Jumatatu, 12 Desemba 2016

TIMU YA WANAHABARI IRINGA YAIGAGADUA CDTI , SHETANI AJIINUA MDEGELA CUP VURUGU ZAVUNJA MCHEZO

Posted by Esta Malibiche on Dec 12,2016 in NEWS

Wachezaji wa  timu ya wanahabari Iringa  wakiwa katika  picha ya pamoja kabla ya  kuanza kwa  mchezo  wao na chuo cha CDTI
Timu ya  CDTI
Mchezaji  Francis Godwi  mzee wa matukiodaima aliyeipatia ushindi timu ya  waandishi wa habari kwa  kufunga goli la kichwa  na kufanya kuibuka na ushindi wa goli 3-2 dhidi ya CDTI 
.............................................................
Na  MatukiodaimaBlog

TIMU ya  soka ya  wanahabari mkoani  Iringa  IMFC) imezidi  kutoa  kichapo kwa timu inazokutana nazo  baada ya  jana  kuidhibu vikali timu ya chuo  cha maendeleo ya jamii (CDTI) Ipogolo Iringa kwa  jumla ya magoli  3-2  hivyo kujiweka  sawa kwa mchezo  wake wa kirafiki kati ya washindi wa kombe la Spanest 2016 utakaopigwa jumapili  kwenye uwanja wa hifadhi ya Taifa  Ruaha .

Humu mashindano ya Mdegela Cup yakirugugika baada ya pepo kujiinua katikati ya mchezo kati ya usharika wa kanisa  kuu ya Mkimbizi kwa wachezaji kuacha kucheza mpira na kuanza kuchapana ngumi .


Katika  mchezo  huo   wa  kirafiki  uliochezwa kwenye uwanja wa chuo  cha CDTI Ipogolo  mchezo uliokuwa kwa ajili ya  kujiandaa na mchezo  wake na mabingwa wa mashindano ya Spanest Cup 2016    timu ya  KItisi Fc , wanahabari  waliweza  kuonyesha  soka lenye upinzani mkali kwa  wanachuo  hao kiasi cha wachezaji wa timu ya  chuo  kuonyesha jazba kwa  kucheza rafu dhidi ya  wanahabari hao .

katika  mchezo  huo hadi dakika ya 80 kipindi cha  pili  timu  zote  zilikuwa  sare ya  goli  2-2 kabla ya  wanahabari kufanya mabadiliko kwa  kumuingiza mchezaji Francis Godwin ambae ni mwandishi wa gazeti hili mkoani Iringa na  kufanikiwa  kufunga goli la  ushindi dakika ya 85 kipindi hicho cha  pili  goli  lililofungwa kwa ufundi mkubwa kwa kichwa  na  kuwaacha mashabiki na  wachezaji wa timu ya  chuo  midomo wazi.

 Hadi mwamuzi  wa  mchezo huo anapuliza  filimbi ya mwisho dakika ya 90  timu ya  wanahabari iliweza  kutoka uwanjani hapo ikiwa na furaha  kubwa baada ya  wanachuo  kushindwa   kusawazisha goli  hilo la lalasalama .

Akizungumza mara baada ya mchezo huo Fredy Mgunda mwenyekiti wakamati ya   ufundi wa  timu ya  wanahabari pamoja na  kupongeza jitihada binafsi  zilizoambatana na ufundi  mwingi  toka kwa mchezaji Godwin bado alisema  timu  hiyo toka imeanza mechi  zake za kirafiki kati ya mechi  zaidi ya tano iliyopata kucheza ni mchezo mmoja pekee ndio  walifungwa  goli moja  bila ila yote  imekuwa  ikiongoza .


Hivyo  alisema matumaini ya  timu  hiyo kuendelea  kufanya  vizuri  zaidi na jumapili  ijayo  wamejipanga  kuipokonya ubingwa  timu ya  Kitisi Fc ambao ni mabingwa wa mashindano ya kupinga ujangili ya Spanest Cup ambao watakutana na timu hiyo ya  wanahabari  Iringa .

Alisema  kwa  ujumla   timu yake  imekamilika na ipo  vizuri uwanjani na kuwa sanjari na  kuwa na wachezaji wengi  wenye vitambi ila bado wachezaji hao  ndio ambao  wanafanya vizuri  uwanjani na  wanafukuza mpira kuliko wachezaji wa  timu pinzani ambao hawana vitambi .

Wakati huo huo mashindano ya  Mdegella Cup yameingia doa baada ya mchezo kati ya timu ya usharika wa kanisa  kuu na Mkimbizi kuvunjika  kutokana na mratibu wa mashindano  kushindwa  kuzingatia kanuni  za soka kwa yeye mwenyewe  kujipa uratibu ,mwamuzi  na mchezaji  wa  timu ya Dira ambayo inashiriki mashindano hayo.

Mchezo  huo  ulioanza  kwa lawama nyingi katika  uwanja wa Gangilonga  jana kipindi  cha kwanza   kilimalizika  vizuri  pasipo vurugu  zozote  ila kipindi cha pili hali ya  utulivu  ilianza  kuonekana baada ya  usharika wa kanisa kuu kufungwa goli moja ambalo hakuna aliyepiga ila bado mmoja kati ya  wachezaji wa Mkimbizi  alimfuata mchezaji wa kanisa  kuu na kumpiga kichwa  na mchezaji mwingine  alipokwenda kuamua aliishia  kichapo hali iliyopelekea uwanja  huo kugeua ulingo wa ngumi kama dakika 5 hivi kabla ya mwamuzi  huyo ambae  kuvunja mchezo huo .


Mratibu  wa  mashindano  hayo Petro Mponzi   kuonyesha uvunjaji wa  wazi wa kanuni za soka la mashindano  hayo pasipo kushirikisha kamati ya mashindano  juu ya mchezo  huo kuvunjia aliiita timu ya Mkimbizi kati kati ya uwanja na kuipa ponti tatu jambo ambalo  limeonyesha  wazi mashindano hayo kukosa usimamizi mzuri  kutokana na mtu mmoja kuongoza nafasi zaidi ya tatu kama  uamuzi , uratibu , uchezaji  na hata kamati ya maamuzi hutoa mwenyewe .

Hadi  sasa timu ya usharika wa kanisa  kuu ipo  njiapanda  kuendelea na mashindano hayo na inataraji  kukutana wakati wowote ili  kuangalia kama  inaendelea na mashindano hayo ama  kujiondoa na  sababu  kubwa na uratibu mbovu wa mashindano hayo ambao  ulilalamikiwa toka kabla ya kuanza kwa mashindano hasa namna ya  wachezaji wanavyopatikana hali mratibu huyo akidai mtu yeyote anaweza kucheza bora awe msharika wa sharika husika  jambo ambalo lilipelekea Mkimbizi kuchukua wachezaji  wasio na maadili ya Kikristo na  hivyo kuvuruga mchezo huo

0 maoni:

Chapisha Maoni