Alhamisi, 1 Februari 2018

UWT MKOA WA IRINGA WAADHIMISHA MIAKA 41 YA KUZALIWA KWA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM KWA KUGAWA VIFAA TIBA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA IRINGA VYENYE THAMANI YA MILIONI 8.3

Posted by Esta Malibiche on FEBRUARI 1,2018 IN SIASA
 Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Iringa Nikolina Lulandala akimkabidhi vifaa tiba Ofisa muuguzi msaidizi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa Bi. Victory Ntara leo hii .

Na Esta Malibiche
Iringa
UWT Mkoa wa Iringa umeadhimisha miaka 41 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM kwa kutoa Msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya Tsh. 8.3 .katika  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa, na kutembelea Wodi ya wagonjwa na kuwafarij.
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa  Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa, Nikolina Lulandala alisema kuwa lengo la kutoa vifa hvyo ni kupunmguza changamoto inayoikabili sekta ya Afya hasa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa

Lulandala alisema kuwa walifanya utafiti kwanza kabla ya kununua vifaa tiba ambavyo wamevitoa msaada ili kuweza kutatua changamoto kwenye maeneo ambayo ndio yanakumbana na changamoto husika.

“Tumeamua kufanya hivi kwa lengo la kuboresha sekta ya afya kwa kuwa tumegundua kuwa hapa kuna changamoto nyingi hivyo sisi kama  wanawake ndio maana tumeamua kutafuta wadau watusaidie kwa kuokoa maisha ya wagonjwa wanaokuja kutibiwa hapa” alisema Lulandala

Aidha vifaa tiba ambavyo wamekabidhi hospitalini hapo nipamoja na Injection Gentramicin,  boksi 1000, Nabulaiza 1, Injection Ampiliciline vipande 1000,Suction Mashine 2, box za sabuni, mafuta ya kupaka watoto na biskuti.

Alisema kuwa anaishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kufanya kazi kwa kuwafikia wananchi wa chini hasa wale wanyonge kwa kutimiza kile ambacho kilikuwa kimeahidiwa wakati wa kuomba kura za kuongoza nchi.


“Uwt Mkoa wa Iringa tunapenda kutoa pongeza za dhati kwa Mh.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwa utensdaji kazi wake ulitukuka kwa kuhakikisha kuwa Tanzania inapiga hatua ya kimaendeleo hivyo ni lazima tuonge mkono juhudi hizi kwa vitendo na leo hii tumeona tuadhimishea miaka 41 ya ccm kwa kuingalia sekta ya Afya” alisema Lulandala


Lulandala alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imefanikisha kuleta mabadiliko ya haraka katika sekta ya afya tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali hivyo wananchi wanatakiwa kuendelea kufanya kazi kwa kujituma ili kuunga mkono juhudi hizi.


“Najua kuwa mnaona kwa macho yenu kiasi gani serikali ya wamu ya tano jinsi gani huduma za afya zilivyo boreshwa na lazima tujivunie hiki kinachofanywa na Rais wetu,mimi binafsi naunga mkono juhudi hizi na ninaomba wananchi nao waunge mkono juhudi hizi” alisema lulandala


Lulandala aliongeza kuwa kuongezaka kwa hospital za rufaa kwenye mikoa,vituo vya afya kwenye kata au tarafa, zahanati kwenye vijiji na mitaa ni hatua kubwa ya kimaendeleo hivyo ndio serikali ya awamu hii inavyotekeleza vilivyo ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2015 hadi 2020.



Lakini sio afya tu hata ukiangalia saizi tunapata elimu bure ambayo inamwezesha kila mwanafunzi kusoma bure na kuhakikisha tunapunguza wimbi la wanafunzi kukosa elimu ambapo inasaidia kuwa nakizazi cha wasomi hapo baadae.


Kwa upande wake  Ofisa muuguzi msaidizi wa Hospital Rufaa ya Mkoa wa Iringa hiyo Victory Ntara aliwashukuru  UWT kwa kutoa vifaa hivyo vya tiba na kuwataka wadau mbalimbali waeweze kuiga mfano huo na hatimae chamngamoto mbalimbali za ukosefu wa vifaa tiba katika Hospitali hiyo iweze kumalizika.

“Tunaomba mtufikishe salamu kwa Rais wa serikali ya awamu ya tano kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuboresha sekta ya afya kwa kuwa hali ya sasa kila kitu kinaenda kwa wakati” alisema Ntara


 Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Iringa Nikolina Lulandala akimkabidhi vifaa tiba Ofisa muuguzi msaidizi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa Bi. Victory Ntara leo hii .
 
 Mwenyekiti UWT Mkoa wa Iringa Nikolina Lulandala akizungumza  wakati wa kukabidhi vifaa tiba kwa uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa leo hii.


Katibu wa UWT Mkoa wa Iringa Chiku Masanja akizungumza  wakati wa kukabidhi vifaa tiba kwa uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa leo 



Ofisa Msaidizi wa Hospital Rufaa ya Mkoa wa Iringa hiyo Victory Ntara aliwashukuru  UWT kwa kutoa vifaa hivyo vya tiba na kuwataka wadau mbalimbali waeweze kuiga mfano huo na hatimae chamngamoto mbalimbali za ukosefu wa vifaaa tiba katika Hospitali hiyo iweze kumaliza

 
 Mwenyekiti UWT Mkoa wa Iringa Nikolina Lulandala akimkabidhi vifaa tiba Ofisa muuguzi msaidizi wa hospital wa Rufaa ya Mkoa wa Iringa.
 Uwt wakiendelea kukabidhi ifaa tiba
 Uwt wakiendelea kukabidhi ifaa tiba
 Uwt wakiendelea kukabidhi ifaa tiba
 Uwt wakiendelea kukabidhi ifaa tiba
 Uwt iwakiendelea kukabidhi ifaa tiba
 Vifaa mbalimbali vilivyokabidhiwa na UWT Mkoa wa Iringa,kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa mapema leo hii


Vifaa mbalimbali vilivyokabidhiwa na UWT Mkoa wa Iringa,kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa mapema leo hii










 



















0 maoni:

Chapisha Maoni