Alhamisi, 8 Februari 2018

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA SULUHU ANATARAJIA KUANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI IRINGA KESHO,MKUU WA MKOA WA IRINGA AZUNGUMZA NA VYOMBO VYA HABARI


Posted by Esta Malibiche on FEBRUARI 8,2018 IN NEWS
Mkuu wa Mkoa wa Iringa,Amina Msenza akizungumza ofisini kakwe na vyombo vya Habari mapema leo hii,kuhusu ujui wa Makamu wa Rais,anaetarajia kuaNza ziara ya kikazi kesho Mkoani Iringa.PICHA NA ESTA MALIBICHE.

Na Esta Malibiche
Iringa
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza  amewataka wananchi wa Mkoa wa Iringa, Kujitokweza kawa wingi kumpokea  Mkamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan anaetarajias kuanza ziara ya kikazi hapo kesho.

.
Mapokezi hayo  yatafanyika kwenye kijiji cha Kising’a wilaya ya Iringa kuanzia saa 3;00 asubuhi.

Akizungumza ofisioni kwake  na Vyombo vya Habari mapema leo hii, alisema kuwa makamu wa Rais atafanya ziara ya kikazi Mkaoani hapa  kuanzia kesho tarehe 9,2,2018 na kuhitimisha tarehe 13,2,2018.

Masenza alisema katika ziara hiyo Makamu wa Rais anatarajia kukagua shughuli mbalimbali  za maendeleo zinazotekelezwa mkoani Iringa na Serikali na Sekata binafsi,vilevile atafanya mikutano ya hadhara.

‘’Ndugu wananchi wa Mkoa wa Iringa,tarehe 9,2,2018 Mheshimiwa  Makamu wa Rais  atapokelewa katika Halmashauri ya Iringa,ambapo atafungua  wodi katika zahanati ya  kijiji cha Kisinga’a,atakagua upanuzi wa kiwanda cha Ivory,atakagua kiwanda cha Ufungashaji wa mazao ya Mbogamboga ,pia atafungua barabara ya mashine tatu’’alisema Masenza ana kuongeza kuwa

‘Tarehe 10,2,2018 Mheshimiwa makamu wa Rais  ataelekea wialaya ya Kilolo ambapo atazindua jengo la utawala katika Shule ya Sekondari Kilolo na atafanya Mkutano wa hadhara kwenye mji mdogo wa Ilula.

Alisema kuwa Tarehe 11,2,2018 atakuwa wilayani Mufindi  ambako ataweka jiwe la Msingi  maabara kwenye Shule ya Sekondari Mgololo,atafungua Zahanati ya kijiji cha Mtili na kukagua kiwanda cha utengenezaji wa Mkaa Mafinga.

Masenza aliongeza kuwa tarehe 12,2,2018  Mheshimiwa makamu wa Rais atazindua   Mradi wa kuendeleza utalii ukanda wa Kusini[REGROW] ambapo Mkoa wa Iringa ni kitovu cha Utalii,ambapo uzinduzi huo utafanyika eneo la kihesa Kilolo Kuanzia  saa 2;30 asubuhi na sa 8;00 Mchana atafanya Mkutano wa hadhara katika uwanja wa mwembetogwa Manispaa ya Iringa.

‘’Ninawaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye uzinduzi  na Mkutano wa hadhara ili kwa Pamoja tupate kupokea ujumbe kutoka kwa Mheshimiwa makamu wa Rais’’Alisisitriza Masenza

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa,Amina Msenza akizungumza   vyombo vya Habari mapema leo hii,kuhusu ujuo wa Makamu wa Rais,anaetarajia kuaNza ziara ya kikazi kesho Mkoani Iringa.Kushoto kakawe ni katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Bi.Wamoja Ayubu.









0 maoni:

Chapisha Maoni