Jumatatu, 5 Februari 2018

MENEJA WA NSSF MKOA WA IRINGA JOSEPHAT KOMBA AWATAKA WANAJESHI WASTAAFU KUJIUNGA NA MFUKO HUO


 Posted by Esta Malibiche on februari 5,2018 IN NEWS
 Meneja wa NSSF Mkoa wa Iringa Josephat Komba akizunguumza na wanajeshi wastaafu katika kikao kilichofanyika mkoani Iringa na kuhudhuliwa na Mwenyekiti wa Chama cha wanajeshi wastaafu MUWAWATA.



Na Esta Malibiche
Iringa

WANAJESHI wastaafu mkoani Iringa wametakiwa kujiunga na mfuko wa hifadhi ya  jamii wa (NSSF) kwa lengo la kupata matibabu badala ya kutumia fedha nyingi pindi wanapostaafu.
Kilio hicho kimekuja mara baada ya kuona wanateseka kupata matibabu kutokana na hali duni ya kipato wanachokipata pindi wanapostaafu.
Akizungumza mapema leo hii na baadhi ya wanajeshi hao kwenye ukumbi wa hol fare uliopo mkoani Iringa Meneja wa NSSF mkoa wa IringamJosephat Komba alisema kuwa  lengo la NSSF inatoa huduma ya matoibabu kwa wanachama kwa bei nafuu,ambapo kila Mwanachama anatakiwa kuchangia kiasi cha Tsh.20  elfu,ukilinganisha na kutibiwa kwa kawaida.
Akizungumzia hali halisi ya wanajeshi wastaafu ambao wanaendelea kusubiri mafao yao alisema kuwa mpaka sasa waliokamilisha usajili ni wanachama 67 pia wanachama 22 fomu zao zipo kwenye mchakato wa kusajiliwa.
‘’Malengo yetu kama NSSF kwa Mkoa wa Iringa ni kufikia wanachama 500.Kwa sasa mwamko wa wanajeshi wastaafu kujiunga ni mdogo tunaendelea kutoa Elimu kpitia muunganiko wao ili  waweze kujiunga
Komba alisema kuwa NSSF  inatoa  mafao mbalimbali kwa wastaafu yakiwemo     Mafao ya matibabu,Fao la msaada wa mazishi kwa kugharamia  mazishi yote ndani ya Mkoa husika.Pia katika msaada wa  mazishi mtu anaehudumiwa ni yule aliyejiunga tu na si vinginevyo,pamoja na fao la urithi’’Alisema Komba
    Asseid Mayugi ni Mwenyekiti wa Chama cha wanajeshi wastaafu Muwawata,akizungumza alisema kuwa wanajeshi hao wamekuwa ajili ya matibabu  matibabu badala ya kutumia fedha nyingi  katika matiabau ukilinganisha na hali duni ya kipato walichonacho.
Mayugi alisema  kuwa hali ya wanajeshi  wastafu kwa sasa ni duni hivyo wanashindwa kupata matibabu kutokana na gharama kubwa ,hivyo aliwataka kujiunga na mfuko wa Nssf ili waweze kupata matibabu kwa bei nafuu.
Mayugi alisema kuwa  wanajeshi hao wamekuwa wakiishi katika mazingira magumu tasngu kustaafu kwao kutokana na hali ya kiuchumi ambapo kwa hivi sasa hutumia pesa nyingi katika matibabu.
Kwa upande wake,katibu wa Muwawata Auguto Sabagi alisema kuwa   wastafu wajeshi wanatakiwa kusaidiwa kutokana na Mchango wao walioufanya kwa Taifa.
‘’Ninawaomba wanajeshi wajiunge na chama hiki ili waweze kunufaika na fursa zinazopatikana’’Alisema Sabagi



 Meneja wa NSSF Mkoa wa Iringa Josephat Komba akizunguumza na wanajeshi wastaafu katika kikao kilichofanyika mkoani Iringa na kuhudhuliwa na Mwenyekiti wa Chama cha wanajeshi wastaafu MUWAWATA
 Mwenyekiti wa Chama cha wanajeshi wastaafu MUWAWATA,Asseid Rajabu Mayugi akizunguumza na wanajeshi wastaafu katika kikao kilichofanyika mkoani Iringa na kuhudhuliwa na Mwenyekiti wa Chama cha wanajeshi wastaafu MUWAWATA
 Wanajeshi wastaafu wakiwa katika kikao













0 maoni:

Chapisha Maoni