Alhamisi, 12 Oktoba 2017

KAMPUNI YA NEW FORESTS YAWAKABIDHI NYUMBA WAUGUZI WA ZAHANATI YA KISING'A WILAYANI KILOLO

Posted by Esta Malibiche on Oct 12,2017 IN NEWS



 Wananchi wa kijiji cha Kising'a Wilayani Kilolo Mkoani Iringa wakiwa katika hafla fupi ya kukabidhiwa nyumba ya wauguzi wa Zahanati ya Kising'a iliyojengwa na Kampuni ya New Forests.PICHA NA ESTA MALIBICHE.

 Mkurugenzi wa kapuni ya New Forests, Tshepiso  Dumasi akitoa risala kwa mgeni rasmi,katika hafla fupi ya kukabidhi nyumba ya wahudumu wa Afya wa Zahanati ya Kising'a iliyopo katika kijiji cha Kising'A Wilayani Kilolo Mkoani Iringa.PICHA NA ESTA MALIBICHE.

Mkurugenzi wa kapuni ya News Forst Tshepiso  Dumasi akitoa risala kwa mgeni rasmi,katika hafla fup[i ya kukabidhi nyumba ya wahudumu wa Afya wa Zahanati ya Kising'a iliyopo katika kijiji cha Kising'A Wilayani Kilolo Mkoani Iringa.PICHA NA ESTA MALIBICHE.








Katibu Tawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo,Yusuph Magwaya akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo,Asia Abdalah.
Katibu Tawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo,Yusuph Magwaya akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo,Asia Abdalah.
Na Esta Malibiche
 Kilolo
Wananchi wa kijiji cha Kising’a Wilayani Kilolo Mkoani Iringa wametakiwa kutunza nyumba ya wauguzi  wa  zahanati ya kijiji hicho iliyokabidhiwa na Kampuni ya New Forest jana ili iweze kuwasaidia  watumishi hao waliokuwa wanakabiliwa na chanagamoto ya kukaa mbali na kituo cha kazi hivyo   kushindwa kuwahudumia wananchi kwa wakati.
Kauli hiyo imetolea jana na Meneja rasilimali watu Sara Tesha wakati akisoma risala ya kampuni hiyo kwa Mgeni Rasmi wakati wakikabidhi Nyumba wa wauguzi wa Zahanati ya Kising’a iliyopo katika kijiji cha Kising’a Wilayani Kilolo Mkoano hapa.
Katika Risala yake alisema kuwa kampuni hiyo kwa  kutambua umuhimu wa jamii zinazowazunguka ndiyo maana imewekeza kwa kiasi kikubwa sana katika kuchangia Kuboresha Afya, hali ya uchumi wa kaya na jamii kwa ujumla.

Tesha alisema kuwa Mradi huo umegharimu pesa za kitanzania milion 51,168,000. hata hivyo Kampuni imechangia Tsh. i 46,051,200 Mill.katika ujenzi wa jengo hilo,ambayo ni sawa na asilimiatisini (90%), jamii imechangia Tsh. Mill 5,116,800 malighafi za ujenzi ambayo ni sawa na asilimia 10 (10%)na wilaya ya Kilolo imechangia kupendekeza muudumu wa afya aliyehusika katika utekelezaji wa Mradi huo.

‘’Lengo la Mradi huu ni kukidhiu haba wa nyumba za wauguzi katika Zahanati hii ya kising’a kama jamii ilivyopendekeza kipindi cha mipango shirikishi ya jamii ambapo kwa kiasi kikubwa shughuli zetu za kijamii zinafanikiwa kutokana na ushirikiano mkubwa kukota katka Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia viongozi wake wa nchi, mikoa, wilaya, Tarafa, kata na vijiji na jamii kwa ujumla.
Alisma  Katika Mradi huu wa ujenzi wa nyumba ya wauguzitumefanikiwa kwa asilimiazote hii ni kutokana na ushirikianomkubwauliokuwepokati ya viongozi wa serikali, kijiji na jamii kwa ujumla na kuongeza kuwa
Kilapenyemafanikiohapakosi changamoto, changamoto kubwatuliyoipata katika utekelezaji wa Mradi huu ni utayarimdogo wa jamii katika kuchangia asilimia 10 (10%). Tulifanikiwa kutatua changamoto hii kwa kuielimisha jamii umuhimu wa Mradi na umiliki wa mradi. Baada ya Elimu jamii ilielewa na kuchangia hata kukamilika kwamradi huu
Kwa upande wake katibu Tawala wa Wilaya ya Kilolo,Yusuph Magwaya aliishukuru Kampuni ya New Forests kwa kujitolea ujenzi wa nyumba hiyo na kusema kuwa  imetatua changamoto ya hapo awali ambapo  wauguzi waliokuwa wanakaa mbali na kituo cha kazi hivyo kushindwa kuwahudumia wananchi  ipasavyo.
‘Mara nyingi tumekuwa tukilalamika  kuwa wahudumu wa Zahanati wanakaa mbali na kituo ,Leoa hii tumepata nyumba kutoka Kampuni ya New Forests na tuaanza kuhudumia vizuri,ninawaomba tuwe walinzi kuhakikisha wale wataokaa hapa wanaitunza hii nyumba ili na wengine wakija waikute’Alisema Magwaya
Pia alisisitiza swala la vyoo bora kwa kuwahamasisha wananchi kuhakikisha wanakuwa na vyoo hivyo ili kujikinga na magonjwa ya amlipuko,kama kipindupindu na magonjwa mengine.
Aidha  aliwataka wanachi kuyatunza mazingira kwa kutochoma moto ovyo katika misitu iliyopandwa na kuhidfadhiwa .





































0 maoni:

Chapisha Maoni