Ijumaa, 2 Desemba 2016

KUELEKEA MABADILIKO BARAZA LA WADHAMINI LA KLABU YA SIMBA,LAZUIA MKUTANO ULIOITISHWA NA VIONGOZI WA SIMBA TAREHE 11-12-2016.

Posted by Esta Malibiche on Dec 2,2016 in MICHE

kilomoni

Baada ya wanachama wa klabu ya Yanga kwenda mahakamani kuzuia Mkutano ambao uliitishwa na Mwenyekiti wao Yussuf Manji kwani walikuwa hawakubaliani na mchakato mzima wa mabadiliko juu ya kukodishwa timu yao hatimaye Leo upande wa pili ambao ni kama ni kulwa na Dotto ameibuka na kauli yao kupitia Baraza la wadhamini la klabu ya Simba SC limeweka kikwazo katika mchakato wa mabadiliko ya uendeshaji katika klabu hiyo yenye maskani yake mtaa wa Msimbazi Dar es Salaam.

Taarifa kwa vyombo vya habari ambayo imetolewa  na mmoja wa wajumbe wa baraza hilo Mzee Hamis Kilomoni inapinga hoja ya mabadiliko ya mfumo wa uendeshwaji wa klabu hiyo.

Tazama mambo ambayo yaliyotolewa na na mdhamini huyu kwa kupitia nakala yake:

● Swala la mabadiliko limegawa wanachama na kupandikiza chuki miongoni mwao kufikia hatua ya kupigana na kutozikana.

● wanachama hawakupewa taarifa ya mabadiliko kama agenda ya 9 ya mkutano wa tarehe 31/7/2016 ilivyosema.

Hivyo basi Baraza hilo la wadhamini ambao ndiyo wana mamlaka na mali za Simba SC imeamua kufanya yafuatayo:

1.Kuzuia mkutano wa tarehe 11/12/2016 ulioitishwa na Viongozi wa Simba mpaka uhakiki wa wanachama ufanyike kupitia kwa msajili.

2. Kutolewe elimu ya mfumo pendekezi ya uendeshaji kwa wanachama wote kupitia matawi yao.

3. Kumwomba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda kusimamisha mkutano huo wa tarehe 11/12/2016  kwani kuna dalili za uvunjifu wa amani.

4. Kuiomba Serikali kuingilia kati mgogoro huu kwa ajili ya usalama wa nchi.

0 maoni:

Chapisha Maoni