Alhamisi, 8 Desemba 2016

WWF-TANZANIA YATOA SEMINA YA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA MAJI NA MAZINGIRAKATIKA MJI WA MAKAMBAKO

Posted by Esta Malibiche on Dec 8,2016 in NEWS

 

Afisa maendeleo  ya jamii  shirika la kuhifadhi mazingira duniani [WWF-TANZANIA] Martha Sanga amewatka wananchi kuhifadhi mazingira ili kuweza kujikinga na uharibifu wa Mazingira kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla.

 Akizngumza jana  wananchi wa mkoa wa Njombe wakati akifungua warsha  ya wadau mazingira iliyohusu kuhusu usimamizi wa wa rasilimali za maji na mazingira iliyofanyika katika mji wa makambako mkoani Njombe.

Bi.Martha alisema kuwa suala la usimamizi wa rasilimali za maji na mazingira sio la wafadhili, bali ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha mazingira yanatunzwa.
‘’’ Ninawaomba wananchi na wadau mbalimbali wa mazingira wanabudi kuendelea hata baada ya programu ya maji Ruaha kumaliza muda wake, kwani utunzaji wa mazingira ni jukumu la kila mtu.Pia  bado mapambano ya  utunzaji wa rasilimali za maji na mazingira  yanaendelea hata bila kuwepo wafadhili’’alisema Martha.

 Alisema kuwa Shirika la WWF kwa kupitia Programu yake ya Maji Ruaha (RWP) kwa kushirikiana na Bodi ya Maji Bonde la Rufiji (RBWB), halmashauri, wananchi na wadau mbalimbali wa mazingira walitekeleza mradi kwa miaka mitano wa katika usimamizi wa rasilimali za maji na mazingira ambao ulikuwa na lengo la rudisha hali ya Mto Ruaha Mkuu ili uweze kutiririsha maji kwa mwaka mzima. 
Evergris Makfura nae ni Ofisa Maendeleo ya jamii   ya jamii kutoka Shirika la WWF Tanzania kupitia Programu yake ya Maji Ruaha alitoa rai kwa wadau kuendelea kuhifadhi mazingira na vyanzo vya maji kwa kutumia dhana ya ushirikishwaji.
Makfura lisema kuwa Serikali ilishaweka sawa mahitaji ya kisheria (legal framework) kama vile kupitishwa kwa Sheria Mama ya Mazingira (2004), kutolewa kwa Sera ya Maji (Julai 2002) na Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji Namba 11 ya mwaka 2009.

Alisema lengo la Warsha hiyo ni kutathmini shughuli zilizotekelezwa na wadau mbalimbali wa mazingira kwa kipindi cha miaka mitano cha utekelezaji ulioratibiwa na shirika la WWF kupitia Programu yake ya Maji Ruaha kwa kushirikiana na Bodi ya Maji Bonde la Rufiji (RBWB).
Kwa upande wake Mhasibu wa Jumuiya ya Watumiaji Maji (WUA) katika Bonde dogo la Mto Mpando wilayani Wanging’ombe, mkoani Njombe, Roy Kadege alisema kuwa jumuiya hiyo atahakikisha inasimamia kikamilifu suala zima la usimamizi wa rasilimali za maji na mazingira.

 Kadege alisema kuwa pamoja kuwa mradi kumaliza muda wake, wataendelea kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira kwa vile vyanzo vingi vya maji vipo katika ukanda wao na ambako vyanzo vya mito vinakoanzia.Alisema kuwa kupitia programu ya Maji Ruaha, jumuiya hiyo ya watumiaji wa maji imeweza kutoa elimu ya usimamizi wa rasilimali za maji na mazingira katika vijiji 20 vinavyozunguka bonde dogo la Mto Mpando.

 Alisema kuwa baada ya kuwepo mradi huo wameweza kutunza vyanzo vya maji na kupelekea kurudisha Mto Mbarali mkoani Mbeya ambao hapo awali Mto huo ulikauka kutokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi zisizo endelevu,lakini lakini kutokana na uwepo wa mradi huo mto umeweza kurudi katika hali yake na  kutunza mazingira

 Mwenyekiti wa jumuiya ya watumia maji (WUA) katika bonde la mto Mpando Adamson Msigala alisema kuwa, ili zoezi la usimamizi wa rasilimali za maji na mazingira liiweze kuwa endelevu kila  halmashauri zinatakiwa  kutenga fedha kwenye bajeti zao kwa ajili ya shughuli za utunzaji mazingira kuliko kutegemea wafadhili.
Msigala alisema kigezo cha umaskini kisiwe chanzo cha kuharibu mazingira ni lazima watu wafanya kazi kutunza mazingira bila kusukumwa bali kwa moyo.Wakati WWF wanaleta mradi huo kwa mara ya kwanza, wananchi walikuwa wagumu kuuelewa kwa vile walikuwa wamezoea kulima kwenye vinyungu ambavyoviko karibu na  vyanzo vya maji.

“Kwa kuwa wadau wetu wa maendeleo wanamaliza mradi wao haina maana kwamba shughuli za usimamizi wa rasilimali za maji na mazingira zatasimama rahasha, sasa ni jukumu letu wananchi kwa shirikiana na halmashauri zetu kuweka mikakati yakuweza kuendelea pale wadau wetu walipoishia,” alisema Msigala.
 Ofisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Wanging’ombe, mkoani Njombe Michael Haule ambaye pia ni timu ya wawezeshaji ya wilaya (DFT) alilipongeza shirika la WWF kupitia programu ya maji Ruaha pamoja na Bodi ya Maji Bonde la Rufiji (RBWB) kwa kuwaunganisha wadau mbalimbali wa mazingira ili kuweza kupanga mipango yao kwa pamoja. 

Haule alisema kuwa siku nyingine za kunapokuwa na warsha kama hizo washirikishe na vyombo vya usalama na mahakama ili waweze kutambua jumuiya za watumia maji kuwa zipo kisheria.

 Bila kushirikisha vyombo hivyo usimamizi wa rasilimali za maji na mazingira utakuwa mgumu kwa vile kutakuwa na na mwingiliano wa shughuli baina ya vyombo hivyo na jumuiya za watumia maji. Kuna wakati fulani jumuiya za watumia maji zilikuwa zikiwakamata waharifu wa uharibifu wa vyanzo vya maji na wakipelekwa polisi wanatolewa,Kumbe kungekuwa na ushirikishaji wa vyombo hivyo na vikatambua kuwa jumuiya za watumia maji zipo kisheria wangeweza kwenda pamoja.’’’’alisema  Haule

  Hata hivyo aliongeza kuwa Bodi ya Maji Bonde la Rufiji wanapoitisha mikutano yao wahakikishe wanawaalika taasisi ya kupambana na rushwa (TAKUKURU), polisi na mahakama ili waweze kuvitambua vyombo hivyo vya watumia maji ili kusimamia kikamilifu suala zima la rasilimali za maji na mazingira.

0 maoni:

Chapisha Maoni