Jumamosi, 21 Aprili 2018

MKUU WA MKOA WA IRINGA AMINA MASENZA AWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KUMPOKEA RAIS MAGUFULI MEI MOSI

Posted by Esta Malibiche on April 21,2018 IN NEWS

Mkuu  wa mkoa wa  Iringa  Amina  Masenza akizungumza na vyombo vya Habari 

MKUU wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amewaomba wakazi wa Mkoa wa Iringa kujitokeza kwa wingi kumlaki Rais wa Jmuhuri ya Muungano wa Tanzania  Dk. John Magufuli anaetarajia kuwa mgeni rasmi katika Maaadhimisho ya Sherehe ya Siku ya wafanyakazi Duniani,[Mei Mosi ambayo kitaifa yanafanyika Mkoani Iringa katika uwanja wa Samora,uliopo Manispaa ya  Iringa.

Akizungumza na Vyombo vya Habari Ofisini kwake aliseama katika  kuelekea kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Mei Mosi kitaifa  matukio Mbalimbali yanaendelea zikiwemo ikiwemo semina,michezo na makongamano yatakayofanyika katika wilaya zote za Iringa.


“Kuelekea kilele cha maadhimisho hayo ya mei mosi mwaka 2018 kutakuwa na michezo mbalimbali itakayokuwa inachezwa katika viwanja mbalimbali hapa mkoani Iringa na michezo hiyo ni kama ifuatayo mpira wa miguu,mpira wa pete,kuvuta kamba,bonanza la michezo mbalimbali na michezo hii ilianza tarehe 17 /04 /2018  na itahitimishwa 30 /04 / 2018” alisema masenza


Akielezea  juu ya maandalizi ya  sherehe  za mei  mosi  mkoani  Iringa  alisema  kwa  sehemu  kubwa   maandalizi yanakwenda  vizuri na  wamepata  ratibu ya  kuzunguka  wilaya  zote za  mkoa  wa Iringa kutoa elimu  pamoja na kututana na  wafanyakazi ili  kujua  changamoto  zao.

“Tumejiridhisha kuwa kila kitu kinaenda kama tulivyopanga ndio maana leo tunahuru wa kusema kuwa mei mosi itafanyika kwa mafanikio makubwa mno” alisema

 Hata hivyo  Masenza aliwataka  wafanyakazi   kujitokeza  kwa  wingi  kushiriki sherehe  hizo  na  kuwa  kupitia sherehe  hizo  watapata fursa ya  kujua  mikakati ya  serikali  dhidi ya wafanyakazi  hapa nchini.


Kwa upande wake katibu Mkuu wa TUCTA Taifa Dk.Yahaya Msigwa alisema wananchi wanatakiwa kuchangamkia fursa ya  Mei Mosi kujiingizia kipato.

‘Tunategemea kwa kipindi hiki ambacho Mkoa unapokea ugeni wananachi hasa wale wenye nyumba za kulala wageni,mama ntilie na wafanyabiashara wadogowadogo na wakubwa’Alisema Msigwa

‘Wafanyakazi wanapopewa elimu  tunapunguza matatizo kwa wafanyakazi hivyo ninawaomba  waendelee kujitokeza katika makongsamano yanayoendelea ili wawaeze kujifunza na kupata majibu ya yale yanayowatatiza mahali pao pa  kazi’Alisema Dk.Msigwa

Aidha aliwataka wananachi wa Mkoa wa Iringa kuitumia  vizuri Mei Mosi  katika biashara ili kutengeneza mahusiano mazuri






.

0 maoni:

Chapisha Maoni