Alhamisi, 26 Oktoba 2017

MBUNGE WA NZEGA MJINI HUSSEIN BASHE AGAWA VITAMBULISHO VYA MATIBBU KWA WAZEE 540 JIMBONI KWAKE

Posted by Esta Malibiche on Oct 27,2017 IN  NEWS

Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini kupitia Chama cha Mapinfuzi CCM Hussein Bashe akisalimiana na Mpiga kura wake katika tukio la kukabidhi vitambulisho vya matibabu ya bure kwa wazee wa jimbo la Nzega Mjini.PICHA NA OFISI YA MBUNGE.
 Mbunge wa jimbo la Nzega Mjini ​Mkoani Tabora,kupitia chama cha Mapinduzi CCM,Mhe. Hussein Mohammed Bashe​ mapema siku ya jana amekabidhi Vitambulisho vya Matibabu ya Bure kwa wazee ndani ya Jimbo la Nzega Mjini.

Katika awamu hii ya kwanza zaidi ya wazee 1,080 watapata  Vitambulisho huku wazee 540 ndio wamekabidhiwa leo hii na wengine wataendelea kupokea kutoka katika Ofisi ya Mbunge kwa muda wa wiki nzima huku matarajio yakiwa ni kuwafikia wazee 3,284 katika jimbo zima.

Aidha; sherehe hizo zimehudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Nzega ​Mhe. Godfrey Ngupula​ ambaye ndiye alikuwa Mgeni Rasmi.

​Katika hotuba yake,alimpongeza bunge kwa  jitihada zake za  ​kuhakikisha wananchi wanaondokana na chanagamoto mablaiambali zilizokuwa zinawakabili,ikiwa nipamoja na kuwaletea  maendeleo,kuwatumikia ikiwa ni mojanya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM.

"Jimbo la Nzega Mjini ni jimbo pekee ndani ya Halmashauri ya Mji wa Nzega hivyo tukio hili linaifanya Halmashauri hii kuwa moja kati ya Halmashauri chache kitaifa kutekeleza kwa vitendo Sera ya Taifa Matibabu ya Bure kwa wazee." Alisema Ngupula
Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini kupitia Chama cha Mapinfuzi CCM Hussein Bashe akiendelea kukabidhi vitambulisho vya matibabu ya bure kwa wazee wa jimbo la Nzega Mjini.PICHA NA OFISI YA MBUNGE.

Mkuu wa Wilaya ya Nzega ​Mhe. Godfrey Ngupula​ ambaye ndiye alikuwa Mgeni Rasmi,akikabidhi vitambulisho vya matibabu kwa wazee wa jimbo la Nzega Mjini.PICHA NA OFISI YA MBUNGE.

 Wazee wa jimbo la Nzega Mjini wakiwa katika tukio la kukabidhiwa vitambulisho vya matibabu vilivyotolewa na mbunge wao Hussein Bashe.
Wazee wa jimbo la Nzega Mjini wakiwa katika tukio la kukabidhiwa vitambulisho vya matibabu vilivyotolewa na mbunge wao Hussein Bashe.

0 maoni:

Chapisha Maoni