Ijumaa, 2 Desemba 2016

LUKUVI ATATUA MIGOGO YA ARDHI YA WANANCHI WA KASULU NA KIBONDO MKOANI KIGOMA

Posted by Esta Malibiche on Dec 2,2016 in NEWS

luku-4

Wakazi wa wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma wenye migogoro ya ardhi wakimsikiliza Mh. William Lukuvi wakati akitatua migogoro yao ya ardhi.

luku
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akipokelewa kwa maandamano na mabango na mamia ya wananchi wa kata ya Nyarubanda katika halmashauri ya wilaya ya Kigoma ambao kwa muda mrefu wamekuwa na kero ya ardhi baada ya mmoja wa wakazi wa kijiji hicho kujimilikisha eneo la serikali ya kijiji.
luku-1
Wananchi wa kata ya Nyarubanda wakimpeleka kumuonesha eneo la mgogoro Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akiwa na Mbunge wa Kigoma Vijijini Mhed. Peter Serukamba (mwenye shati jeupe).
luku-2
 Wakazi wa wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma wakiwa na nyaraka za migogoro ya ardhi walizo zileta ili kumpatia Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi aweze kuitatua migogoro yao.
luku-3
  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akitatua migogoro ya ardhi ya wakazi wa Kasulu mara baada ya kupokea malalamiko hayo.


Hassan I. Mabuye
Information Officer
The Ministry of Lands, Housing
and Human Settlements Development

Dar es salaam, Tanzania

0 maoni:

Chapisha Maoni