Jumatatu, 12 Desemba 2016

MBUNGE WA VITI MAALUM CHADEMA MKOA WA IRINGA AMPONGEZA RAIS DKT. JOHN MAGUFULI

Posted by Esta Malibiche on Dec 12,2016 in NEWS
MBUNGE wa  viti maalum  mkoa  wa Iringa Suzan Mgonukulima (Chadema) amempongeza  Rais Dkt  John Magufuli  kwa  kuwapigania wafanyabiashara  ndogo ndogo maarufu kama machinga  nchini kwa  kutaka   wasinyanyasike kuwa ndicho  kilikuwa  kilio  cha chama  cha Demokrasia na maendeleo (chadema) katika  kuona machinga hawanyanyasiki ila  ashauri  wawekewe maeneo yao .

Akizungumza  leo alisema  kuwa,  siku  zote  machinga  wamekuwa ni  watu wa  kunyanyasika katika  nchi yao   hali iliyopelekea  Chadema  wakati wa Kampeni za uchaguzi mwaka 2010  kutumia majukwaa yake ya kampeni   kueleza ni namna gani ambavyo chama  hicho  kingewapigania machinga .

Mgonukulima  alisema  uamuzi  wa Rais Dkt Magufuli  wa  kuruhusu machinga   kufanya kazi popote  bila   kufukuzwa na mtu ni uamuzi mzuri  ambao  umejibu  kilio  cha Chadema na  machinga hao ambao  walikuwa  wakinyanyasika  zaidi.

''Pamoja na machinga  kutakiwa  kufanya kazi  popote  ila  ilipendeza   serikali  kutenga eneo maalum  kwa ajili ya machinga  hao  ili  kuwawezesha  wafanyabiashara  ambao wamekodi  ofisi kwa ajili ya kufanya biashara nao   kuweza  kufanya biashara  maana  shida  iliyopo ni  wafanyabiashara   wakubwa ambao  ndio  wanaolipa kodi   mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kuyumba   kiuchumi  iwapo machinga  watafanyabiashara  nje ya maduka  yao''alisema Mgonukulima

Aidha aliongeza kuwa   inawezakana  kukawa na muda ama  siku maalum kwa  machinga  kufanyabiashara  katika maeneo yaliyotengwa  ili kuwawezesha  wafanyabiashara  wakubwa nao kufanya   biashara na kama  itabaki  hivi   hivi   upo  uwezekano wa  wafanyabiashara  wakubwa  kujiingiza katika biashara ya umachinga kama njia ya  kukwepa kulipa  kodi.

0 maoni:

Chapisha Maoni