Jumamosi, 28 Oktoba 2017

MKUU WA WILAYA YA MBULU AMEZITAKA KAYA MASIKINI KUTUMIA KWA MALENGO KUSUDIWA FEDHA ZA TASAF

Posted by Esta Malibiche on Oct 28,2017  IN NEWS


Mkuu Wa  wilaya ya  mbulu Chelestino s Mofuga leo ,28/10/2017 atembelea kaya maskini zilizopo katika mpango wa Tasaf na kupata maelezo ya wanufaika jinsi wanavyotumia fedha hizo. Baada ya kutembelea kaya hizo amefanya mkutano na wananchi kuhamasisha uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa, na kupiga vita pombe haramu ya moshi ambaye inasababisha matukio ya uhalifu mbalimbali.
Pia mkuu wa wilaya ameonya vikali wanaopata fadha za Tasaf na kunywa pombe, kuolea wake wa pili badala ya kuanzisha miradi na kusomesha wastoto.


Aidha baadhi ya wanufaika wamekiri na kusema kuwa fedha za Tasaf ni mkombozi katika maisha yao kwani wameweza kusomesha watoto, kujenga nyumba na kuanzisha miradi ufugaji wa Ngo'mbe, mbuzi ,nguruwe na hata kufuga kuku.




0 maoni:

Chapisha Maoni