Jumapili, 29 Aprili 2018

RAIS MAGUFULI AANZA ZIARA LEO MKOANI IRINGA,AFUNGUA MRADI WA BARABARA WENYE THAMANI YA BILL.207.4

Posted by Esta Malibiche on April 29,2018 IN KITAIFA

Rais  Dkt Magufuli na  viongozi wengine  wakishirikiana kufungua  barabara.



Rais  Dkt  John Magufuli na  viongozi mbali  mbali  wakikata  utepe  kufugua barabara ya Migori-Fufu  iliyojengwa  kwa mkopo  toka  benk ya  Afrika  na Japani   katika uziduzi uliofanyika  kijiji  cha Ndolela  wilaya ya  Iringa
Waziri  wa Ardhi  nyumba na maendeleo ya makazi na mbunge wa Ismani  katikati mwenye  miwani akiwa na  spika Job Ndugai na  viongozi wengine
MNEC  Iringa Salima Asas  akiwa na mwenyekiti wa CCM mkoa wa  Dodoma  kushoto na katibu wa CCM mkoa wa Iringa
Waziri  Lukuvi  akiongozana na spika  wa bunge Job Ndugai
Spika wa  bunge JOb Ndugai  akisalimiana na  viongozi wa  dini
Waziri  Lukuvi  akiwa na  viongozi mbali mbali wa chama tawala
Askafu wa KKKT Dayosisi ya Iringa Blaston Gavile  akisalimia
Mkuu wa   mkoa wa Iringa Amina Masenza  akiwa na viongozi  mbali mbali jukwaaa  kuu
Mke  wa Rais  mama  Janet Magufuli  akisalimia wananchi
Rais Dkt  Magufuli  na  viongozi  wengine  wakiwasili jukwaaa kuu
Waziri  Lukuvi  akitoa  salam kwa  wananchi
Mbunge wa Mafinga Cosato Chumi  akiwasilisha vchangamoto za  jimboni kwake mbele ya  rais
Mbunge wa  Kilolo Venance Mwamoto  akiomba  barabara ya Ipogolo -Kilolo  ikijengwa ipewe  jina la  Mfugale 
Mbunge wa  viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati  akiomba  Rais  kusaidia   Hospitali ya  Frelimo mashine
Mbunge Kabati  akitoa  salam za  wana Iringa mjini
Rais Dkt  Magufuli  akifungua barabara 
Rais  Dkt Magufuli na  viongozi wengine  wakishirikiana kufungua  barabara

Rais Dkt Magufuli  akimpongeza kwa  kumpa mkono  mkuu wa  mkoa wa Iringa Amina Masenza,mara baada ya ufunguzi wa barabara hiyo.
Mkurugenzi wa  kiwanda cha Iory  Iringa akiwa amejumuika na  wananchi kumsikiliza Rais Dkt Magufuli
Mwenyekiti wa ccm Iringa Vijijini [kulia]akiwa na kada wa CCM Arif Abri [katikati] na anaefuatia ni Mwenyekiti wa Uvccm Iringa Vijijini Mkala Mapesa na  viongozi  wengine
Wana CCM  Iringa mji  walivyoupamba mji wa Iringa


Na Esta Malibiche
Iringa
RAIS  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli amefungua barabara ya Iringa,Migori Fufu iliyojengwa kwa kiwango cha rami yenye umbali wa KM 189.

Akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Iringa jana wakati wa uzinduzi barabara uliofanyika  katika kijiji cha Ndolela kata ya Kihorogota Tarafa ya Isimani Wilaya ya Iringa Mkoani Iringa,Mheshimiwa Rais aliwashukuru wafadhiri ambao ni Benki ya Maendeleo ya Afrika na Serikali ya Japan kwa kutoa mikopo yenye riba nafuu hivyo kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo.

"Tumepewa barabara,hivyo tunatakiwa tuchangamkie fursa kwa kujishughulisha na Biashara,kufuga na kulima mazoa tofauti yanayostahimili ukame.Ninawaomba Barabara hii kuitunza na iwe mkombozi wetu kwa kujiingizia kipato na si vinginevyo"


Rais Magufuli alisema Serikali imeamua kuwa Iringa iwe sehemu ya Mkoa wa Utalii kutokana na mbuga kubwa ya wanyama iliyopo.
Tumeamua kuutengeneza uwanja wa Nduli kuwa wa rami ili ndege ziweze kutua ili wananchi wa Iringa waweze kunufaika kwa kutumia fursa zinazotokana na watalii.


Aliwataka wananchi kuijenga Nchi kwa   kufanya kazi kwa bidiii kila mmoja katika nafasi yake ili pato la Nchi liendelee  kuongezeka.Pia aliwasihi watanzania kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuondokana na ajali zinazoweza kuepukika.

 Wakati huo huo amezitaka Halmashauri kuweka mikakati ya kuwapunguzia Wananchi ushuru katika Mazoa ili waweze kunufaika na Kilimo na hivyo kujikwamua kiuchumi.


Akisoma taarifa  ya Mradi wa ujenzi wa barabara,mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng.Joseph Nyamhanga alisema kuwa kiasi cha Bil.207.4 zimegharimu ujenzi huo,ambapo Tz.imechangia 12.8 %,Benki ya  Maendeleo ya Afrika 65.9% na Serikali ya Japan imechangia 21.3%.

Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika   Dejene Demessie akitoa  salam kutoka Benki hiyo alisema kuwa Benki inaipongeza Serikali ya awamu ya Tano chini ya Uongozi wake Rais Magufuli kwa kutekeleza miradi yake kwa wakati.

"Hii inaleta Matumaini makubwa kwa wananchi na wale wanaojitoa kusaidia ili waendelee kusaidia"

Demessie alisema Benki ya Maendeleo ya  Afrika  inaipongeza Serikali ya awamu ya Tano  kwa hatua  ya kukuza uchumi wa Nchi.

"Tunaamini barabara hii itaweza kuboresha maisha ya wananchi  kiuchumi kwa kufanya biashara hivyo kujiingizia kipato.Pia Benki inatambua  vipaumbele vilivyowekwa kuhakikisha  Maendeleo  ya uchumi yanaongezeka" Alisema 

Nae Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na mawasiliano Makame Mbarawa alisema kuwa kukamilika kwa barabara hii kutarahidisha usafiri na usafirishaji  katika mikoa ya Iringa na Dodoma pamoja na mikoa jirani.

"Mheshimiwa Rais  Wizara yangu itahakikisha  fedha zilizotengwa kwq ajili ya Miradi ya Barabara zinatumika ipasavyo huku tukiakikisha barabara inatunzwa" Alisema Waziri Mbarawa



Alisema Barabara hii ya Iringa_Migori_Fufu ni sehemu ya  barabara ya Iringa_Dodoma yenye KM 260.

0 maoni:

Chapisha Maoni