Ijumaa, 30 Desemba 2016

ALIYEKUWA MTUMISHI WA TANAPA ADAI KUTELEKEZWA NA MWAJIRI WAKE


Posted by Esta Malibiche on Dec 30,2016 in NEWS




Aliyekuwa mtumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha (RUNAPA), Emiliyo Mwadila Lugiriva pichani amemuomba Rais John Pombe Magufuli aingilie kati suala la madai yake ya kutelekezwa na mwajiri wake, baada ya kustaafu kwa hiari mnamo tarehe 01.07.2007. 

Akizungumza na mtandao huu wa Habari mapema leo hii, ametaja baadhi ya madai yake hayo kuwa ni pango la chumba kimoja ambacho kilihifadhi mizigo iliyoletwa Iringa na kuahidiwa kusafirishwa hadi sehemu husika yaani, Minjingu, Manyara, pango la vyumba viwili ambavyo familia ilikua ikishi mjini Iringa kabla ya kupewa nyumba nyingine kwa ajili ya familia na pango la vyumba viwili ambavyo alitumia baada kutekelezwa na mwajiri wake tangu tarehe 30.10.2007. 

Lugiriva alisema kuwa mnamo mwezi wa kumi (10) 2007 aliambiwa atasafirishwa hadi nyumbani kwake (Mijingu), lakini cha ajabu alifikishwa Iringa na kuambiwa hapo ndiyo nyumbani kwake, wakati nyumbani kwake ni Minjingu wilyani Babati, mkoani Manyara. 

Alitaja madai mengine kuwa ni posho ya kujikimu yeye na familia yake tangu kutekelezwa na mwajiri huyo pamoja na nauli kutoka Serengeti-Ruaha-Iringa-Tungamalenga-Msembe. 

Alisema kuwa aliomba kustaafu kwa hiari kutokana ya matatizo ya afya yake kwani, alikuwa anasumbuliwa na magonjwa ya kisukari, vidonda vya tumbo, macho na masikio. 

Lugiriva alizaliwa mwaka 1952 na mwaka 2007 akiwa na miaka 55, hivyo kutokana na maradhi hayo yalipelekea utendaji wake kudhoofu ndipo alipoandikia barua ya kustaafu kwa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadi za Taifa (TANAPA) kuomba kustaafu kwa hiari. 

Aidha, alisema kuwa aliwahi kuwaandikia barua ya madai Ofisi ya Wizara ya Maliasili na Utalii tarehe 31.07.2011 bila mafanikio, kwa hivyo amemuomba Rais Magufuli amsaidie katika suala lake, kwani anateseka na familia yake.

Alisema kuwa anaomba asafirishwe nyumbani kwako Mijingu wilayani babati, mkoani Manyara, kwani huko ndio alikozika wazazi wake na baadhi ndugu zake.

Alisema kuwa katika mazungumzo yake na Kaimu Mhifadhi Mkuu kupitia barua yake tarehe 03.07.2007 kuhusu haki zake, aliambiwa anastahili kupewa ‘Certificate of Service’ , malipo ya PPF (Pension) pamoja na gharama ya kusafirishwa yeye na familia yake na mizigo isiyozidi tani 1.5 hadi nyumbani kwake. 

Nipashe ilifanikwa kuongea na mmoja ya viongozi wa Hifadhi ya Taifa Ruaha na kudai kwamba madai yake (Lugiriva) wanayafahamu na kuongeza kuwa suala hilo linachanganya. 

Kiongozi huyo alidai kuwa suala la mstaafu huyo linachanganya sana kwa sababu wakati anaajiriwa alijiandikisha kuwa nyumbani kwake ni Iringa lakini baada ya kupelekwa Iringa alibadilisha mawazo kuwa kwake ni Minjingi Wilaya ya Babati, mkoani Manyara. 

Alisema kuwa bwana Lugiriva ametembea sehemu mbalimbali kuhusu suala lake ameenda mpaka mahakamani lakini bado hajaridhika na majibu yake. 

Naye Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Ruaha, Dk. Christopher Timbuka  akiongea kwa njia  simu alisema suala hilo kuhusiana mtumishi huyo linaeleweka na kwa sasa   lipo mikono mwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa linashughulikiwa.

Alisema kuwa masuala waliyamaliza na mkuu wa mkoa na bawana hiyo  aliapa kuwa kwao ni Iringa na sio Mijingu kama anavyodai mtumishi huyo.

Kuhusu suala la certificate of service nalo alisema kuwa hilo lipo juu  hawezi kulisemea.

0 maoni:

Chapisha Maoni