Alhamisi, 12 Oktoba 2017

WANANACHI WA KIJIJI CHA KIMALA WILAYANI KILOLO WAISHUKURU KAMPUNI YA NEW FORESTS KWA KUJENGA VYUMBA VYA MADARASA

Posted by Esta Malibiche on OCT 12,2017 IN NEWS

Mkurugenzi wa kapuni ya News Forst Tshepiso  Dumasi akitoa risala kwa mgeni rasmi,katika hafla fupi ya kukabidhi Jengo la vyumba vya madarasa shule ya Msingi Kimala iliyopo katika kijiji cha Kimala  Wilayani Kilolo Mkoani Iringa.PICHA NA ESTA MALIBICHE.
 
Na Esta Malibiche,Majira

Kilolo


WANANCHI wa kijiji cha Kimala ,kilichopo kata ya Kimala Wilaya Kilolo Mkoani Iringa,wameishukuru kampuni ya News Forest kwa kuwajengea madarasa mawili kwa ajili ya kusomea watoto wa Shule ya Msingi Kimala.


Kauli hiyo imetolewa jana na Ezekiel Nyamonga ambae ni Mwenyekiti wa kamati ya Shule hiyo wakati wa uzinduzi wa vyumba vya madarasa    katika shule ya Msingi Kimala Wilayani Kilolo, huku akiwataka wanadau wengine wa maendeleo kujitoa hasa katika setkta ya Elimu  ili changamoto zinazoikabili shule hiyo ziweze kupungua ama kumalizika kabisa.


Nyamonga alisema kuwa hapo awali walikuwa wanakabiliwa na uhaba wavyumba vya madarasa kutokana na wimbi kubwa la wanafunzi  kuongezeka mara baada ya serikali kutamka kuwa Elimu bure,wazazi wengi wamekuwa na mwamko na kuwaandikisha watoto wao.


Bado tunakabiliwa na changamoto ya vyumba vya madarasa,ninawaomba wadau wa Elimu mjitokeze kutusaidia ili watoto wetu waweze kusoma wakiwa wamekaa mahali panapostahili,hii itasaidia kuinua kiwango cha ufauru katika shule yetu’Alisema Nyamonga


Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kilolo  Asia Abdalah,Katibu Tawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Yusuph Magwaya aliwasihi walimu kuahakikisha wanasimamia swala la ulinzi  kwa wananfunzi ili madarasa waliyokabidhiwa yasiharibiwe.


Magwaya aliwasihi wazazi kuwa karibu na walimu na  kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya watoto wao shuleni, kuwapunguzia kazi za kufanya pamoja na hatimae kuwapa muda mwingi wa kujikumbusha masomo wawapo  nyumbani.


'Ninawaomba wawazi hasa akina mama,kuweni karibu na watoto wenu,acheni tabia ya kuwaachia walimu kila kitu.Ili ndoto zao ziweze kutimia manatakiwa kukagua masomo yao,kuwapa muda wa kujifunza na kuhakikisha mnawapa satahiki zao zinazotakiwa kama daftari,karamu nk.’’’Alisema Magwaya

Awali akisoma Risala ya kampuni ya News Forest Mkurugenzi Tshepiso Dumas alisema kuwa kutokana na kampuni hiyo kutambuau muhimu wa jamii zinazowazunguka sababu pekee iliyowasukuma kwa kiasi kikubwa sana kuchangia Kuboresha katika Elimu, hali ya uchumi wa kaya na jamii kwa ujumla huku kushirikiana na wadau mbalimbaliwa maendeleo.


Dumas alisema kwa kiasi kikubwa shughuli zetu za kijamii zinafanikiwa kutokana na ushirikiano mkubwa kukota katka Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia viongozi wake wa nchi, mikoa, wilaya, Tarafa, kata na vijiji pamoja na   jamii kwa ujumla. Na kuongeza kuwa katika Mradi huo wa ujenzi wa vyumba vya madarasa wamefanikiwa kwa asilimia kubwa, hii ni kutokana na ushirikiano mkubwa uliokuwepo kati ya viongozi wa serikali, kijiji na jamii kwa ujumla.


‘’ Ndugu mgeni rasmi, Kampuni ya New Forests ilianza rasmi kufanya kazi hapa nchini Tanzania mwaka 2010, inajishughulisha na misitu na inafanya kazi katika nchi za jangwa la Saraha, ambapo inajishughulisha na uuzaji wa nguzo za umeme zilizotibiwa, pia  inapanda miti ya biashara ikiwemo Miringoti (Eucalyptus) na Misindano (Pine).Pia Kampuni ya New Forest imepata umaarufu mkubwa  katika kukuza sekta ya ujenzi, Miundo mbinu na  sekta ya umeme  Mashariki na  Kusini mwa Africa kwa bidhaa za mbao na nguzo za umeme zenye kiwango cha hali ya juualisema Dumas na kuongeza kuwa

Mradi huu wa ujenzi wa vyumba vya madarasa umegharimu pesa za kiasi cha milion 48,707,340.Kampuni imechangia kiasi cha milioni 44,279,400 katika ujenzi wa jengo ambalo ni sawa na asilimia 90.{90%),jamii imechangia kiasi cha milioni 4,427,940 malighafi za ujenzi ambayo ni sawa na asilimia 10 (10%)na wilaya imechangia kupendekeza mwalimu aliyehusika katika utekelezaji wa Mradi’’Alisema Dumas

Ninapenda kuwapongeza wananchi wa kijiji cha kimala kwa ushirikianowao mkubwa waliouonyesha wakati wa utekelezaji wa Mradi, kwa hakika hakukuwa na changamoto yoyote tangu tulipoanza ujenzi  hadi tumemaliza na hatimae kuukabidhi kwa wananchi hii leo.


Aliongeza kuwa Mradi huo ulianza kutekelezwa mwezi wa nane mwaka 2016 na ulikamilika mwezi wa kumi na mbilimwaka 2016.,wakiwa na lengo la kukidhi uhaba na uchakavu wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo ya msingi kama jamii ilivyopendekeza kipindi cha mipango shirikishi ya jamii.

Kampuni inapendakuwasihi walimu na wanafunzi wa shule ya msingi Kimala kuyatunza madarasa haya  ili yawe msadda kwaos asa na kwa vizazivijavyo.Pia tunapenda kuishukuru Halmashuri ya Wilaya ya Kilolo kwa ushirikiano walioutoa katika kutekeleza shughuli zetu ikiwa nipamoja na mradi huu.

Katibu Tawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo,Yusuph Magwaya akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo,Asia Abdalah.PICHA NA ESTA MALIBICHE.






Wanafunzi wa shule ya Msingi Kimala wakishiriki hafla ya kukabidhiwa jengo la vyumba vya madarasa yaliyojengwa na wadau wa maendeleo ambao ni Kampuni ya New Forests



















































0 maoni:

Chapisha Maoni