Ijumaa, 30 Desemba 2016

MGANGA WA TIBA ZA ASILI ATATUA CHANGAMOTO YA MAJI NJOMBE

Posted by Esta Malibiche on Dec 30,2016 in NEWS




MGANGA mkogwe wa tiba Ya asili wa wilayani Njombe mkoani Njombe, Dk Antony Mwandulami akionyesha chanzo cha maji alichokihifadhi na kukitumia kusambaza maji kwa wananchi wa  kijiji chake cha Itunduma, wilayani humo.






 MGANGA mkogwe wa tiba ya asili wa wilayani Njombe mkoani Njombe, Dk Antony Mwandulami akionyesha kituo cha kuchotea maji baada ya kuifadhi chanzo cha maji na kuamua   kuyasambaza maji hayo  kwa wananchi wa  kijiji chake cha Itunduma, wilayani humo.




Dk Antony Mwandulami ambae ni  Mganga  mkogwe wa tiba za asili wa wilayani Njombe mkoani Njombe  ametumia zaidi ya Sh Milioni 65 kumaliza tatizo  la  upatikanaji wa maji lilikuwa likiwakabili   wananchi wa  kijiji  cha Itunduma, wilayani humo.

Akizungumza na Mtandao huu wa Habari ulipomtembelea juzi  kijijini na kufanya mahojiano maalum kuhusu namna alivyopambana na hatimae  kufanikiwa kutatua changamoto hiyo ya maji alisema; akiwa mkazi  wa kijiji hicho aliguswa sana na tatizo la ukosefu wa maji na ndipo alipoamua kukifufua chanzo cha maji hicho kilichopo mita 200 kutoka brabara kuu ya Njombe Makambako.

Dkt.Mwandulami alisema chanzo hicho chenye chemichemi nyingi kilikauka kutokana na kukithiri kwa shughuli za kilimo, ufugaji na ukataji wa miti.

 “Nilianza kwa kutumia zaidi ya Sh Milioni 18 kukirudisha chanzo hicho katika hali yake ya kawaida na kwa kushirikiana na serikali ya kijiji tukakihifadhi na kukilinda hadi kikaleta mafanikio yote hayo,” alisema Mwandulami

 Alisema baada ya kuanza kutiririsha maji alilazimika kujenga bwawa pembeni yake, akapandikiza samaki wa aina mbalimbali na kujenga njia za maji za kisasa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji.
“Mbali na bwawa hilo kuwezesha usambazaji wa maji majumbani na mashambani lakini limetoa ajira inayowaongezea kipato vijana wanaojishughulisha na uvuvi.Alisema Mwandulami 

Aidha alivitaka vijiji vyenye changamoto ya maji viende kijijini hapo vikajifunze namna bora na rahisi ya kuhifadhi na kulinda vyanzo vya maji kwa manufaa yao na ya vizazi vijavyo akisema maji ni uhai na ni maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji hicho,  Medson Nyagawa alisema kabla ya kushughulikia changamoto hiyo  wananchi wa kijiji hicho walikuwa wanatembea umbari mrefu  kutafuta maji.
 Nyagawa alisema kuwa baada ya tatizo hilo kuwasumbua kwa muda mrefu Dk Mwandulami aliamua kutumia fedha zake kuhifadhi na kuanza kukilinda chanzo cha maji cha Nyhengeza, alichimba bwawa katika chanzo hicho, alipeleka umeme na pampu ya kusukuma maji na akajenga tenki lenye uwezo wa kuhifadhi lita 32,000 za maji.

 “Pamoja na kujenga tenki hilo akatengeneza mtandao wa kusambaza maji kwa wananchi na kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji,” alisema huku akimshukuru mganga huyo kwa mchango huo kwa jamii inayomzunguka’’.Alisema Nyagawa

 Mmoja wa vijana anayefanya shughuli ya uvuzi katika bwawa hilo, Samsoni Mwinami alimshukuru Dk Mwandulami akisema mchango wake huo, umemuhakikishia kupata wastani wa Sh 10,000 kila siku kutoka katika shughuli yake yake ya uvuvi katika bwawa hilo. 

0 maoni:

Chapisha Maoni