Ijumaa, 30 Desemba 2016

MBUNGE WA JIMBO LA KILOLO MWAMOTO ,ACHANGIA MILIONI 6 KUKARABATI SHULE


Posted by Esta Malibiche on Dec 30,2016 in NEWS
Mbunge  wa  Kilolo Venance  Mwamoto (wa  pili kulia)  akitoka kukagua  shule  ya Msingi Mazombe  ambayo ni  shule  aliyosoma  aliyekuwa  mbungbe  wa  jimbo la  Kilolo Prof Peter Msola na kuahidi  kuikarabati  upya  shule   hiyo  kutokana na uchakavu iliyonao
Hili  ndilo  jengo  lenye  mwonekano mzuri Mazombe shule ya Msingi
Mtendaji wa kijiji  cha Ikula Patricia Nyomolelo  akimsikiliza mbunge Mwamoto
Familia ya mwalimu  wa  shule ya Msingi Ikula  ikiwa  nje ya  nyumba yao
Mbunge  wa  Kilolo Venance  Mwamoto  akiwa ameshika kiuno baada ya  kuonyeshwa  nyumba  anayoishi mwalimu mkuu wa  shule ya msingi Ikula  wilaya ya  Kilolo ambayo  madirisha  yake  yamewekwa mabati na  kuahidi kuziboresha  nyumba   hizo jana  wakati wa ziara  yake ya  kukagua miradi ya maendeleo katika  shule   hiyo
Mbunge  Mwamoto  akisalimiana na walimu wa Ikula  waliokuwa ndani ya  nyumba  yao
Mbunge  Mwamoto wa tatu  kulia  akitazama mchezo kati ya  Simba na Ruvu pamoja na  wapiga kura wake
Mwalimu  wa shule ya Msingi Ikula akiwa na mbunge Mwamoto 
Na MatukiodaimaBlog 
MBUNGE  wa  Kilolo mkoani  Iringa amechangia kiasi cha Tsh  milioni 1 kwa  ajili ya  ukarabati  wa  shule  ya  Msingi Mazombe ambayo   viongozi mbali  mbali  wamesoma katika  shule   hiyo akiwemo aliyekuwa  mbunge wa   jimbo hilo kabla yake Prof Peter Msolla  huku kiasi cha Tsh  milioni milioni 7  zikitolewa kwa  shule ya Kiheka  sekondari  na shule ya msingi Ikuvala kwenye kata ya  Nyalumbu  inayoongozwa na  diwani wa chama  cha  Demokrasia na maendeleo (chadema)

Mwamoto  ambaye  katika ziara  yake  ya ukaguzi wa  miradi ya maendeleo  inayoendelea  katika  jimbo  hilo la  Kilolo ametumia  kiasi cha  Tsh milioni 45  za  mfuko  wa  jimbo  kuunga mkono  jitihada mbali  mbali za  wananchi wake  alisema kuwa  huu si  wakati wa siasa ni  wakati wa  kuwatumikia wananchi wote  bila  kuwabagua kwa itikadi za  kisiasa .

Akizungumza na  uongozi wa shule ya Msingi Mazombe jana  baada ya  kufanya ziara ya ghafla shuleni hapo  kukagua  shule   hiyo alisema haitapendeza   kuona anaitelekeza shule   hiyo ambayo  ni  shule  aliyosoma mtangulizi wake katika  ubunge Prof Msolla hivyo  kuahidi kuikarabati vizuri  na  kuwa  shule  yenye ubora  kama  shule  nyingine .

“Natambua  mchango  wa Prof  Msolla katika wilaya ya  Kilolo na Taifa   itakuwa  si busara  kwangu kama mbunge  kushindwa  kuikarabati  shule  hii ya Mazombe …..naomba  ukarabati  uanze  mara  moja kwa  kuweka  madirisha  na  sakafu nzuri  nje  ya hii ambayo ni mashimo mashimo” alisema  mbunge  huyo

Kuwa  kwa  ajili ya kuonyesha kuwa  huu ni  wakati wa kazi kwa kila  kiongozi  kuwatumikia  wananchi  bila  kuwabagua kwa itikadi  zao amefika katika ya  Nyalumbu  ambayo ni moja kati ya kata  mbili  za  wilaya ya Kilolo zinazoongozwa na  madiwani wa  Chadema  na  kuchangia  miradi ya maendeleo inayoendelea katika kata   hiyo .

Hivyo  aliwataka  wananchi  na  wanasiasa  katika  wilaya ya  Kilolo kwa  sasa  kuungana pamoja  kuleta maendeleo  kwani  huu si wakati wa siasa  ni wakati wa  wanasiasa  kuwatumikia wananchi  wao kwa  vitendo  si maneno  .

Katika  shule ya msingi Ikula  mbunge  huyo amechangia Tsh  milioni 1 ili  kukamilisha  ujenzi  wa  vyoo vya  wanafunzi shuleni hapo huku  akieleza  kusikitishwa na mvutano wa madaraka katika  kijiji   hicho   na kupelekea  wananchi  kushindwa  kuendelea na ujenzi wa nyumba ya  mwalimu  kwa  zaidi ya miaka  miwili  sasa  nyumba  kutokamilika .

Hivyo  alisema atamjulisha mkuu  wa  wilaya na  mkurugenzi ili  kufika  kutatua mgogoro  huo na  kuona namna gani Halmashauri  inaweza  kuunga mkono  jitihada za  wananchi hao hasa  kumalizia nyumba hiyo na wodi ya  wazazi japo kwa  upande  wake  ameahidi  kutoa bati za  kuezekea nyumba  hiyo ya  mwalimu  itakapomalizika.
 
Mwakilishi  wa  mkurugenzi  mtendaji  wa Halmashauri ya  Kilolo Henry Kaywanga  alisema kuwa  Halmashauri  ya  Kilolo  imechangia miradi mbali  mbali ya maendeleo ya  wananchi  kiasi cha Tsh milioni 120 zilizotumwa kama  ruzuku ya  serikali  (LGDG-CDG) .
Alisema  baadhi ya maeneo  miradi imekuwa  ikisuasua  kutokana na migogoro  ya viongozi  na kuwa  jitihada za  kufika katika maeneo  hayo yenye  migogoro  zimekuwa  zikifanyika na katika  kijiji cha Ikula watafika  kushughulikia mgogoro huo.
 Image result for DC Kilolo
Mkuu  wa  wilaya ya  Kilolo Asia Abdalah  akizungumza na  mwandishi  wa habari  hizi kwa  njia ya  simu  juu ya ombi la wananchi  wa  Ikula  kutaka  kufika  kumaliza tofauti zao  alisema  kuwa toka  ameteuliwa  kuwa  mkuu wa  wilaya ya  Kilolo na mheshimiwa Rais Dkt  John Magufuli amekuwa  hakai ofisini  kila siku ni kuzungukia wananchi vijijini na  kuwa  kijiji  hicho ni miongoni mwa  vijiji ambavyo vipo kwenye  ratiba  wakati  wowote  kuanzia sasa atafika .
 
Alisema  kuwa  kuna baadhi ya maeneo alifika  na kutoa maagizo ya  kukamilisha  miradi na  tayari miradi  husika  imekamilishwa  na kutolea  mfano  kijiji  cha Mahenge  wanafunzi wa  awali  shule ya msingi Mlowa  walikuwa  wakisomea chini ya mti na katika ziara yake  alitoa agizo la  kujenga vyumba  viwili  vya madarasa ndani ya mwezi mmoja na wananchi  wamekamilisha ujenzi huo ndani ya  wiki tatu pekee.

0 maoni:

Chapisha Maoni