Ijumaa, 23 Juni 2017

KKKT DAYOSISI YA IRINGA YAMPONGEZA RAIS MAGUFULI



Posted by Esta Malibiche on JUNE 23,2017 IN NEWS

Katibu mkuu KKKT dayosisi ya Iringa Nayman chavala akizungumza naVyombo vya Habari.


Na Esta Malibiche,Majira
Iringa
KANISA la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya Iringa limempongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya ya kuwatumikia watanzania kwa uadilifu mkubwa,hivyo kuwataka  watanzania kuendelea kumpa ushirikiano  na kumuombea.

Akizungumza na vyombo vya Habari ofisini kwake,Katibu mkuu wa KKKT dayosisi ya Iringa Nayman Chavala alisema, hatua anazochukua Mh.Rais zinatakiwa kupongezwa kwa vitendo hasa za kuwabana wasio waadilifu pamoja na kupambana na wizi wa mchanga wa dhahabu (MAKINIKIA) ni hatua ya kupongezwa kwani suala hilo lilikuwa likiwanufaisha wachache huku Taifa likibaki patupu .

" Sisi kama kanisa tumekuwa tukimuombea kila wakati tena kwa kumtaja kwa jina na hatutachoka kuendelea kumuombea maana kazi anayoifanya ni ngumu ambayo silaha kubwa ni maombi "Alisema Chavala

Aidha akizungumzia maandalizi ya kumwingiza kazini askofu mteule Mchungaji Blaston Gavile na msaidizi wake Mchungaji Himidi Saga alisema yamekamilika na yanatarajia kufanyika siku ya jumapili tarehe 25,6,2017,Kuanzia saa tatu asubuhi kwenye viwanja vya shule ya Msingi Gangilonga Manispaa ya IOringa.


Alisema ibada hiyo itaongozwa na askofu mkuu wa KKKT Dkt Frederick Shoo pamoja na askofu mstaafu Dkt Owdenburg Mdegella na kuwa kabla ya idaba kutakuwa na maandamano ya wachungaji na washarika yatakayoanzia usharika wa kanisa kuu hadi Gangilonga.

" Tunaomba wananchi wote na washarika kujitokeza kwa wingi kushuhudia tukio hilo la kihistoria pia tunategemea kuwa na viongozi mbali mbali wa serikali na wageni mashuhuri kutoka ndani na nje ya Tanzania"Alisema Chavala na kusisitiza kuwa


Aliongeza kuwa Askofu Gavile amechukua nafasi ya aliyekuwa askofu wa kanisa hilo Dkt Mdegella ambaye alistaafu kwa heshima kubwa na kuacha heshima ya aina yake ndani ya KKKT .







0 maoni:

Chapisha Maoni