Alhamisi, 1 Februari 2018

UVCCM MKOA WA IRINGA YAADHIMISHA MIAKA 41 YA KUZALIWA KWA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM KWA KUCHANGIA DAMU KATIKA HOSPITALI YA MUFINDI, YAVUNA WANACHAMA WAPYA 120

Posted by Esta Malibiche on Februari 1,2018 IN SIASA
Na Esta Malibiche
Mufindi
JUMUIYA  ya Umoja wa vijana ccm Mkoa wa Iringa imeadhimisha miaka 41 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM kwa kufanya usafi katika Hospital ya wilaya ya Mufindi, kuwaona na kuwafariji wagonjwa kwa kutoa vifaa mbalimbali Pamoja na kuchangia damu,ambapo zilipatikana unit 15.

Akizungumza  na mtandao huu wa Habari,[KALI YA HABARI BLOG]Mwenyekiti wa  Jumuiya ya  Umoja wa Vijana  CCM Mkoa wa Iringa, Kenani Kihongosi alisema  kuwa Lengo la kuadhimisha miaka 41 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi  kwa kuchangia damu ni kupunguza vifo vinavyokana na ukosefu wa Damu katika Hospital mara Mgonjwa anapohitajika kuongezewa Damu.
Kihongosi alisema kuwa hitaji la Damu salama katika Hospital ni kubwa,kutokana  kuongezeka kwa wananchi wanaohitaji kuongezewa damu kuwa kubwa.

Alisema kutokana na mwammo mdogo wa wananchi wanaojitolea kuchangia damu,hivyo Hospital nyingi zimekuwa zikikabiliwa na uhaba wa damu salama,hivyo aliwataka watanzania kujitokeza kuchangia damu ili kupunguza wimbi kubwa la vifo  vinavyotokana na ukosefu wa damu.

 ‘Hospital zetu zina kabiliwa na changamoto ya uhaba wa damu salama kutokana na ongezeko la watanzania hasa watoto akina mama wanaopoteza damu wakati wakujifungua,na majeruhi wanaotokana na ajali wapotaka kuongezewa damu lakini inashindikana kutokana na uhaba wa damu hivyo hupoteza maisha.

Tumeshuhudia  matukio mengi ya ndugu zetu wakipoteza maisha yao kwa kukosa damau, na wengine wakifikishwa Hospitalini wanakosa hata chupa moja ya damu na hatimae kupoteza maisha,hivyo jukumu la kuchangia damu ni la kila mtanzania ili kupunguza wimbi hili la ukosefu wa damu katika Hospital zetu na hatimae kupunguza au kumaliza kabisa  vifo vinavyotokana na ukosefu wa damu,kwa kuchangia damu tutakuwa tumewaokoa watanzania wenzetu’’Alisema Kihongosi na kuongeza kuwa

‘Sisi kama vijana tumaeamua tuadhimishe miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi kwa kuchangia damu ili tuweze kuokoa uhai wa watanzani’’Alisema Kihongosi.
Akizungumza katika Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi,Kenanai Kihongosi  aliitaka Halmashauri kuhakikisha asilimia 5 ya vijana inyotokana na makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri inawafikia  walengwa kwa wakati na si vinginevyo.

 ‘’Ninakuomba Mkurugenzi  uwasimamie maafisa maendeleo  wa wilaya wa hakikishe  wanatoa Elimu kwa Vijana  juu ya uundaji wa vikundi ili waweze kunufaika na mikopo hiyo.
Pia  aliwataka watumishi wa  kufanya kazi kwa weredi na bidii ili kuendana na kasi ya Seriakali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dakta John Magufuli

‘’Kwa mtumishi ambae anaona hwezi kuendana na kasi ya Serikali hii ya awamu ya tano ni bora akatupisha ili waachie wengine amabao watakuwa tayari kuendana na kasi hii’’Alisema Kihongosi.
Aidha Uvccm Mkoa wa Iringa kwa Pamoja wamempongeza Mh.Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta John Magufuli kwa  kazi kubwa anayoifanya ya kuwatumikia watanzania bila kujali itikadi za vyama vyao,huku akitekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi CCM,huku wakiwaomba watanzania waendelee kumuombea kila iitwapo leo.


Wakati huo huo wanachama wapatao  120 wapya waliojiunga na chama cha Mapinduzi  katika maadhimisho hayo walikabdhiwa kadi na kuapishwa.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umovja wa Vijana CCM Mkoa wa Iringa Kenanai Khongosi akichangia Damu katika Hospital ya Wila ya Mufindi jana wakati wa maadhimisho ya miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi ccm yaliyofanyika,ambapo Uvccm Mkoa wa Iringa Iliadhimisha kimkoa wialayani Mufindi. jana.

Katibu wa Jumuiya ya Umovja wa Vijana CCM Mkoa wa Iringa James Mgego akichangia Damu katika Hospital ya Wila ya Mufindi jana wakati wa maadhimisho ya miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi ccm yaliyofanyika,ambapo Uvccm Mkoa wa Iringa Iliadhimisha kimkoa wialayani Mufindi. jana.

Katibu wa Jumuiya ya Umovja wa Vijana CCM Mwialaya ya Mufindi  akichangia Damu katika Hospital ya Wila ya Mufindi jana wakati wa maadhimisho ya miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi ccm yaliyofanyika,ambapo Uvccm Mkoa wa Iringa Iliadhimisha kimkoa wialayani Mufindi. jana.

 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umovja wa Vijana CCM Mkoa wa Iringa Kenanai Khongosi akifyeka katika eneo la Hospital ya wilaya ya Mufindi  wakati wa maadhimisho ya miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi ccm yaliyofanyika,ambapo Uvccm Mkoa wa Iringa Iliadhimisha kimkoa wialayani Mufindi. jana.
 Katibu waa Jumuiya ya Umovja wa Vijana CCM Mkoa wa Iringa James Mgego akifyeka katika eneo la Hospital ya wilaya ya Mufindi  wakati wa maadhimisho ya miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi ccm yaliyofanyika,ambapo Uvccm Mkoa wa Iringa Iliadhimisha kimkoa wialayani Mufindi. jana.
Mjumbea wa Baraza Kuu Uvccm Taifa anaewakilisha Mkoa wa Iringa, Zawadi akifanya usafi kwa kufyeka katika eneo la Hospital ya wilaya ya Mufindi  wakati wa maadhimisho ya miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi ccm yaliyofanyika,ambapo Uvccm Mkoa wa Iringa Iliadhimisha kimkoa wialayani Mufindi. jana.






 








0 maoni:

Chapisha Maoni