Jumamosi, 21 Aprili 2018

SERIKALI YA CCM YANG'ARISHA IKUNGI KWA UMEME

 Waziri wa Nishati Medard Kalemani akiwa na mkuu wa wilaya ya Ikungi Miraji Mtaturu na mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu wakati wa uzinduzi wa uwashaji wa umeme kijiji cha Nkuninkhana wilayani Ikungi.
 Mkuu wa wilaya ya Ikungi Miraji Mtaturu akijadiliana jambo na Waziri wa Nishati Dk.Medard  Kalemani wakiwa  kwenye kijiji cha Nkunikhana .
 Mkuu wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida Miraji Mtaturu akizungumza wakati akimkaribisha Waziri wa Nishati Dk.Medard  Kalemani kuongea na wananchi kabla ya kuzindua uwashaji wa umeme kijiji cha Nkuninkhana wilayani humo.
 Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu akitoa salaam kabla Waziri wa Nishati Dk.Medard Kalemani  hajazungumza na wananchi wa kijiji cha Nkhuninkana.

 Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya  Ikungi Mika Likapakapa akitoa salaam wakati wa zoezi la kuwasha umeme kijiji cha Nkuninkhana.
Wanachi wa kijiji cha Nkhuninkana wakionyesha furaha yao baada ya kuelezewa neema ya umeme katika kijiji chao.

..............................................................

WAZIRI wa Nishati Dk.Medard Kalemani amefanya ziara na kukagua miradi ya umeme iliyopo wilayani Ikungi mkoani Singida huku akiwasisitiza wakandarasi kumaliza miradi kabla ya muda uliowekwa ili kuweza kujitathimini kabla ya mkataba kuisha.

Dk. Kalemani amesema serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk.John Pombe Magufuli imedhamiria kufikisha umeme kila kijiji na kitongoji hivyo wakandarasi wanapaswa kuunga mkono dhamira hiyo kwa kufanya kazi kwa uadilifu.

“Pamoja na kuwasisitiza,niwapongeze pia wakandarasi mnaoendelea kujenga miundombinu ya umeme,nilishawapa maelekezo ya kuwasha umeme vijiji vitatu kila wiki na leo tutawasha kijiji cha Ikungi Utaho, Nkhuninkana na Kipumbuiko,”alisema Dk.Kalemani.

Amesema serikali imetoa shilingi bilioni 15 kwa ajili ya miradi ya umeme nchi nzima na umeme ni wakutosha baada ya kuzindua mitambo ya Kinyerezi ambapo kwa sasa kuna ziada ya megawati 194.

“Maombi yaliyotolewa na mkuu wa wilaya yenu Miraji Mtaturu na ya mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu nimeyasikia na nitayazingatia kwa kuwa viongozi hawa wanasimamia maendeleo ya wananchi vizuri sana,nielekeze tu umeme ukifika kwenye kijiji ufike na kwenye vitongoji vyake na kila nyumba itawekewa umeme,

“Mkoa huu wa Singida REA awamu ya tatu kwa sehemu ya kwanza utavifikia vijiji 150 na kubakiza vijiji 72 tu ambavyo vitamaliziwa na sehemu ya pili na ya tatu ya REA awamu ya tatu kufikia mwaka 2021 hivyo nawaomba wananchi mtumie fursa hii adimu kujiinua kiuchumi,”alisema Dk. kalemani.
Amesema msingi wa kufanya yote hayo ni kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM 2015 -2020 katika kuwaletea wananchi Maendeleo na hasa kufikia Tanzania ya Viwanda.

Akisoma taarifa mbele ya dokta Kalemani,meneja wa Shirika la Umeme Nchini(TANESCO)mkoa wa Singida mhandisi Abdulrahman Nyenye ameeleza kuwa Mkoa umeendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme kupitia Mradi wa umeme vijijini  (REA )na kwamba REA awamu ya Pili ilianza novemba 25 mwaka 2013 hadi novemba 24 mwaka  2015 na ilitarajiwa kufikia vijiji 88 na kuunganisha wateja 8,332.

“Katika awamu hiyo vilitakiwa vijiji 88 ila vilivyounganishwa ni vijiji 35 mpaka sasa hii ni kutokana na mkandarasi kutokuzingatia mkataba na alishaondolewa na kupatikana mkandarasi mwingine,na kwa sasa mradi wa BACKBONE unaendelea katika mkoa wa Singida ambapo vijiji 39 vitapatiwa umeme,”alisema meneja huyo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya Mtaturu amempongeza dokta Kalemani kwa kazi nzuri anayofanya ya kuzunguka nchini kuangalia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme jambo linalodhihirisha namna anavyomuwakilisha mh Rais vizuri.

“Pamoja na pongezi hizo kwako sisi wakazi wa Ikungi tunakuomba utupelekee shukrani zetu kwa  mhe Rais kwa kutuweka kwenye mpango wa miradi ya REA mwaka huu kwa mara ya kwanza ambapo  vijiji 41 vitaunganishwa kwenye umeme ikiwa ni pamoja na vijiji 11 vya backbone,

"Hii ni historia mpya inaandikwa kwa kupata umeme toka nchi imeumbwa,nikuhakikishie mh waziri umeme huu utatusaidia kuchochea uchumi wa wananchi wetu,kwa sasa mkoa wetu tupo kwenye mkakati wa kuhakikisha tunajenga viwanda ili kuunga mkono juhudi za mhe Rais kuifikia Tanzania ya Viwanda na Uchumi wa kati kwa kuchakata mazao ya kilimo kama alizeti na viazi,mifugo na kuweka kiwanda cha chumvi bonde la Misughaa na hivyo kuongeza mnyororo wa thamani ya mazao ya wakulima.,”aliongeza Mtaturu.

Amesema kwa kuwa sasa wanapata umeme vijiji 41 kati ya 101 wanaomba REA awamu ya tatu iunganishwe kwa pamoja ili kuvifikishia umeme vijiji vyote mapema na kuyaweka kwenye mpango kwa sasa  maeneo yanayohitaji umeme kwa umuhimu wake kwa ajili ya kuvuta maji kwa wananchi kama Matongo,Ulyampiti, Ihanja na Kimbwi.

Naye, Mbunge Kingu amempongeza  Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya ya kumsaidia Rais kwenye Sekta ya Nishati na kuomba vijiji vilivyosahaulika katika eneo la jimbo lake viingizwe  kwenye mpango.

“Pamoja na pongezi kwako nimpongeze pia mkuu wa wilaya yetu Mtaturu kwa kusimamia vizuri Maendeleo ya wananchi wa Ikungi,na kutokana na kazi nzuri hii mkuu wa wilaya nakukabidhi shilingi laki 400,000 hii ikiwa ni mchango wangu kwa wananchi katika kuwasaidia gharama za kuweka umeme,hapa ni shilingi 5,000 kwa kaya 80,”alisema kingu.

0 maoni:

Chapisha Maoni