Kwa Habari za kitaifa na kimataifa

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za michezo na burudani

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za afya

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za Kilimo

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za uchumi na biashara

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za elimu

Tembelea Kali ya habari

Jumanne, 31 Oktoba 2017

RITHA KABATI AENDELEZA MPANGO WAKE WA KUKARABATI SHULE ZA MSINGI ZILIZOPO MANISPAA YA IRINGA.

 Posted by Esta Malibiche on Oct 31,2017 IN NEWS
 MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa Iringa kupitia chama cha Mapinduzi CCM,Ritta Kabati akizungumza na kamati ya shule na wazazi hawapo pichani,kwenye kikao cha uchangiaji vifaa kwa ajili ya   ukarabati wa shule ya Msingi Igeleke iliyopo Mnispaa ya Iringa,ambayo inakabiliwa na uchakavu wa majengo.PICHA NA ESTA MALIBICHE.



Na Esta Malibiche
IRINGA
MBUNGE wa Viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha Mapinduzi CCM Ritha kabati  ameendelea na mpango wake wa kukarabati shule za Msingi kongwe zilizochakaa zilizopo  Manispaa ya Iringa,ili wanafunzi waweze kusoma katika mazingira yanayostahili.

Akizungumza na wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika shule ya Igeleke iliyoko kata ya Mkimbizi Manispaa ya Iringa wakati akihamasisha uchangiaji wa vifaa vya ujenzi ili kukarabati majengo ya Shule hiyo yaliyochakaa,alisema ni aibu kwa shule kongwe kama hiyo kuwa miundo mbinu mibovu ambayo inawafanya wanafunzi kukaa kwa wasi wasi,hivyo aliwataka wazazi kuwekeza katika Elimu kwa kuchangia ili watoto waweze kusoma katika Mazingira rafiki na yanayostahili.

Ninawaomba Wazazi tuwarithishe watoto katikaElimu na siyo mali,mtoto akipata Elimu ataweza kujipangia nini cha kufanya na siyo mkurithisha mtoto mali.Mali bila Elimu ni sawa na bure.Elimu kwa mtoto ni muhimu sana kuliko kitu chochote,kwa kutambua hilo ninawaomba  wa Elimu tuwekeze katika Elimu"Alisema Kabati.

Aidha Katika kikao hicho,wazazi walitoa mchango wa  vifaa mbalimbali  ikiwa nipamoja na Cement mifuko 33,Kokoto ndoo 17,Misumari kg13 na fedha kiasi cha Tsh.56950,vifa hivyo vilitolewa na wazazi ambapo mbunge alichangia  mifuko 100 ya Saruji na pamoja na  Singboard 100 

''Sisi sote ni mashuhuda,watoto wetu wanasoma katika mazimgira magumu ambayo hayastahili,hali inayopelekea kutofanya vizuri  katika masomo yao.Baada ya kuliona hilo,nikaweka mpango mkakati wa kuhakikiasha shule kongwe chakavu zinakarabatiwa kwa kushieikiana na wazazi pamoja na wadau wa Elimu""Alisema Kabati.


Kabati alisema shule hiyo licha ya kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani majengo yake hayaendani kabisa na hali halisi ya ufaulu wa wanafunzi hivyo kwa kushirikiana na wazazi ambao wamechangia vitu mbalimbali ukarabati wa shule hiyo utaanza jumamosi wiki hii.

 “ Nimetembelea shule nyingi mkoani kwetu hasa za msingi kuweza kuangalia miundo mbinu na majengo yake kwa kweli hali inatisha na majengo mengi yamekuwa chakavu hivyo nitajitahidi kwa kushirikiana na wadau wa elimu kuweza kukarabati yaendane na hali ya sasa ya kuwa bora zaidi” alisema

Aliongeza kuwa shule ya Igeleke ni moja ya shule zinazofanya vizuri katika mitihani yake lakini imeharika hovyo na inahitaji msaada wa haraka kuikarabati kwa kuwa wanafunzi wanasoma katika mazingira magumu na kudumisha elimu ya wanafunzi hao waendelee kuongoza mkoani hapa.

Hadi sasa mbunge huyo amekwisha fanya ukarabati kwa shule za msingi za Azimio, Kihesa,Mtwivira na shule ya Kibwabwa ambazo alizitembelea na kubaini uchakavu mkubwa wa majengo na miundo mbinu mibaya na shule nyingine alizoahidi kuzifanyia ukarabati ni shule ya msingi Gangilonga.
Peter Kyando mmoja wa wazazi alimshukuru Mbunge huyo kwa niaba ya wazazi huku akiwataka wadau wa Elimu kujitoa kuchangia vifaa mbalimbali ili zoezi la ukarabati liweze kukamilika kwa wakati ili wanafunzi waweze kusoma katika mazingira rafiki.


Tunamshukuru Mbunge kwa kuona umuhimu wa Elimu,na kujitoa kukarababti majengo ya madarasa yaliyochakaa.Tuanaghitaji na wadau wengine waje,kwasababu bado vifaa vinahitajika ili kukamilisha.


  MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa Iringa kupitia chama cha Mapinduzi CCM,Ritta Kabati akizungumza na kamati ya shule na wazazi hawapo pichani,kwenye kikao cha uchangiaji vifaa kwa ajili ya   ukarabati wa shule ya Msingi Igeleke iliyopo Mnispaa ya Iringa,ambayo inakabiliwa na uchakavu wa majengo.PICHA NA ESTA MALIBICHE.



 















MKUU WA MKOA WA IRINGA AMINA MASENZA AZINDUA KAMPENI YA KITAIFA YA USAFI WA MAZINGIRA.

Posted by Esta Malibiche on Oct 31,2017 IN NEWS
Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akizindua kampeni ya kitaifa ya usafi wa Mazingira,iliyozinduliwa eneo la  mapema leo hii katika la Nduli MaNispaa ya Iringa,Mkoani Iringa.PICHA NA ESTA MALIBICHE.


Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amewaagiza wakuu wa wilaya mkoani hapa kuhakikisha wanawahimiza wananchi ujenzi wa vyoo bora na utunzaji wa mazingira.

Agizo hilo amelitoa mapema leo hii wakati akikagua ujenzi wa choo katika shule ya Msingi Ndukli Mnispaa ya Iringa.

Aidha mkuu wa Mkoa amezindua kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira na kuwasisitiza wananchi wazingatie usafi katika mazingira yanayowazunguka ili kuepukana na magonjewa ya mlipuko.

''Ninaomba tuunge mkono kampeni hii ya kitaifa na kila mmoja atimize wajibu wake kuhakikisha anajenga choo bora na kutunza mazingira''
Meneja wa Kiwanja cha Ndege Iringa,Hana Kibopile akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya usafi wa Mazingira,uliofanyika mapema leo hii katika shule ya Msingi Nduli Manispaa ya Iringa.

Diwani wa kata ya Nduli kupitia chama cha Mapinduzi CCM,Bashiri Mtove,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya usafi wa Mazingira,uliofanyika mapema leo hii katika shule ya Msingi Nduli Manispaa ya Iringa.


Mwandishi wa Habari Gazeti la MjiraMkoa wa Iringa,na mmiliki wa blog ya KALI YA HABARI,Esther Malibiche akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya usafi wa Mazingira ,uliofanyika katika shule ya Msingi Nduli Manispaa ya Iringa.
Mwandishi wa Habari wa Radio Nuru fm,Dajari Mdigange akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya usafi wa Mazingira ,uliofanyika katika shule ya Msingi Nduli Manispaa ya Iringa.


 Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Msenza,akikagua choo cha mkaziwa Nduli
 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akitoa magizo kwa watendaji wa Afya Mnaspaa ya Iringa,kuhakikisha wanasimamia swala la ujenzi wa vyoo bora kwa kila nyumba.














 Choo kinachoendelea kujengwa  shule ya Msingi Nduli,kikiwa na matundu 5 kwa wanaume na matundu 6 wanawake
  Choo kinachoendelea kujengwa  shule ya Msingi Nduli,kikiwa na matundu 5 kwa wanaume na matundu 6 wanawake
 Choo kinachoendelea kujengwa  shule ya Msingi Nduli,kikiwa na matundu 5 kwa wanaume na matundu 6 wanawake
Matundu ya choo kipya kinachoendelea kujengwa kwa ajili ya matumizi ya wananfunzi katika Shule ya Msingi Nduli Manispaa ya Iringa.

 

  Choo kinatumika hivi sasa na wanafunzi wa shule ya Mdsingi Nduli wakati ujenzi wa choo bora unaendelea

 Choo kinatumika hivi sasa na wanafunzi wa shule ya Mdsingi Nduli wakati ujenzi wa choo bora unaendelea

 Choo kinatumika hivi sasa na wanafunzi wa shule ya Mdsingi Nduli wakati ujenzi wa choo bora unaendelea
  Choo kinatumika hivi sasa na wanafunzi wa shule ya Mdsingi Nduli wakati ujenzi wa choo bora unaendelea
 Choo kinatumika hivi sasa na wanafunzi wa shule ya Mdsingi Nduli wakati ujenzi wa choo bora unaendelea
 Mwanafunzi wa shule ya Msingi Nduli akiingia chooni,Choo ambacho  kinatumika hivi sasa wakati ujenzi wa choo bora unaendelea.
   Mwanafunzi wa shule ya Msingi Nduli akiingia chooni,Choo ambacho   kinachotumiwa hivi sasa wakati ujenzi wa choo bora unaendelea.







































RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AFUNGUA VIWANDA VIWILI JIJINI MWANZA

Posted by Esta Malibiche on Oct 31,2017 IN NEWS


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi katika eneo la kona ya Butimba wakati akitokea Igogo jijini Mwanza.
Wananchi wa Butimba na Mkuyuni wakifurahi wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza nao katika eneo la kona ya Butimba wakati akitokea Igogo jijini Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage mara baada ya kufungua kiwanda cha Victoria molders and polybags kilichopo Igogo jijini Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono mafundi wa Kiwanda cha Victoria molders and polybags mara baada ya kutengeneza Tanki la kuhifadhia maji.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia utengenezaji wa viti vya plastiki katika kiwanda cha Victoria molders and polybags katika eneo la Igogo jijini Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia mfuniko uliotengenezwa katika kiwanda hicho cha Victoria molders and polybags Igogo jijini Mwanza.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Meya ya jiji la Mwanza James Bwire mara baada ya kufungua kiwanda cha Victoria molders and polybags Igogo jijini Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kiwanda cha madawa cha  Prince Pharmaceuticals kilichopo Buhongwa nje kidogo jijini Mwanza.
PICHA NA IKULU

Jumamosi, 28 Oktoba 2017

HAPPYBITHDAY MH.RAIS DKT.MAGUFULI

Posted by Esta Malibiche on Oct 29,2017.
Uongozi wa blog hii ya KALI YA HABARI  inaungana na Watanzania wote kumtakia heri ya kuzaliwa Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania Dkt.John Pombe Joseph Magufuli.Tunamuombea Mungu amjalie Afya njema na maisha marefu ili azidi kulitumia Taifa la Tanzania.
HAPPYBIRTH DAY MH.RAIS MAGUFULI.

MAGAZETINI JUMAPILI YA LEO OKTOBA 29/2017

Posted by Esta Malibiche on Oct 29,2017 IN KITAIFA


MKUU WA WILAYA YA MBULU AMEZITAKA KAYA MASIKINI KUTUMIA KWA MALENGO KUSUDIWA FEDHA ZA TASAF

Posted by Esta Malibiche on Oct 28,2017  IN NEWS

Mkuu Wa  wilaya ya  mbulu Chelestino s Mofuga leo ,28/10/2017 atembelea kaya maskini zilizopo katika mpango wa Tasaf na kupata maelezo ya wanufaika jinsi wanavyotumia fedha hizo. Baada ya kutembelea kaya hizo amefanya mkutano na wananchi kuhamasisha uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa, na kupiga vita pombe haramu ya moshi ambaye inasababisha matukio ya uhalifu mbalimbali.
Pia mkuu wa wilaya ameonya vikali wanaopata fadha za Tasaf na kunywa pombe, kuolea wake wa pili badala ya kuanzisha miradi na kusomesha wastoto.


Aidha baadhi ya wanufaika wamekiri na kusema kuwa fedha za Tasaf ni mkombozi katika maisha yao kwani wameweza kusomesha watoto, kujenga nyumba na kuanzisha miradi ufugaji wa Ngo'mbe, mbuzi ,nguruwe na hata kufuga kuku.