Alhamisi, 1 Februari 2018

MICHUANO TULIA CUP YAANZA KUTIMUA VUMBI KATA YA KIBAMBA DAR ES SALAAM

Posted by Esta Malibiche on  Februari 1,2018 IN  MICHEZO


MSHAMBULIAJI wa timu ya Kibamba Worious Emmanyel Athanas (kulia) akijitahidi kumtoka beki wa timu ya Mpakani FC, Haruna Ramadhani, timu hizo zilipopambana katika mechi ya fungua dimba ya Tulia Cup, katika uwanja wa Kibwegele, Kibamba Dar es Salaam, juzi.
MSHAMBULIAJI wa timu ya Kibamba Worious (kulia) akijitahidi kumtoka beki wa timu ya Mpakani FC, timu hizo zilipopambana katika mechi ya fungua dimba ya Tulia Cup, katika uwanja wa Kibwegele, Kibamba Dar es Salaam, juzi.
Katibu wa Kamati ya Uratibu wa Michuano ya Tulia Cup Moreen Ngasala akimkaribuisha Diwani wa Kata ya Kibamba (CHADEMA) Ernest Mgawe (kulia) baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Mpiga wa Kibwegele, katika ufunguzi wa michuano hiyo
Msanii wa kujitegemea akichangamsha Uwanja kabla ya michuano hiyo kuanza
Kibamba Warious na Mpakani FC wakiwa tayari kwa mtanange
MC akitangaza hatua mbalimbali zilizokuwa zikiendelea katika uzinduzi wa michuano hiyo
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Dar es Salaam, Elizabeth Majige aakisalimiana Katibi wa Siasa na Uenezi Kata ya Kibamba Clement Mgabo walipokutana kwenye uzinduzi wa michuano hiyo
Wadau wa friends Of Tulia wakiwa kwenye michuano hiyo
Mgeni rasmi akienda kukagua timu ili mpambano uanze
Mgeni Rasmi akisalimiana na mwamuzi wa mechi hiyo
Mgeni rasmi akisalimia wachezaji wa timu ya Kibamba Warious
Mgeni rasmi akiwa na baadhi ya viongzi baada ya kukagua timu
Timu zikiwa tayari kwa mpambano
Mmoja wa waraibu wa michuano hiyo Moreen akisoma risala
Mwenyekiti wa Friends of Tulia akizungumza kabla ya mpambano kuanza
Wadau wa Friends of Tulia wakiwa kwenye michuano hiyo
Diwani wa Kata ya Kibamba (CHADEMA),  Ernest Mgawe akizungumza kabla ya kipute kuanza. "Michezo siyo siasa, inasaidia sana kuweka jamii pamoja hasa vijana. Napongeza sana uamuzi wa kuanzisha michuano hii", alisema.
Mgeni rasmi akizungumza kufungua michuano hiyo ambayo leo kuu ni kuwaweka vijana pamoja na pia kuchangisha vifaa na fedha kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Mtaa wa Hondogo katika Kata hiyo ya Kibamba. Mgeni huyo rasmi aliahidi kuchangia mifuko mia moja ya saruji
Wadau wa Friends Of Tulia
Baadhi ya wadau wakiwa na wachezaji
Mdau wa Friends of Tulia akiwa na baadhi ya wachezaji
Mgeni rasmi akijiandaa kupiga mpira kuanshiria mechi kuanza
Mgeni rasmi akiwa ameshapiga mpira
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na timu zote
mpambano ukaanza
"vipi umenusurika?' refa akimuuliza mchezaji huku akimpapasa baada ya mchezaji wa timu ya Kibamba Warious baada ya  kuchezewa vibaya na mchezaji wa Mpakani FC
Kipa wa Mpakani FC akiuangalia mpira wakati ukiingia kimiani kufuatia penati iliyopigwa na mchezaji wa Kibamba Warious kutokana na mchezaji wa timu hiyo kufanyiwa rafu katika eneo la hatari
Mpambano ukiwa umeiva
Mdau wa Friends of Tulia akiwa na mmoja wa wasanii waliofika kuhangamsha uzinduzi wa Tulia Cup
Mwandishi wa Uhuru FM akiwa na mmoja wa wasanii waliofika kutia chachandu michuano hiyo
"Inaonekana naweza kuwa migapicha mzuri", mdau wa Friends Of Tulia akijaribu kupigapicha baadhi ya matukio kwenye michuano hiyo
Wadau wakitazama picha zao katika Blog ya taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM Blog). PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

0 maoni:

Chapisha Maoni