Jumatatu, 26 Februari 2018

WAHAMIAJI HARAMU 83 WAKAMATWA IRINGA WAKIWA HOI

Posted by Esta Malibiche on Fbruari 26,2018

 Wahamiaji  haramu waliokamatwa Iringa

WAHAMIAJI haramu 83 wamekamatwa na idara ya Uhamiaji kwa kushirikiana na jeshi la polisi mkoa wa Iringa jana huku baadhi yao wakiwa katika hali mbaya baada ya kukosa chakula siku tatu.

Akizungumza mara baada ya kuwafikisha katika kituo cha Polisi mkoa wa Iringa, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji  Mkoa wa Iringa, Hope Kawawa ,alisema wahamiaji hao walikamatwa katika maeneo ya kijiji cha Mbigili wilaya ya Kilolo mkoani Iringa wakiwa katika roli aina ya Scania baada ya kupata taarifa kutoka raia wema.

Kawawa alisema kuwa baada ya kupata taarifa hizo walifanikiwa kulikamata roli hilo lenye namba  T903 AKH mali ya Gabriel Mwakyambiki mwenyeji wa Tukuyu ambapo dereva alifanikiwa kukimbia na kulitekeleza roli hilo kijiji cha Mbigili.

Alisema wahamiaji hao walikamatwa majira ya saa  kumi na moja juzi jioni na maafisa wa uhamiaji kwa kushirikiana na jeshi la polisi hivyo wakiwa katika hali mbaya ambapo wengi wao walionekana wakiwa hawajapata chakula hali iliyolazimu kuwapatia kwanza huduma ya kwanza hadi hali zao zitakapotengemaa.

Alisema Kawawa alisema kuwa baada ya wiki iliyopita kuwakamata wahamiaji wanne waliendelea kufanya doria na kufanikiwa kuwakamata wahamiaji 83 juzi ambao watawafikisha mahakamani mara baada ya hali zao kuwa njema.

Aidha alitoa wito kwa wanaofanya biashara ya kuwasafirisha wahamiaji hao kuwa kwa sasa mkoa wa Iringa si mahala pa kupitisha wahamiaji bali wataendelea kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wahamiaji wote watakaogundulika mkoani hapo na wako kazini kwa masaa ishirini nne.


“Naomba niwaambie madalali wanaosafirisha hawa wahamiaji mkoa wa Iringa sio mahala salama kabisa kuwapitisha hao watu kwani tuko makini masaa 24 na pindi tukiwabaini hatua kali zitachukuliwa dhidi yao kwa kufanya biashara ya  kuwasafirisha wahamiaji hivyo wasitarajie watapita mkoa wa Iringa bila kuwakamata” alisema

Kawawa alitoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na idara ya uhamiaji kwa kutoa taarifa pindi wanapohisi baadhi ya watu sio raia wa Tanzania na watu wasiowajua kwenye vyombo vya usalama ili wachunguzwe na kuchukuliwa hatua madhubuti.
 
Kwa  upande  wake  mkuu wa mkoa  wa  Iringa Amina Masenza ambae  ni  mwenyekiti  wa kamati ya  ulinza  na usalama mkoa  wa  Iringa akizuingumza  baada ya kuwatembelea  wahamiaji  hao  ambao baadhi  yao wamelazwa katika Hospitali ya  Rufaa ya  mkoa wa  Iringa alisema kuwa mkoa  wa  Iringa umejipanga  kiusalama  na  kuwa  si rahisi  kwa  wahamiaji  kuvuka  ndani ya  mkoa  huo .

wahamiaji haramu raia wa Ephiopia wanaswa Iringa wakisafirishwa kwenye Lori 


Wahamiaji hao wakiwa hoi

0 maoni:

Chapisha Maoni