Jumapili, 4 Februari 2018

KATIKA KUELEKEA KILELE CHA MADHIMISHO YA MIAKA 41 YA KUZALIWA KWA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM TAIFA,CHAMA CHA MAPINDUZI CCM MKOA WA IRINGA KIMEADHIMISHA MIAKA 41 YA KUZALIWA KWAKE KWA KUIKABIDHI HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA MIFUKO YA SARUJI 500 NA BATI 300 KWA AJILI YA KUKARABATI MIUNDOMBINU YA SHULE.


Posted by Esta Malibiche on FEBRUARI 3,218

Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akikabidhi mifuko ya saruji kwa Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela,wakiwemo  viongozi  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.PICHA NA ESTA MALIBICHE.


Na Esta Malibiche
Iringa
CHAMA cha Mapinduzi CCM  Mkoa wa Iringa kimesherekea miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha hicho  kwa kuchangia shughuli za maendeleo katika sekta ya Elimu.

CCM Mkoa wa Iringa imekabidhi mifuko ya saruji 500 na  bati 300 kwa uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwa lengo la kukarabati miundombinu ya shule zilizochakaaa,huku ikiunga mkono juuhudi za Serikali ya awamu ya Tanao kwa vitendo.


Akizungumza na wananchi katika Shule ya Sekondari ya Mawelewele iliyopo kata ya Mwangata Manispaa ya Iringa,wakati akikabidhi bati 60 na mifukio ya Saruji 60,katibu wa Chama cha Mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa,Christopher Magala alisema kuwa chama cha amapinduzi kwa kutambua umhimu wa Elimu na Changamoto zinazoikabili seta hiyo wameona washerekee miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama hicho kwa kuiangalia sekta ya Elimu ndani ya manispaa ya Iringa.

‘Tumeamua kusherekea kwa kumuunga mkono Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM taifa,Rais Dakta John Magufuli kwa vitendo kwa kukabidhi msaada huo ili Pamoja na kuwaonyesha wananchi waliotuweka madarakani jinsi gani tunatekeleza Irani yetu kwa vitendo na si kwa mamneno tu’’Alisema Magala.
'Katika Risala ya Shule inaonyesha kuwa kuna upungufu wa walimu wa sayansi,ninawaomba walimu muwajengee wanafunzi wapende kusoma masomo ya sayansi ili tuweze kuwapata walimu wa masomo ya sayansi ili Taifa liweze kuondokana na uhaba wa walimu wa Sayansi'aliema Mgala na kuongeza kuwa
'Katika shule hii kuna kero  ya vyumba vya madarasa,Hosteli za watoto wa kike,Nyumba za walimu na Maabala,ninawaomba wananchi tuendelee kushirikiana wote bila kuiachia serikali pekee'Alisema Mgala na kuongeaza kuwa
'Sisi kama chama cha amapinduzi kwa kuonyesha njia leo tunaikabidhi Serikali vifaa hivi ili viweze kupunguza kero ya miundombinu katika shule yetu hii na Shule za Manispaa.'


Aidha Katibu wa Chama cha Mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa,aliwaongoza wanaccm kuchimba Msingi wa ujenzi wa vyumba vya amadarasa katika eneo la shule ya Sekondari ya Mawelewele.Viongozi hao walioshiriki nipamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela,Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Jmahuri David Willium,Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Iringa Mjini,Iringa Vijiji,Kilolo na Mufindi.Pia wengine walioshiriki kuchimba Msingi nipamoja na Katibu wa chama cha Mapinduzi ccm Iringa Mjini,Kilolo na Mufindi pamoja na viongozi wa uvccm Mkoa wa Iringa na wilaya zote za mkoa wa Iringa,wanachama na viongozi wa jumuiya za Chama cha Mapinduzi.

Akipokea Msaada huo,Mkuu wa wilaya ya  Iringa,Richard Kasesela alikishukuru chama cha Mapinduzi kwa majitoleo yao na kusema kuwa vifaa hivyo vitaweza kukarabati vyumba vya madarasa viwili vinavyotarajia kujengwa ambapo Msingi wakeuliozinduliwa kuchimbwa na Chama cha Mpinduzi ccm.

Kasesela aliwataka wadau wa amaendeleo wengine kujitolea ili waweze kukamilisha vyumba vya madarasa vinavyoendelea kujengwa katika shule ya Sekondari ya mawelewele pamoja na kuboresha miundombinu ya shule  zilizopo Mnispaa ya Iringa.

 Tunakishukuru Chama cha Mapinduzi kwa kuona umuhimu wa Eliimu kwa vijana wetu na hatimae mmeweza kuchangia vifaa hivi vitakavyoweza kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa uweze kukamilika,ninawaomba na wadau wengine wa maendeleo wajitikeze kuchangia’’Alisema Kasesela na kuongeza kuwa

 “Halmashauri ya manispaa ya Iringa ni yatima hivyo tunaomba chama cha mapinduzi kupitia viongozi wangu mtusaidie kufanya shughuli za kimaendeleo msiishie leo tu maanakuna vitu vingi bado havijakaa sawa” alisema Kasesela

Pia Kasesela alitoa agizo kwa mkuu wa Shule kuhakikisha masaada huo uliotolewa na Chama cha Mapinduzi utatumika kama ilivyopangwa na kuongeza kuwa kwa kiongozi yeyote atakae diriki kufanya ubadhirifu hatua za kinidhamu zitachulkuliwa dhidi yake.



Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akikabidhi mifuko ya saruji kwa Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela,wakiwemo  viongozi  wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.
Mifuko 60ya saruji iliyokabidhiwa katika Shule ya Sekondari ya Mawelewele ikiwa ni miongoni mwa mifuko 500 iliyokabidhiwa Halmashauri ya Manispaa ya IRINGA
Mifuko 60ya saruji iliyokabidhiwa katika Shule ya Sekondari ya Mawelewele ikiwa ni miongoni mwa mifuko 500 iliyokabidhiwa Halmashauri ya Manispaa ya IRINGA
Mifuko 60ya saruji iliyokabidhiwa katika Shule ya Sekondari ya Mawelewele ikiwa ni miongoni mwa mifuko 500 iliyokabidhiwa Halmashauri ya Manispaa ya IRINGA
Katibu wa Chama cha Mapinduzi ccm Mkoa a Iringa,Christopher Magala akionyesha baadha i ya bati ambazo chama kimekabidhi kwa Shule ya Sekondari Mawelewele ikiwa ni miongoni mwa bati walizokabidhi kwa  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.
 
 Mkuu wa wilaya ya Iringa,Richard Kasesela  akichimba Msingi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Mawelewele ikiwa ni moja ya kufanya kazi kwa vitendo
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi manispaa ya Iringa Said Rubeya akichimba Msingi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Mawelewele ikiwa ni moja ya kufanya kazi kwa vitendo.

 
 Mbunge waviti maalum mkoa wa Iringa kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Ritha Kabati  akichimba Msingi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Mawelewele ikiwa ni moja ya kufanya kazi kwa vitendo.
Mwenyekiti wa umoja wa vijana Mkoa wa Iringa Kenani kihongosiakichimba Msingi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Mawelewele ikiwa ni moja ya kufanya kazi kwa vitendo.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akizundgumza na wananchi kijiji cha Mawelewele katika Shule ya Sekondari ya Mawelewele mara baada ya kuhitimisha zoezi la kufantya kazi kwa vitendo kwa kuchimba Msingi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akizundgumza na wananchi kijiji cha Mawelewele katika Shule ya Sekondari ya Mawelewele mara baada ya kuhitimisha zoezi la kufantya kazi kwa vitendo kwa kuchimba Msingi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa Shule ya Sekondari ya Mawelewele
Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Halmashauri ya Mnispaa ya Iringa,wabunge wa viti Maalum ,wakuu wa wilaya na  pamoja na viongozi wa chama cha Mapinduzi.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akiwa katika picha yapamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mawelewele
 Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wanafunzi


0 maoni:

Chapisha Maoni