Jumanne, 3 Aprili 2018

DOROTH MWAMPOMA AWATAKA WAZAZI KUWASOMESHA WATOTO


Posted by Esta Malibiche on April 3,2018 in NEWS
 Jengo la utawala la Shule ya Sekondari wenda.

Shule ya Sekondari Wenda iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya  Mbeya Vijiji Mkoani Mbeya,eneo la Mbalizi,imewataka wazazi kuona umuhimu wa Elimu kwa kuwasomesha watoto  wao.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Uhusiano  wa Shule hiyo Doroth Mwampoma wakati akizungumza na mtandao huu wa Habari [KALI YA HABARI BLOG]ofisini kwake,ulipotembelea shule hiyo jana kwa lengo la kufanya mahijiano maalum.

Doroth alisema kuwa shule hiyo ina wanafunzi  mchanganyiko ambao wanatoka ndani ya Nchi na Nje,yenye malezi bora na inamjerngea mtoto uwezo wa kufanya vizuri katika masomo yake,na wanafunzi wote ni wa bweni.

'Toka Shule hii ilipoanza wanafunzi hawajawahi feli katika matokeo ya kidato cha pili,nne na sita.Hii ni kutokana na umahili wa walimu wetu katika ufundishaji.Tuna walimu wa kutosha kabisa,mazingira ya shule ni rafiki,vyumba vya madarasa vipo vya kutosha,na mazingira mazuri ya mkumfanya mwanafunzi aendelee kujifunza zaidi na zaidi'Alisema Doroth

Doroth alisema kuwa  maendeleo miongoni mwa jamii yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na kiwango cha uwekezaji katika elimu, ni vema jamii iwekeze kutambua na kuona umhimu katika elimu  kwa kuwasomesha watoto wao  ili wawaeze  kujikwamua na umaskini uliopo na kupambana katika soko la ajira. 




Ninawaomba wazazi wawalete  watoto wao katika shule  ya sekondari Wenda,ada zetu ni nafuu na unalipa kidokidogo.Pia,Fomu za kujiunga na Shule hii zinapatika wenda sekondari na katika tofutti ya wenda ambayo ni www.wenda High school.com

Aidha aliwataka  wazazi na walezi kote nchini kuwa msatari wa mbele na kuona umuhimu wa kuwekeza katika elimu.Nawaomba wawalete katika Shulea ya Sekondari Wenda ili wawaeze kupata elimu iliyobora.























0 maoni:

Chapisha Maoni