Alhamisi, 19 Aprili 2018

RAIS WA TUCTA AWATAKA WANANACHI MKOANI IRINGA KUITUMIA MEI MOSI KAMA FURSA

Posted by Esta Malibiche on April 19,2018 in NEWS

Rais  wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi (TUCTA) Tumaini Nyamhokya akizungumza na vyombo vya Habari ,kushoto kwake ni Paulo Sangeze  Mwenyekiti  Tuico taifa.


Na Esta Malibiche
Iringa.
Rais  wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi (TUCTA) Tumaini Nyamhokya amewataka wafanyakazi,wajiri,wananachi hasa wakazi wa amkoa wa IRINGA  wametakiwa kushiriki katika matukio  mbalimbali  yakiwemo kongamano,Semina  na Maonesho ili kufikia Kilele cha Mei Mosi 2018 kinachotarajiwa kufanyika Mkoani Iringa.
Akizungumza na vyombo vya Habari Mkoani hapa  kuhusu maandalizi ya Mei Mosi kitaifa alisema kuwa katika kuelekea kilele kutakuwa na matukio muhimu  zikiwemo semina mbalimbali  mahala pa kazi na sekta zisizo rasmi zikiwa na maudhui ya kuelimisha sheria za kazi,Afya na Usalama kazini.
Nyamhokya alisema kuwa kabla ya kilele kutakuwa na makongamano mawili ya kimkoa na moja la kitaifa,ambapo yanatarajiwa kufanyika Wilayani Mufindi na Wilayani Kilolo huku yakiambatana na kongamano kubwa la kitaifa litakalohusu TANZANIA YA VIWANDA,ambalo litafanyika katika ukumbi wa kichangani Manispaa ya Iringa na litakalo washirikisha  viongozi wa kitaifa,wanazuoni,waajiri,viongozi wa vyama vya wafanyakazi na wafanyakazi kwa ujumla.
    ''Maadhimisho ya Mei Mosi 2018,yamebeba ujumbe usemao’Kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii nchini kulenge kuboresha mafao ya mfanyakazi,na Mgeni rasmi anatarajia kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli ‘alisema Nyamhokya na kuongeza kuwa



Michezo ya Mei Mosi ya fani mbalimbali inaendelea katika viwanja vya samora ambayo ilianza toka tarehe 16,4,2018 mpaka 30,4,2018.
Aidha alisema kutakuwa na banda ya maonesho ya huduma  na bidhaa kutroka taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi,wajasiliamali wakubwa na wadogo kutoka ndani ya  Mkoa na nje, na yatafanyika katika viwanja vya kichangani kuanza tarehe 25,4,2018 mpaka 28,4,2018.Pia kutakuwa na burudani zikiwemo Muziki wa dansi,kizazi kipya, ngoma za asili,kwaya na tenzi.

0 maoni:

Chapisha Maoni