Ijumaa, 30 Juni 2017

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA MWAKA 2017 ASIFU USHIRIKIANO KATI YA VIONGOZI WA WILAYA YA IKUNGI NA WANANCHI

Posted by Esta Malibiche on JUNE 30,2017 IN KITAIFA

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2017 Ndg Amour Hamad Amour 
 
  
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2017 Ndg Amour Hamad Amour afurahishwa na kusifu mshikamano ulipo kati ya viongozi na wananchi katika Wilaya ya Ikungi Jambo ambalo limepelekea kutekeleza vyema miradi ya Mandeleo.
Mwenge wa Uhuru ukiwa umepata mapokezi makubwa ya wananchi waliojitokeza kuulaki umekimbizwa umbali wa Kilomita 77.9 ambapo umezuru Miradi yenye Jumla ya shilingi 2,417,184,466.72
Kati ya fedha hizo Wananchi wamechangia Shilingi 239,500,000/= ambapo Halmshauri ya wilaya ya Ikungi imechangia Shilingi 22,500,000/=, Serikali kuu imechangia 2,003,359,466.72 huku wahisani wakiwa wamechangia shilingi 151,500,000/=
Akizungumzia Uwepo wa Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu amewapongeza wakazi wa Wilaya hiyo kwa kujitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru uliowasili Katika Wilaya hiyo Leo Alhamisi June 29, 2017 katika Kijiji cha Mkiwa, Kata ya Mkiwa ukitokea katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.
Mhe Mtaturu amesema kuwa Jumla ya Miradi tisa imetembelewa na Mwenge wa Uhuru ambayo ni miradi ya  Sekta ya elimu, Afya, kilimo, Maendeleo ya Jamii, Biashara, Viwanda na Utawala.
Miradi itakayozinduliwa ni pamoja na Programu ya Kilimo cha Korosho,  Madarasa ya Shule ya  Sekondari Mkiwa pamoja na matundu 10 ya vyoo vya shule hiyo.
Aidha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg Amour Hamad Amour ameweka Jiwe  la msingi ujenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Jiwe la msingi Zahanati ya Kijiji cha Ulyampiti sambamba na kugawa vyandarua ili kujikinga na Malaria na kuweka Jiwe la msingi kiwanda cha Mwananchi Cha kukamua Mafuta ya Alizeti sambamba na kufungua klabu ya wapinga Rushwa katika shule ya Sekondari Ikungi.
Mhe Mtaturu amesema kuwa Wilaya ya Ikungi inaunga mkono kauli mbiu ya mwaka huu 2017 ya Shiriki ukuzaji wa uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu.
Mkesha wa Mwenge wa Uhuru umefanyika katika viwanja vya shule ya Msingi Puma, Kijiji cha Puma ambapo pia umetembelea vikundi vya vijana na wanawake vya kiuchumi ambavyo vimewezeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kupitia mapato ya ndani, sambamba na Kuwapatia kadi za Bima ya Afya waathirika wa Virusi Vya UKIMWI na UKIMWI.
Aidha, June 30, 2017  Mwenge wa Uhuru Utaelekea Manispaa ya Singida ambapo utakabidhiwa katika Kijiji cha Unyamikumbi.
 
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni