Alhamisi, 8 Desemba 2016

KAYA 6,464 WILAYANI KILOLO ZANUFAIKA NA MPANGO WA TASAF

Posted by Esta Malibiche on Dec 8,2016 in NEWS

Afisa Maendeleo ya Jamii na Mratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Mkoa wa Iringa, William Kingazi akizungumza na walengwa wa malipo katika mpango wa unusuru kaya maskini Kijiji cha Magunguli wilayani Mufindi, mkoani Iringa hivi karibuni.
HaLMASHAURI ya Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa imefanikiwa kutekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kuanzia zoezi la utambuzi, uandikishaji, uhakiki na malipo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Hayo yamesemwa na Ofisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Kilolo, Grace Killo wakati akizungumza na mtandao huu wa Habari  [Blog ya KALI YA HABARI] katika  mahojiano maalum  kuhusu  kaya masikini zinavyonufaika na TASAF

Killo alisema kuwa jumla ya kaya maskini 6,464 zilitambuliwa na kujengewa uwezo katika vijiji 70 vilivyo kwenye mpango.

'''Ugawaji wa ruzuku katika vijiji 70 vilivyo kwenye mpango umesababisha kuongezeka kwa mzunguko wa fedha kwenye vijiji hivyo na kusababisha kukua kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi'''''alisema killo.

Alisema kuwa baadhi ya kaya nufaika zimefanikiwa kuanzisha miradi midogo midogo kwa ajili ya kukuza kipato ili waweze kujitegemea hata baada ya mradi kuisha kwa mfano; ufugaji wa kuku, mbuzi na shughuli za kilimo cha mbogamboga.

“…Uhamasishaji umefanyika ili walengwa wajiunge na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) hadi kufikia Novemba jumla ya Kaya 3,878 kati ya kaya 6,401 zilijiunga na mfuko wa afya ya jamii sawa na asilimia 60.6, uhamasishaji unaenedelea,” alisema Killo.

Alisema kuwa kaya maskini zilizotambuliwa na kuwezeshwa kupata huduma za afya, malezi, chakula na elimu mpaka sasa kiasi cha fedha zilizotolewa ni shilingi 1,602,245,272.72.

  '''Zipo changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa mpango kama vile baadhi ya Kaya kutotumia fedha kulingana na malengo ya mpango wa TASAF, kwa mfano; kutojiunga na CHF na kutoanzisha miradi midogo midogo kwa ajili ya kuongeza kipato''alisema Killo

  Hata hivyo alisema kuwa baadhi ya kaya zilishindwa kusimamia mahudhurio ya shule na kliniki kwa watoto kwa asimilia 80 kama muongozo wa TASAF unavyoelekeza.

Alisema kuwa changamoto nyingine ni pamoja na miundo mbinu mibovu ya barabara na mawasiliano ya simu kwa baadhi ya vijiji.

  Aidha aliongeza kuwa halmashauri hiyo inapokea kiasi cha fedha kisichotosheleza kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji wa mpango kwa ngazi ya wilaya na vijiji ukilinganisha na hali halisi ya mahitaji.

''''Ili kuweza kutatua changamoto hizo halmashauri inaendelea kuzijengea uwezo Kaya nufaika juu ya utumiaji wa fedha kulingana na malengo ya mpango kwa kutumia kamati za Usimamizi za Jamii (CMCs), wawezashaji ngazi ya Wilaya (PAA Facilitators), uongozi wa kijiji kwa ujumla pamoja na kusisitiza kupeleka watoto shule na kliniki''alisema '''Kaya 92kati ya 6,464 zimefariki kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kuzolota kiafya na kuwa na umri mkubwa kwa baadhi ya kaya'''alisema killo

0 maoni:

Chapisha Maoni