Jumatano, 25 Oktoba 2017

LEO VIWANJA SITA KUWAKA MOTO KOMBE LA SPANEST CUP


Posted by Esta Malibiche on Oct 25,2017 IN MICHEZO
Image result for SPANEST CUP 2017

MZUNGUKO wa Ligi ya Kombe la SPANEST Okoa Tembo Piga Vita Ujangili iliyozinduliwa Oktoba 21, mwaka huu katika uwanja wa Kimande, Pawaga; unaendelea kesho Jumatano kwa michezo sita itakayopigwa katika viwanja mbalimbali vya Tarafa ya Pawaga.
Katika mzunguko huo, washindi wa pili wa kombe hilo mwaka 2016, Kinyika  FC watakuwa uwanja wa nyumbani wakiikaribisha Isele FC.
Katika kijiji cha Ilolompya, Ilolompya FC itakuwa mwenyeji wa Magozi FC huku Mkombilenga FC ikiikaribisha katika uwanja wake wa nyumbani Luganga FC.
Nayo Mbuyuni FC itakuwa mwenyeji wa Kimande FC wakati Magombwe FC itaikaribisha Kisanga FC na Mboliboli FC itaikaribisha Mbugani FC.
Ligi hiyo inayopigwa kwa mwaka wan ne sasa inazishirikisha timu 24 za vijiji vya tarafa ya Idodi na Pawaga vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha kwa upande wa wilaya ya Iringa.
Mratibu wa Spanest Godwell Ole Maing’ataki amesema mshindi wa kwanza wa ligi hiyo inayopigwa kwa mwezi mmoja ataondoka na kombe, medali za dhahabu, seti moja ya jezi, cheti, Sh Milioni Moja taslimu na atapata fursa ya kutembelea hifadhi ya taifa ya Ruaha.
Wakati mshindi wa pili wa ligi hiyo ataondoka na medali za shaba, cheti, mipira miwili na Sh 700,000 taslimu, mshindi wa tatu ataondoka na cheti, medali na Sh 500,000.
Meingataki amesema kwa kupitia ligi hiyo, makundi makubwa ya vijana yanapata fursa ya kukutana na wadau mbalimbali wa uhifadhi na utalii, kufurahia mchezo huo na kupata taarifa mbalimbali zinazohitaji ushiriki wao katika vita dhidi ya ujangili wa rasilimali zilizohifadhiwa.

0 maoni:

Chapisha Maoni