Ijumaa, 23 Juni 2017

ASKOFU MINANI KUTOKA UGANDA AONGOZA MAOMBI YA KUMUOMBEA JPM.

Posted by Esta Malibiche ON JUNE23,2017 in NEWS

Na Tiganya Vincent
 
IGUNGA
 
Askofu Henery Minani wa Makanisa la Pentecostal kutoka Uganda amesema uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli utasaidia wananchi wengi kunufaika rasilimali walizopewa na Mungu.
 
Kiongozi huyo alisema hayo jana wilayani Igunga wakati wa kongamano la Kwaya kutoka ndani na nje ya Tanzania ambapo pamoja na uimbaji waliendesha maombi mbalimbali ya kuombea nchi na viongozi wake.
 
Alisema kuwa Mungu aliamua kuwapa wananchi wa Tanzania Rais Magufuli ili awaongoze katika kuibadilisha nchi hii kutoka ilipokuwa na kuwa ya neema kwa watu wote kwa kufaidi utajiri walipewa na Mungu.
 
Akifungua kongamano hilo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Aggrey Mwanri alisema kuwa kazi nzuri aliyoiana Rais katika vita ya uchumi inahitaji kuungwa mkono na viongozi wa dini ili Mungu ampe nguvu katika mapambano ambayo yanalenga kuwaleta maisha bora wananchi wengi kwa kunufaika na rasilimali zao.
 
Alisema kuwa Rais Magufuli akiachwa pekee bila msaada wa maombi na dua kutoka kwa viongozi wa dini Shetani anaweza kupata nafasi na zoezi hilo likawa gumu.
 
Bw. Mwanri alisema kuwa yeye kama Mkuu Mkoa kwa niaba ya wananchi wa Tabora wanaungana na Rais Magufuli katika vita hiyo na hawatamuacha apigane pekee yake wako nyuma yake na wataendelea kumuombea kwa Mungu.
 
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewaomba viongozi wa dini kuuombea Mkoa wa Tabora ili mauji yanatokana na ushirikina, wivu wa kimapenzi, ujambazi na kulipa visasi yakome.
 
Alisema kuwa mauaji hayo yamekuwa yakinyima usingizi na hivyo kwa nguvu ya maombi na ya dola mauaji hayo yatakoma.
 
Bw. Mwanri alisema kuwa viongozi wa dini hawawezi kujitoa katika mapambano dhidi ya mauji hao, kwani wakijitoa na kuiachia Serikali pekee yake damu ya watu inayomwagika itakuja kuwalilia.
 
Kongamano hilo la Kwaya ambalo linawashiriki kutoka Tanzania, Kenya na Uganda limeandaliwa na Kanisa la FPTC na linalizika Jumapili hii.

0 maoni:

Chapisha Maoni