Jumatatu, 5 Juni 2017

WATANZANIA WAMETAKIWA KUMUOMBEA RAIS MAGUFULI

Posted by Esta Malibiche on JUNE 5,2017 IN NEWS



Na Esta Malibiche
Mufindi
WATANZANIA wametakiwa kumuombea  Mh.Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tnazania Dkt.John Pombe Magufuli  kutokana na kazi kubwa anayoifanya  kuwatumikia wananchi na kuhakikisha lasilimali za Nchi zinawanufaisha watanzania wote.
Kauli hiyo imetolewa jana na Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba wakati akizungumza wna wananchi wa amkoa wa Iringa katika Halmashauri ya wilaya ya Mfindi kwenye tamasha la uzinduzi sa nyimbo za Injili kwaya ya Mtakatifu Secilia parokia ya Mafinga Jimbo Katoliki la Iringa.
Katika uzinduzi huo waziri Mwigulu aliambatana na Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Iringa Rose Tweve,Mbunge wa mafinga mjini Cosato Chumi,Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Willium Jamuhuri,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga pamoja na Viongozi wa vyma vya Siasa.Katika uzinduzi huo jumla ya Mill.24 zilichangwa,ambapo yeye na familia yake walikabidhi kisai cha Tsh.5 Mill.
 Katika Hotuba yake Waziri Mwigulu alisema Mh.Rais anania nzuri kwa watanzania,hivyo hatuna budi kumuombea kila mmoja kwa dini yake ili awewe kuendelea kuwatumika wananchi kwa kutatua changamoto mbalimbali.
‘’Tuendendelee kumuombea Rais wetu bila kukoma kwa kazi yake kubwa nayoifnya na  kwa hatua anaozozifanya  kuhakikisha  rasilimali za Tanzania zinalindwa  na hatimae kuwanufaisha watanzania wote bila kubagua dini,kabila wa itikadi za siasa.’’Alisema Mwigulu.
Aidha Waziri Mwigulu amewataka viongozi wa dini kuhakikisha wanatoa Elimuya  ya kutosha kwa waumini wao kuhusu vitendo vya unyanyasaji  wa kijinsia,ubakaji kwa watoto wadogo,ulawiti na mauaji ya vikongwe.
Alisema viongozi wa dini wanayonafasi kubwa ya kuongea na waumini wao na wakasikilizwa kutokana na kalama aliyowapatia Mwenyezi Mungu,kwa kuisaidia Serikali  wanao uwezo mkubwa  kukemea  ili vitendo hivyo  na mtukio ya kiuharifu yasiendelee kutokea hapa Nchini.
Tuendelee kushirikiana na Serikali na wizara ya ndani kukemea vitendo viovu vinavyokiuka madili ya kitanzania,hasa katika maeneo ambayo wananchi hawashiriki katika imani.Pamoja na serikali kuweka nguvu kubwa kukemea lakini viongozi na wazaZi mna jukumu kubwa la kuongea na waumni wenu pamoja na familia zenu.
Aliongeza kuwa Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali  wanaobainika na kufanya vitendo visivyofaa katika jamii kama mauji ya watu wenye ulemavu,mauaji ya vikonge ,ubakaiji kwa watoto wadogo na kuwalawiti.

‘’Kama watanazania kupige vita dhidi ya vitendo hivo na sisi kama serikali tunaendelea kuchukua hatua mbalimbali kwa yeyote anainika kuhusika na vitendo hivyo.Pia ninawaomba kusema katika ngazi za familia,tuzungumze na watoto wetu dhidi ya athari zinazotokana na Madawa ya kulevya pia tuendelee kuongeza katika  ngazi za   familia ili tuweze kuwanusuru vijana wetu na Taifa kwa ujumla.

Akisoma Risala ya kwaya kuu ya Mtakatifu Cesilia kwa Mgeni Rami.Mwalimu Mkuu wa kwaya hiyo Pius Kalimsenga alisema kuwa  toka kuanzishwa kwa kwaya hiyo mpaka leo wamefanikiwa kurekodi DVD toleo la kwanza mwaka lenye jina ‘NATANGAZA HADHARANI’ na toleo maalumu la Albamu ya nyimbo za pasaka iliyoratibiwa na Baraza la maaskofu Tanzania (TEC) kwa kushirikiana na shirika la Utangazaji Taifa (TBC) hivi karibuni, wamefanikiwa kufungua akaunti ya kwaya katika banki ya wananchi Mufindi (MUCOBA).
wameongeza ari na imani kwa waumini kupitia uimbaji wao,  Kuongoza  ibada mbalilmbali kwa nyimbo kila tunapohitajika kufanya hivyo,wamefanya ziara mbalimbali ndani ya parokia na nje ya Parokia kupitia michango ya waumini.
Kalimsenga alisema pamoja na mafanikio hayo lakini wanakabiliwa na cganamoto mbalimbali ambazo zinapelekea kutosonga mbele katika uinjilishaji, kama Ukosefu wa chombo cha usafiri kwa ajili ya safari za uinjilishaji nje ya Parokia yetu,Mahudhurio hafifu ya waimbaji kutokana na ugumu wa maisha na ukosefu wa ajira,Wanakwaya kujiunga na kuacha kwasababu ya kukimbia michango ya kutegemeza kwaya pamoja na Kukosa miradi ambayo ingepunguza mzigo wa michango ambayo inasababisha wanakwaya kutodumu katika uinjilishaji.

Ndugu Mgeni Rasmi,kwaya yetu ina malengo yatakayoweza kutusaidai ili kuweza kujikwamua kutoka katika utegemezi ikiwa pamoja na kupunguza michango inayochangishwa na waumini kwa ajili kutegemeza kwaya zetu pale hasa pale kwaya zinapohitaji kusafiri kwenda kuinjilisha nje ya parokia, ununuzi wa vyombo na kurekodi albamu mpya.. Baadhi ya malengo hayo ni pamoja na Kuwa na usafiri wa basi ambalo litatuwezesha kusafiri maeneo mbalimbali kwa ajili ya kufanya Uinjilishaji kama lisemavyo agizo la Bwana wetu Yesu “enendeni ulimwenguni kote mkaihubiri Injili (Marko 16:15),Kuwa na miradi midogomidogo ambayo itawawezesha wanakwaya kujikwamua kiuchumi ikiwa na kuzalisha ajira kwa vijana ili kuendana kauri mbiu ya serikali yetu ya awamu ya tano isemayo”Hapa kazi tu”.

‘’’Jumla ya mahitaji  yetu kwa malengo yaliyotajwa hapo juu yanakadiriwa kufikia shilingi za kitanzania Milioni Miamoja na kumi (110,000,000/=.Tunaamini malengo haya yakitimia, kwaya itaweza kuondokana na utegemezi pamoja na michango mikubwa kwa wanakwaya wenyewe’’Alisema Kalimsenga.
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba akiwa katika vazi rasmi la kabila la Kihehe mara baada ya kuvalishwa na viongozi wa mila ya Kihehe katika jana katika uzinduzi wa kwaya ya Mtakatifu Cesilia Parokia ya Mafinga Jimbo katoliki la Iringa.
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba akiwa katika vazi rasmi la kabila la Kihehe mara baada ya kuvalishwa na viongozi wa mila ya Kihehe katika jana katika uzinduzi wa kwaya ya Mtakatifu Cesilia Parokia ya Mafinga Jimbo katoliki la Iringa.

Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba akiwa katika vazi rasmi la kabila la Kihehe mara baada ya kuvalishwa na viongozi wa mila ya Kihehe katika jana katika uzinduzi wa kwaya ya Mtakatifu Cesilia Parokia ya Mafinga Jimbo katoliki la Iringa.
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba akiwa katika vazi rasmi la kabila la Kihehe mara baada ya kuvalishwa na viongozi wa mila ya Kihehe katika jana katika uzinduzi wa kwaya ya Mtakatifu Cesilia Parokia ya Mafinga Jimbo katoliki la Iringa.
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba akiwa katika vazi rasmi la kabila la Kihehe mara baada ya kuvalishwa na viongozi wa mila ya Kihehe katika jana katika uzinduzi wa kwaya ya Mtakatifu Cesilia Parokia ya Mafinga Jimbo katoliki la Iringa.

0 maoni:

Chapisha Maoni