Jumatatu, 9 Oktoba 2017

Dk.HAMIS KIGWANGALA;TUZIDI KUOMBEANA DUA ,SITAWAANGUSHA WATANZANIA

Posted by Esta Malibiche On Oct 9,2017 IN NEWS

Mbunge wa Nzega Vijijini ambaye pia alikuwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto kabla ya uteuzi mpya wa Wizara ya Maliasili na Utalii hiyo jana Oktoba 7,2017, Dk. Hamisi Kigwangalla amewataka watanzania kuendelea kumuombea dua pamoja na ushirikiano katika majukumu yake mpya.

“Nimepokea salamu nyingi za pongezi na shukrani kwa Mungu aliye juu. Sintoweza kumjibu kila mtu, uungwana ni kutambua pongezi zenu na dua tele mlizotuombea, nawashukuru sana ndugu zangu. Tuzidi kuombeana dua tu.
Tuna kazi ngumu ya kukimbia kukidhi matarajio ya kiongozi wetu Mkuu aliyetuamini na matarajio ya wananchi wenzetu. Binafsi nawaahidi nyote kuwa sintowaangusha! Ahsanteni sana ndugu zangu, natarajia ushirikiano wenu wa kila hali.” Alieleza Dk. Hamisi Kigwangalla.

Awali taarifa za kuteuliwa kwake katika wizara nyingine, alizipata kupitia kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi kwa njia ya simu  wakati akiwa kwenye majukumu ya  ziara ya kuboresha mfumo wa afya, akiwa Wilayani Nachingwea, Kata ya Kilimalondo umbali wa zaidi ya kilometa 100, kutoka Makao makuu ya Wilaya hiyo ya Nachingwea, aliweza kusitisha ziara yake hiyo ambayo alitakiwa kuendelea katika Vijiji na Wilaya nyingine ya Liwale.


 
Mbunge wa Nzega Vijijini ambaye pia alikuwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto kabla ya uteuzi mpya wa Wizara ya Utalii hiyo jana Oktoba 7,2017, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua chumba cha upasuaji mkubwa cha kituo cha AAfya Kilimalondo, Wilayani Nachingwea Mkoani Lindi. 
Dk.Kigwangalla akipata maelezo kutoka kwa Mganga wa kituo cha Afya Kilimalondo wakati wa ziara hiyo
Mbunge wa Nzega Vijijini ambaye pia alikuwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto kabla ya uteuzi mpya wa Wizara ya Utalii hiyo jana Oktoba 7,2017, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua vifaa vipya vya chumba cha upasuaji mkubwa cha kituo cha AAfya Kilimalondo, Wilayani Nachingwea Mkoani Lindi. Kituo hicho kilifungiwa kisifanye upasuaje mpaka kitakapokidhi vigezo, hata hivyo Dk.Kigwangalla alitoa miezi mitatu kiwe kimefanyiwa marekebisho na kianze kazi mara moja
Katibu Tawala wa Wilaya ya Lindi akimpatia taarifa Dk. Kigwangalla juu ya uteuzi wake mpya hivyo kusitisha shughuli zote zilizokuwa zimepangwa kuendelea katika wilaya hiyo.
 
 Dk.Kigwangalla akiagana na viongozi wa Wilaya ya Nachingwea  baada ya kusimamisha ziara yake kufuatia uteuzi mpya. Baada ya kupata taarifa hiyo kila kitu ilibidi kisimame hapo hapo. Namba za NW AMJW ilibidi ziondolewe na safari ya kutoka huko ianze.
 
Dk. Kigwangalla akiwa Mhe. Hassan Elias Masala (Mb.), Mbunge wa Jimbo la Nachingwea wakiagana mapema jana Oktoba 7,2017, majira ya saa nane za mchana baada ya kupata ujumbe wa kuteuliwa nafasi mpya. Hiyo ni baada ya kumaliza kazi kituoni hapo  Kilimalondo na kuanza kuelekea Liwale, Kituo cha Afya Kibutuka, Ndipo alipopata taarifa kuna mabadiliko ya Baraza la mawaziri.
Awali kabla ya kupata taarifa za majukumu mapya, Dk. Kigwangalla alikuwa aendelee na ziara hiyo katikaWilaya ya Liwale, Kituo cha Afya Kibutuka.
Dk. Kigwangalla alikuwa katika ziara yake hiyo ya kikazi ya siku tano ndani ya Mkoa wa Lindi ambapo alitoa maagizo mbalimbali ya kuhakikisha viongozi wa Vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali wanatekeleza maagizo yote aliyotoa kwani ni maagizo halali ya kiserikali na watakaoshindwa watachukuliwa hatua. Miongoni mwa maagizo hayo ni pamoja na kila kituo cha Afya kuhakikisha kina chumba cha upasuaji kufuatia agizo/tamko la Mwandoya alilolitoa Novemba 2016, Mwandoya Meatu Mkoani Simiyu.

0 maoni:

Chapisha Maoni