kampuni ya Hualang Electric Company Ltd ya China.
“Uhuru Music (T) Ltd, ndio ambao tuna mkataba wa kusambaza vyombo vya muziki na matangazo vya Candy kwa nchi tano za Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania na sio vinginevyo” alisema na kuongeza kuwa pia kuna mawakala ambao wana mikataba na kampuni yake katika kanda tofauti nchini.
Alisema wamewasiliana na mamlaka zote ikiwa ni pamoja na vyombo vya usalama kuhusiana na uhalifu huo ambao pia unaikosesha serikali mapato na kuwatia hasara wananchi kwa kuwauzaia vifaa visivyo na ubora unaotarajiwa.
Anataka watu ambao wanahitaji kununua vifaa vya muziki vya Candy kujiridhisha kwanza kabla ya kufanya manunuzi kwa kuangalia alama tatu muhimu ambazo zinavitambulisha vyombo hivyo ikiwa ni pamoja na ile ambayo ipo katika nembo ya kampuni hiyo ambayo ni kama iliyopo katika fedha za noti.
“Katika logo ya Candy ukiangalia vizuri kuna alama ya fedha ambayo inabadilika badilika na kusomeka maandishi Candy American Technology” anasema na kuongeza kuwa kama bidhaa hiyo ya Candy katika nembo yake haina hiyo chombo hicho ni feki.
Anasema utambulisho mwingine unapatikana kupitia simu ya mkononi aina za Smart kwa mteja ku-scan  alama ya siri ya biashara (Barcode) ambayo inapatikana katika bidhaa hizo na kumletea taarifa zote ikiwa ni pamoja na jina la kampuni yake ya Uhuru Music (T) Ltd.
Pia anabainisha kuwa nembo (logo) za Candy ni za chuma na wala si plastiki kama zilivyo hizo za feki hivyo ni wajibu wa wateja kuzitambua alama hizo na kukataa kufanywa dampo la bidhaa feki ninyingi ni hafifu na zisizodumu katika matumizi.
Anasema wameamua kutoa ufafanuzi huo na kuunda kikosi kazi cha kuchunguza uharamia unaofanyika baada kupokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya wateja ambao wamenunua ala za muziki zenye nembo ya Candy kwa bei ya chini, mbaya zaidi havikuwa na ubora unaotakiwa.
“Tulipofuatilia tulibaini wanapotengenezea,  mbinu wanazotumia kuwahadaa wateja na tumeshirikisha mamlaka zingine wakati wote wa ufuatiliaji” anasema na kuongeza kuwa kuanzia sasa kinachofuata ni hatua za kisheria.
Anazitaja vyombo hivyo vya muziki na matangazo kuwa ni pamoja na vipaza na vinasa sauti, vyombo vya matangazo, spika, mic kwa ajili ya kurekodi muziki, vinanda, stendi maalum za kurekodia, vyombo vya matangazo katika magari na Deck za aina mbalimbali.
Pia taa kwa ajili ya kumbi za disco, vifaa vya kuchanganyia muziki, vifaa vya studio kwa ajili ya kurekodia na bidhaa zingine ambazo zinahusiana na masuala ya muziki na matangazo.
Uhuru Music (T) Ltd, ndio wenye mkataba pia wa kusambaza vyombo hivyo vya muziki na matangazo katika nchi za Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda.

DKT. MWAKYEMBE AZINDUA RASMI OFISI ZA WIZARA YAKE MKOANI DODOMA

Posted by Esta Malibiche on JAN 31,2017 IN NEWS

dz1
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akikata utepe kuzindua rasmi Makao Makuu ya Wizara yaliyopo katika jengo la Masomo ya Biashara na Sheria katika Chuo Kikuu cha Dodoma ambako Wizara imehamia rasmi makao maku ya Serikali mkoani Dodoma
dz2
Katibu Mkuu Prof sifuni Mchome akitoa maelezo mafupi kwa Mhe. Waziri Dkt Mwakyembe mara baada ya kukata utepe na kuzindua rasmi ofisi za wizara mjini Dodoma
dz3
Katibu Mkuu Prof sifuni Mchome akitoa maelezo mafupi kwa Mhe. Waziri Dkt Mwakyembe mara baada ya kukata utepe na kuzindua rasmi ofisi za wizara mjini Dodoma
dz4
Mhe. Waziri Dkt Mwakyembe akitia saini kitabu cha wageni mara baada ya kukata utepe na kuingia ndani ya jengo la Wizara ambako alizindua rasmi ofisi za wizara mjini Dodoma
dz5
Mhe. Waziri Dkt Mwakyembe katika picha ya pamoja na watumishi na wageni wake mara baada ya kuzindua rasmi  ofisi za wizara mjini Dodoma ambako wizara imehamia rasmi mkoani Dodoma
dz6
Mhe. Waziri Dkt Mwakyembe aksalimiana na viongozi mbalimbali kabla ya  kukata utepe na kuingia ndani ya jengo la Wizara ambako alizindua rasmi ofisi za wizara mjini Dodoma
dz7
……………………………………………………………………..
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe amezindua rasmi Ofisi za wizara yake mkoani Dodoma na kuwataka Watumishi wa wizara waliohamia Makao Makuu ya Serikali, Dodoma kutekeleza majukumu yao kama inavyotakiwa.
Dkt Mwakyembe amezindua rasmi makao makuu ya Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria yaliopo mkoani Dodoma katika viunga vya Chuo Kikuu cha Dodoma baada ya wizara hiyo na watumishi wake 31 kuhamia rasmi makao makuu ya Serikali mkoani Dodoma.
Baada ya uzinduzi huo Mhe. Mwakyembe alisema kitendo cha kuhamia mkoani DODOMA ni utekelezaji wa agizo la kuhamia makao makuu ya Serikali ambalo lilitolewa mwezi Julai mwaka 2016 na hivyo watumishi wanapaswa kutekeleza majukumu yao na kuwahudumia wananchi kama walivyokuwa Dar es salaam.
Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Jaji Mfawidhi Kanda ya Dodoma, Mkuu wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kanda ya Dodoma, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Dodoma, Prof Kikula na watumishi 31 wa wizara ambao wamehamia Dodoma katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa agizo hilo la Serikali.
Awamu ya Kwanza yenye watumishi 31 wa wizara wakiongozwa na Waziri Dkt Dkt. Harrison Mwakyembe, Katibu Mkuu Prof. Sifuni Mchome na Naibu Katibu Mkuu Bw. Amon Mpanju imehamia rasmi mkoani Dodoma. Awamu ya pili na ya tatu zitafuata utaratibu ambao umewekwa na zoezi hilo linatarajiwa kukamilika mapema mwaka 2018.
Kufuatia kuhama rasmi kwa ofisi za wizara sasa mawasiliano yote yatafanywa kupitia anuani ya Katibu Mkuu Sanduku la Posta 315 Dodoma, namba ya simu ni 026 2321680, nukushi ni 026 2321679 na baru pepe ni ile ile ya km@sheria.go.tz

Serikali Yatenga Bil. 13.9 Kujenga Nyumba 1,157 za Walimu

posted by Esta Malibiche on JAN 31,2017 IN NEWS

indexNa: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma
Katika bajeti ya mwaka 2016/17, Serikali imetenga shilingi bilioni 13.9 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu 1,157 wa shule za msingi  nchini.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo ameyasema hayo leo, Mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge Viti Maalum, Mhe. Juliana Daniel Shonza juu ya mpango wa kuboresha miundombinu ya elimu vijijini kama vile nyumba za walimu pamoja na kulipa malimbikizo ya madeni ya walimu.
“ Katika bajeti ya mwaka 2016/17, Serikali imetenga shilingi Bil. 13.9 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu 1,157 kwa shule za msingi na shilingi bilioni 11.14 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 661 kwa shule za sekondari,” alifafanua Jafo.
Aliendelea kwa kusema kuwa, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMESII) imekamilisha ujenzi wa nyumba 146 kati ya nyumba 183 ambazo kila nyumba wataishi walimu Sita (6 multi-unit houses).
Aidha ameeleza kuwa ujenzi wa nyumba  hizo umegharimu shilingi bilioni 21.9 ambapo nyumba 37 zinaendelea kujengwa kwa gharama  ya shilingi bilioni 5.5 na zinategemea kukamilika tarehe 30 Aprili, 2017.
Kuhusu ulipaji wa madeni ya walimu, Jafo amesema kuwa Serikali imeendelea kulipa madeni kadri yanavyojitokeza na kuhakikiwa ambapo katika mwezi  Oktoba, 2015 Serikali ililipa madeni ya shilingi bilioni 20.12 kwa walimu 44,700 na shilingi bilioni 1.107 zililipwa mwezi February, 2016 kwa walimu 3221.

MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA NNE 2016

Esta Malibiche on JAN 31,2017 IN NEWS

  matokeo ya mtihani kidato cha nneBaraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2016 ambapo umefaulu wa jumla umeongezeka kwa 2.56% kutoka 67.53% mwaka 2015 hadi 70.09% mwaka 2016.

Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Dkt Charles Msonde amesema kati ya wanafunzi 408,372 waliofanya mtihani, jumla ya wanafunzi 277,283 wamefaulu, wakiwemo wasichana 135,859 sawa na asilimia 67.06 na wavulana 141,424 sawa na asilimia 73.26.

Kwa upande wa watahiniwa wa shule, Dkt Msonde amesema kuwa 244,762 sawa na asilimia 70.35 ya waliofanya matihani wamefaulu ikilinganishwa na wanafunzi 240,996 sawa na asilimia 67.91 waliofaulu mwaka 2015.

Kwa upande wa ubora wa ufaulu, amesema watahiniwa wa shule wenye ufaulu mzuri wa Daraja la kwanza hadi la tatu ni 96,018 sawa na asilimia 27.60

AZAM MARINE YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA MKOANI TANGA, YASHUSHA MELI ITAKAYOKWENDA PEMBA NA UNGUJA KUTOKA MKOANI TANGA

Posted by Esta Malibiche on JAN31,2017 IN NEWS


Meli Kubwa inayoweza kuingia abiria 1600, magari 50  na mizigo kwa pamoja ambayo itafanya safari zake kati ya Tanga-Unguja na Pemba ikiwa inaingia bandari ya Tanga leo wakati wa uzinduzi wake ambapo uwekezaji huo mkubwa umefanywa na kampuni ya Azam Marine ili kuwanusuru wananchi wa mkoa wa Tanga na changamoto za usafiri huo
Meli Kubwa inayoweza kuingia abiria 1600 na magari hamsini yenye mizigo kwa pamoja ambayo itafanya safari zake kati ya Tanga-Unguja na Pemba ikiwa inaingia bandari ya Tanga leo wakati wa uzinduzi wake ambapo uwekezaji huo mkubwa umefanywa na kampuni ya Azam Marine
 Meneja Mkuu wa Azam Marine Hussein Mohammed wa pili kulia akitazama namna wananchi wanavyoshuka kwenye meli hiyo itakayopunguza adha na usumbufu kwa wananchi wanaosafiri kutoka mkoani Tanga kwenda Unguja na Pemba

Meneja Mkuu wa Azam Marine Hussein Mohammed katikati akizungumza na watumishi wa mamlaka ya Bandari Mkoani Tanga wakati wa ujio wa meli hiyo kwenye bandari ya Tanga kulia ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Tryphoni Ntipi kushoto ni PRO wa Mamlaka hiyo,Moni Jarufu.
 Meneja Mkuu wa Azam Marine Hussein Mohammed katikati akisalimiana na Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga, Tryphoni Ntipi wakati wa ujio wa meli hiyo kushoto ni PRO wa Mamlaka hiyo Bi. Moni Jarufu.
Mazungumzo yakiendelea
Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ujio wa meli hiyo kulia  Mkurugenzi Mkuu wa Ulinzi na Usalama wa vyombo vya majini (SUMATRA) Kaptain Mussa Mandia
Mkurugenzi Mkuu wa Ulinzi na Usalama wa vyombo vya majini (SUMATRA) Kaptain Mussa Mandia katikati akizungumza na waandishi wa habari kushoto ni  Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed
Nahodha wa Meli hiyo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufika Bandari ya Tanga.
 Waandishi wa Habari wakiwa kazini kushoto ni Amina Omari wa Gazeti la Mtanzania katikati ni Mariam Shedafa wa Azam TV
 Vifaa vya uokozi wakati wa majanga ya ajali hivyo
 Baadhi ya Sehemu ya VIP ndani ya Meli hiyo kama inavyo onekana 

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

RC SHIGELLA AFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA VIWANDA MKOANI TANGA,AVITAKA KUONGEZA UZALISHAJI

Posted by Esta Malibiche on JAN 31,2017 IN NEWS

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigella akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye kiwanda cha kuzalishia chuma cha Mjini Tanga cha (Unique Steel Mill ) wakati wa ziara yake ya kukaagua maendeleo ya viwanda mbalimbali jijini hapa ili kuona namna ya ufanisi wake na changamoto zinazowakabili.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigella wa pili kutoka kushoto akiteta jambo na mmoja kati ya wamiliki wa kiwanda cha kuzalisha chuma cha (Unique  Steel Mill) wakati wa ziara yake ya kukaagua maendeleo ya viwanda mbalimbali jijini hapa ili kuona namna ya ufanisi wake na changamoto zinazowakabili kulia ni Mhasibu wa kiwanda hicho,Sikander Husein Omari na Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella katikati akimsikiliza kwa umakini Mhasibu wa kiwanda cha chuma cha Unique  Steel Mill Sikander Hussein Omari  wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya viwanda mbalimbali jijini hapa ili kuona namna ya ufanisi wake na changamoto zinazowakabili.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella  katikati akionyeshwa namna chuma zinavyozalishwa kwenye kiwanda cha Unique  Steel Mill) wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya viwanda mbalimbali jijini hapa ili kuona namna ya ufanisi wake na changamoto zinazowakabili kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella  katikati akitazama namna chuma zinazozalishwa kwenye kiwanda cha chuma cha Unique Steel Mill  wakati wa  ziara yake ya kukagua maendeleo ya viwanda mbalimbali jijini hapa ili kuona namna ya ufanisi wake na changamoto zinazowakabili.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga  Mhe. Martine Shigella  akitazama namna chuma akiwa amepanda kwenye chuma hizo kuona ubora wake  wakati waa  ziara yake ya kukaagua maendeleo ya viwanda mbalimbali jijini hapa ili kuona namna ya ufanisi wake na changamoto zinazowakabili.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akiangalia ubora wa nondo zinazozalishwa kwenye kiwanda cha kuzalishia chuma cha Unique Steel Mill wakati waa  ziara yake ya kukaagua maendeleo ya viwanda mbalimbali jijini hapa ili kuona namna ya ufanisi wake na changamoto zinazowakabili.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akiangalia ubora wa nondo zinazozalishwa kwenye kiwanda cha kuzalishia chuma cha Unique Steel Mill  wakati waa  ziara yake ya kukaagua maendeleo ya viwanda mbalimbali jijini hapa ili kuona namna ya ufanisi wake na changamoto zinazowakabili.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa pili kutoka kushoto akimuonyesha kitu mmoja wa viongozi wa kiwanda cha kuzalishia chuma cha Unique Steel Mill wakati wa  ziara yake ya kukagua maendeleo ya viwanda mbalimbali jijini hapa ili kuona namna ya ufanisi wake na changamoto zinazowakabili

Picha na habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

SSRA NA TRA ZAKOMBA TUZO ZA UMOJA WA AFRIKA (AU)

Posted by Esta Malibiche on JAN 31,2017 IN NEWS


Ofisa Habari wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Freddy Maro, akizungumza wakati akimkaribisha Msemaji wa Serikali kutoka Kitengo cha Mawasiliano cha wizara hiyo, Mindi Kasiga.
Msemaji wa Serikali kutoka Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mindi Kasiga, akifurahia jambo pamoja na Ofisa Habari wa wizara hiyo, Freddy Maro, wakati wa hafla ya kukabidhi Tuzo kwa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) na TRA jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Baadhi ya Maofisa wa SSRA na TRA, wakiwa katika hafla ya kikabidhi tuzo hizo za Umoja wa Afrika (AU) kwa taasisi hizo.
Msemaji wa Serikali kutoka Kitengo cha Mawasiliano cha wizara hiyo, Mindi Kasiga, akizungumza wakati wa kukabidhi tuzo za Umoja wa Afrika (AU) katika kipengele cha Ubunifu wa mradi wa kazidata ya Taifa ya Sekta ya Hifadhi ya Jamii na ushindi wa Jumla kwa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) jijini hivi karibuni.
Baadhi ya waandishi wa habari, wakiwa katika hafla hiyo ya kukabidhi tuzo hizo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Sarah Kibonde, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Taasisi yake ilivyofanikiwa kupata tuzo ya Ubunifu wa mradi wa kazidata ya Taifa ya Sekta ya Hifadhi ya Jamii, iliyotolewa na Umoja wa Nchi za Afrika (AU).
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii, Bi. Sarah Kibonde, akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhiwa tuzo hizo.
Meneja Huduma za Mlipa Kodi toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo akielezea namna Mamlaka ya Mapato ilivyofanikiwa kupata tuzo katika kipengele cha Ubunifu wa mradi TANCIS, ambao umeunganisha mifumo midogomidogo ya Forodha na kupelekea kurahisisha utoaji wa huduma na kuongeza ukusanyaji wa mapato, tuzo iliyotolewa na Umoja wa Nchi za Afrika (AU).
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Sarah Kibonde (kulia) akiwa na Meneja Huduma za Mlipa Kodi toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo.
Msemaji wa Serikali kutoka Kitengo cha Mawasiliano cha wizara hiyo, Mindi Kasiga, akifafanua mambo mbalimbali wakati wa kukabidhi tuzo hizo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Sarah Kibonde na katikati ni Meneja Huduma za Mlipa Kodi toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo.


Meneja Mifumo ya Forodha toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  Bw. Tinkasimile Felix (kushoto) akipokea tuzo ya ubunifu wa mradi TANCIS, ambao umeunganisha mifumo midogomidogo ya Forodha toka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga.




Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Sarah Kibonde, akilifurahia kombe hilo la ushindi wa jumla.
Maofisa wa SSRA, David Nghambi (kushoto) na Ally Masaninga, wakiwa wamelishikilia kombe hilo.

n JAN 2017 IN NEWS