Ijumaa, 9 Februari 2018

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA SULUHU AUPONGEZA MKOA WA IRINGA KWA KUANZA KUTEKELEZA SERA YA VIWANDA

Posted by Esta Malibiche ON Februari 9,2018 IN NEWS
Makamu wa Rais Mama Samia Hassan Suluhu akisalimiana na Mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza mara bada ya kuwasili Mkoani Iringa,katika kijiji cha Kising'a kilichopo kata ya Kisinga'a Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya wilaya ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa.


Na Esta Malibiche
Iringa
MAKAMU  wa  Rais  wa  Jamhuri  ya  Muungano  wa  Tanzania  Samia  Suluhu  Hassan  leo hii amezindua Zahanati katika kijiji cha Kiding'a kilichopo Tarafa ya Isiman Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa.
Akizungumza na wananchi wa Iringa katika hafla fupi ya uzinduzi wa Zahanati hiyo,Mama Samia Suluhu Hassan  aliwapongeza  wadau wa Maendeleo ambao ni kampuni ya Asas group kwa kuchangia kiasi cha Mill  125  na wananachi ambaoa walichangia kiasi cha Mill 4,higyo kufikia jumla ya Mill 129  na hatimae ujenzi ukakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi,ambapo inahudumia vijiji vitatu  na kaya 129 zinanufaika na mataibabu.

Alisema kuwa kutokana na juhudi kubwa iliyofanywa na wadau wa maendele kwa kushirikiana na wananchi Serikali kwa kushirikiana na wadau wa Maendeleo itahakikisha zahanati hiyo inapanuliwa na kuwa kituo cha Afya ili    
  kiweze kuhudumia wananchi wengi zaidi hivyo kupunguza Msongamamno katika Hospital ya wilaya na Hospital ya  Rufaa ya Mkoa wa Iringa.
  “

"Ninawaomba wananchi tuendelee kushirikiana  kuchangia ili wodi nzima ya akina mama .Pia tunawashukuru wananchi kwa kupisha ujenzi wa wodi hizi mbili ya wanaume na wanawake,kilichobaki tushirikiane kea pamoja kuhakikisha tunaongeza wodi nzima ya akina mama ikiwa ninpamoja na kuipanua kiwe kituo cha Afya"Alisema Mama Samia


Aidha Makamu wa Rais alikagua upanuzi wa kiwanda cha Ivory kilichopo katika Eneo la Ipogolo Manispaa ya Iringa,na kuipongeza Kampuni ya Ivory kwa kuboresha kiwanda hicho  na kuunga mkonomjuhudi za Serikali.Pia alipongeza kwa kutoa ajira kwa vijana wapatao  150   

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Cha Mapinduzi CCM wilaya ya Iringa,aliomba Serikali kupitia Makamu wa Rais kuwasaidia wananchi wa Kising'a ususani kata Tarafa ya Isimani kutatua kero ya Maji iliyodumu kwa muda mrefu bila kutatuliwa, hasa vijiji vya pembezoni.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa Zahanati  kwa Mh.Makamu wa Rais,Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa Vijijini,alisema kuwa zahanati hiyo itahudumia wananchi wa vijiji 3,ambavyo ni Kising'a,Kinywang'anga na Igingilanyi pia jumla ya wananachi wapatao13672,wakiwamo wanaume 1943  na wanawake  229 watanufaika na matibabu katika Zahanati hiyo,ambayo inahudumiwa na wahudumu 4.

Aidha aliishukuru Kampuni ya Asas group kwa kujitoa katika Sekta ya Afya na kiboresha Afya za wananachi wa Kising'a na kuwataka wadau wa maendeleo wilayani humo,kujitolea katika sekta mbalimbali na si kuiachia Serikali pekee.
Akizungumzia  hali ya upatikananji wa matibabu ndani ya Halmashauri hiyo alisema kuwa Halmashauri hiyo inavituo vya kutolea huduma ya  Afya 76,ambapo  kati ya hivyo  vituo 65  ni Zahanati,vituo vya Afya 10  pamoja na Hospital ya wilaya 1.

"Mheshimiwa Makamu wa Rais kati ya vituo hivi,vituo 61  vinamilikiwa na Serikali na vituo..vinamilikiwa na Taasisi za mashirika ya dini na taasisi binafsi ni 15.Pia huduma za Afya ya uzazi na mtoto zinaendelea vizuri pamoja na huduma za wajawazito na huduma za kuondoa maabukizi ya vvu zinatolewa katika vituo vyote 72"" Alisema.

Aliongeza kuwa kuna pamoja na mafanikio hayo lakini wanakabiliwa na  changamoto ya uzio zunguka zahanati hiyo na pamoja na fedha kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi waliopisha eneo hilo kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya.
Makamu wa Rais anaendelea na ziara yake Mkoani hapa,ambapo kesho Februari 10 atakagua miradi ya Maendeleo katika Wilaya ya Kilolo.
Makamu wa Rais mama Samia Sulu
hu Hassan akisqlimiana na viongozi wa uswlama mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa,na kupokelwa na viongozi mbalimbali wqkiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza,ikiwa ni moja ya ziara ya kukagua shughuli za maendeleo.
Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan akisqlimiana na viongozi wa uswlama mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa, na kupokelwa na viongozi mbalimbali wqkiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza,ikiwa ni moja ya ziara ya kukagua shughuli za maendeleo.
Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan akisqlimiana na viongozi mbali!bali  mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa,na kupokelwa na viongozi mbalimbali wqkiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza,ikiwa ni moja ya ziara ya kukagua shughuli za maendeleo.
Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa,na kupokelewa na Viongozi mbalimba akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza,ikiwa ni moja ya ziara ya kukagua shughuli za maendeleo

Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan akiendelea kusaqlimiana na viongozi mbalimbali  mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa, na kupokelwa na viongozi mbalimbali wqkiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza,ikiwa ni moja ya ziara ya kukagua shughuli za maendeleo.
Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan akiendelea kusaqlimiana na viongozi mbalimbali  mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa, na kupokelwa na viongozi mbalimbali wqkiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza,ikiwa ni moja ya ziara ya kukagua shughuli za maendeleo
Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan akiendelea kusaqlimiana na wadau wa Maendeleo pamoja na viongozi mbalimbali  mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa, na kupokelwa na viongozi mbalimbali wqkiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza,ikiwa ni moja ya ziara ya kukagua shughuli za maendeleo


Mnec wa Mkoa wa Iringa,ambae pia ni Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Salim Asas akizungum leo  katika hafla fupi ya ufunguzi wa Zahanati ya Kising'a iliyofanyika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa
    Waziri  wa  Ardhi  Nyumba na maendeleo ya makazi  Wiliam Lukuvi ambae pia ni Mbunge wa jimbo la Isimani kupitia Chama cha Mapinduzi CCM   akizungum leo  katika hafla fupi ya ufunguzi wa Zahanati ya Kising'a iliyofanyika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa


Katibu wa chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akizungum leo  katika hafla fupi ya ufunguzi wa Zahanati ya Kising'a iliyofanyika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa.


Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akizungum leo  katika hafla fupi ya ufunguzi wa Zahanati ya Kising'a iliyofanyika kijiji cha Kising'a kilichopo Tarafa ya Isimani,Halmashauri ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa.





0 maoni:

Chapisha Maoni