Alhamisi, 8 Desemba 2016

DK.KALEMANI;IFIKAPO 2020 VIJIJI, KAYA ZOTE NCHINI KUWA NA UMEME

Posted by Esta Malibiche on Dec 8,2016 in NEWS

Akizungumza na wananchi wa vijiji vya Sadani wilayani Mufindi na Ng’uruwe wilayani Kilolo kwa nyakati tofauti jana, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani ili mwananchi aweze kuunganisha umeme katika nyumba yake atalazimika kulipa Sh 27,000 tu.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani alisema Se rikali imeliagiza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kujiandaa kusambaza wataalamu wake katika vijiji visivyo na umeme, watakaofanya usajili wa wananachi wanaotaka kuunganishwa na nishati hiyo.

''Vijiji 7,873 kati ya vijiji 12,268  Tanzania Bara vinatarajiwa kuunganishwa na nishati ya umeme kupitia utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu unaofanywa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ndani ya miaka mitano.''alisema Mh.Kalemani

0 maoni:

Chapisha Maoni