Jumamosi, 17 Juni 2017

JAMII IMETAKIWA KUWAFICHUA WANAOJIHUSISHA NA VITENDO VYA UNYANYASAJI,UBAKAJI,UTEKAJI NA ULAWITI KWA WATOTO WADOGO

Posted by Esta Malibiche on JUNE 17,2017 IN NEWS

Wanafunzi kutoka shule mbalimbali Mkaoni Iringa wakiwa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkaoni Iringa.PICHA NA ESTA MALIBICHE.



N a Esta Malibiche
Iringa
JAMII imetakiwa  kuwafichua wale wote wanaojihusisha na vitendo vya  unyanyasaji  ikiwemo ubakaji, ulawiti kwa watoto wadogo  ili waweze kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Kilio hicho kimetolewa jana na watoto wa Mkoa wa Iringa katika Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika kijiji cha Kising’a  kata ya Kising’a Tarafa ya Isimani Mkoani Iringa,iliyo hudhuriwa na viongozi wa serikali,dini, vyama vya siasa na asasi zisizo za kiserikali.
Akisoma Risala  ya watoto katika  maadhimisho  hayo, ,Elizabeth Mhaso ambae ni mwanafunzi wa shule ya Msingi Ilambilole iliyopo katika Halamsahauri ya Iringa, alisema kuwa  kutokana na kauli mbiu ya mwaka 2017 inayosema ‘’Maendeleo endelevu 2013;Imarisha ulinzi na fursa sawa kwa watoto’’ ujumbe huu unawataka wazazi,walezi,serikali na jamii kwa ujumla  kuimarisha ulinzi na usalama kwa watoto sambamab na kuwapatia watot wa kike na kiume  pamoja na watoto walemavu fursa sawa katika Nyanja za Elimu,kiutamaduni na kiuchumi.
Mhaso alisema swala la ulinzi na usalama kwa watoto linahitaji msukumo mkubwa katika jaamii nzima kwasababu kumekuwa kukitokea matukio ya unyanyasaji,ulawiti,ubakaji,utekaji  na  ukatili kwa watoto lakini jambo la kusikitisha na kushangaza familia zimekuwa zikifanya mapatano ya kificho na kumalizana wao kwa wao pasipo kuzifikisha katika vyombo vya sheria.,hivyo jitihada za makusudi zinahitajika katika kuelimisha jamii ili kuwafichua wale wanaojihusisha na vitendo hivyo.
‘’’Ndugu Mgeni Rasmi,Tunaomba Taifa letu lijikite katika kuimarisha familia zetu ili ziweze kuwajibika kikamilifu katika kuweka mikakati ya kutuendeleza watoto kwa kutulinda na kutupatia fursa sawa katika Elimu bora pamoja na kutupatia  haki ya kuishi katika mazingira salama,Afya bora,Chakula,Malazi,Kulindwa,Kusilizwa na kushirikishwa.Pia  juhudi za makusudi zifanyike ili kujenga uelewa kwa familia zetu kutumia fursa sawa kwa watoto bila kujali jinsi ya mtoto na hali ya maumbile ya mtoto’’’’’’Alisema Mahaso.
 Alisema Familia ambayo ni  msingi wa maisha na yenye jukumu la malezi,makuzi na ulinzi wa Mtoto imeonekana kulegalega katika kutoa Fursa sawa kwa watoto kwani baadhi ya wazazi wamejengea tafsiri potofu za kutokumwendeleza mtoto wa kike na kuona kwamba yeye ni wa kuolewa tu,hivyo kufifisha ndoto za maendeleo ya watoto wa kike.
 ‘’’Ndugu Mgeni Rasmi,sisi watoto tunasikitishwa sana na kitendo cha baadhi ya wazazi,walezi na jamii kwa ujumla  kuona baadhi ya watoto wenye ulemavu  wakiachwa bila kupelekwa shule na wengine kufichwa kabisa ndani wasionekane katika jamii,hivyo kupoteza fursa mbalimbali ambazo watoto walemavu wangeweza kuzipata na kuwa na mchango katika maendeleo ya Nchi.Pia kuna baadhi ya wazazi wamekuwa  imani potofu ya kuwa mtoto wa kiume anastahili kuchunga na kulinda mifugo ya familia,hivyo kufifisha ndoto za maendeleo ya watoto wa kiume pia imeombwa kuongeza nguvu    kupambana dhidi ya waoto unaofanyika majumbani,Shuleni na katika jamii kwa ujumla’’’’Alisisitiza Mhaso.
 Aidha katika maadhimisho hayo,Mgeni Rasmi alikuwa ni Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamuhuri Davidi Willium aliyemuwakilisha mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza,akitoa hotuba  yake  alisema kuwa pamoja na juhudi za serikali kuandaa Sheria,Sera,Miongozo na mkakati mbalimbali  ya kumjali mtoto,kumekuwepo na changamoto  zinakazo kwamisha utekelezaji wa programu za kumwendeleza,kumjenga mtoto wa kike na kulinda haki zake.
Jamhuri alisema changamoto hizo nipamoja na ukosefu wa rasilimali fedha,ushiriki mdogo wa jamii katika kuatatua tatizo la uvunjaji wa haki za watoto,na uelewa mdogo wa jamii kuhusu haki za watoto.Kwa hali hiyo,umuhimu wa swala la ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi yanoayohusu maisha yao upewe kipaumbele ili sauti zao ziweze kusikika na mchango wao uonekane katika kutekeleza haki zao.
 ‘’’’Sote ni walezi wa familia ,niawaombe tuungane kwa pamoja kukemea vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia hususani ubakaji na ulawiti dhidi ya watoto ambao umeendelea kujitokeza katika mkoa wetu.Kibaya zaidi unyanyasaji huu umekuwa ukiwahusisha  watu wazima na watoto wadogo,hivyo daima tuhakikishe usalama wa watoto wetu unaimarika  kikamilifu katika kuwalinda na kuwahakikishia  usalama wa maisha yao kwa kutoa ushahidi ili waototo waweze kupata haki zao.
 Alisema Madhara ya vitendo vya ubakaji  katika jamii ni pamoja na wahanga wa vitendo hivi kupata athari za kisaikolojia kama kutokujiamini,kuwa na wasisawasi, kutokuwa na furaha kutokana na matokeo ya vitendo hivyo,ugumba ,mimba za utotoni na kuharibu mahusiano baina ya wanajamii.
‘’’’Vitendo hivi viovu vinadidimiza sana jitihada za Mkoa wa Iringa za kupambana na maambukizi ya virusi vya Ukimwi na Ugonjwa wa ukimwi.Tafadharini wanaume na wanawake wote tuungane kwa pamoja tupaze sauti ili kukabiliana na changamoto hii kwa manufaa ya Taifa zima.’’’’Alisema Jamuhuri.
Alisema juhudi za kuanzisha mabaraza ya watoto katika Mkoa wa Iringa zinaendelea,ambapo Halmashauri ya Iringa imeshaanza kwa kuunda mabaraza ya watoto katika kata 22 ambayo yanafanya kazi nzuri ya kutetea haki za watoto ukilinganisha na Halmashauri zingine za Mkoa wa Iringa ambazo zimeunda mabaraza machache.Pia aliwaagiza wakurugenzi wote washirikiane na wakuu wa wilaya amabo Halmashauri zao hazijakamilisha uundwaji wa  mabaraza ya watoto katika ngazi  zote kwa mujibu wa serikali wahakikishe mabaraza  hayo yanaundwa haraka iwezekanavyo.
‘’’Kwa hali ilivyo sasa,ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi ya masuala yanayohusu maisha yao ni suala linalotiliwa makazo sana Nchini Tanzania hasa baada ya kuridhia makataba wa haki za watoto mwaka 1991,baada ya hapo Serikali iliona umuhimu  wa ushiriki  wa watoto katika kufanya maaamuzi mbalimbalinkwa utaratibu rasmi na wenye muendelezo mzuri hasa baada ya tukio la ushiriki wa watoto katika kikao maalum  kilichoandaliwa na umoja wa Mataifa cha mwaka 2002 na hivyo  kupendekeza uwepo wa chombo mahususi cha kitaifa cha uwakilishi wa kudumu wa watoto  chini ya usimamizi wa wizara ya maendeleo ya Jamii ,Jinsia na watoto’’’’Alisema Jamuhuri.
Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamuhuri David Willium akizungumza katika madhimisho ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika jana katika kijiji cha Kising'a ,Halmashauri ya wilaya ya Iringa,na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa serikali,Dini,Vyama vya Siasa na asasi zisizo za kiserikali.
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali Mkaoni Iringa wakiwa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkaoni Iringa
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali Mkaoni Iringa wakiwa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkaoni Iringa.
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali Mkaoni Iringa wakiwa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkaoni Iringa
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali Mkaoni Iringa wakiwa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkaoni Iringa.


Mgeni rasmi Jamuhuri David Willium,ambae ni Mkuu wa wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa,akipokea zawadi zilizotolewa na wananchi, viongozi wa serikali ya mitaa pamoja na vikundi vya mbalimbali vya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkoani Iringa.
Mgeni rasmi Jamuhuri David Willium,ambae ni Mkuu wa wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa,akipokea zawadi zilizotolewa na wananchi, viongozi wa serikali ya mitaa pamoja na vikundi vya mbalimbali vya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkoani Iringa.
Mgeni rasmi Jamuhuri David Willium,ambae ni Mkuu wa wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa,akipokea zawadi zilizotolewa na wananchi, viongozi wa serikali ya mitaa pamoja na vikundi vya mbalimbali vya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkoani Iringa.
Mgeni rasmi Jamuhuri David Willium,ambae ni Mkuu wa wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa,akipokea zawadi zilizotolewa na wananchi, viongozi wa serikali ya mitaa pamoja na vikundi vya mbalimbali vya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkoani Iringa.
Mgeni rasmi Jamuhuri David Willium,ambae ni Mkuu wa wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa,akipokea zawadi zilizotolewa na wananchi, viongozi wa serikali ya mitaa pamoja na vikundi vya mbalimbali vya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkoani Iringa.
Mgeni rasmi Jamuhuri David Willium,ambae ni Mkuu wa wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa,akipokea zawadi zilizotolewa na wananchi, viongozi wa serikali ya mitaa pamoja na vikundi vya mbalimbali vya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkoani Iringa.
 Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela ,akipokea zawadi zilizotolewa na wananchi, viongozi wa serikali ya mitaa pamoja na vikundi vya mbalimbali vya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkoani Iringa.
Mkuu wa wilaya ya Kilolo Bi.Asia Abdallah ,akipokea zawadi zilizotolewa na wananchi, viongozi wa serikali ya mitaa pamoja na vikundi vya mbalimbali vya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Iringa Mkoani Iringa.
 
Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamuhuri David Willium,pamoja na  Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela wakicheza ngoma ya Mangala  iliyotumbuizwa na kikundi  katika Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika hapo jana.
Mgeni rasmi,Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamuhuri David Willum akimkabidhi hati maalum mwakilishi wa Radio Maria Jimbo Katoliki la Iringa Thobias Augustino Myovela.
Mgeni Rasmi na Meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja na vikundi vya sanaa.
Mgeni Rasmi na Meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja na vikundi vya sanaa.

Mgeni Rasmi na Meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi kutoa shule mbalimbali walioshiki katia maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika
Mgeni Rasmi na Meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja  washindi  waliopata tuzo ya Maalum.
Mgeni Rasmi na Meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja  washindi  waliopata tuzoMaalum.








































0 maoni:

Chapisha Maoni