Jumamosi, 2 Desemba 2017

DEOGRATIUS NDEJEMBI;UVCCM MKOA WA IRINGA KUWENI WAZALENDO KWA KUTANGULIZA MASLAI YA CHAMA MBELE

Posted by Esta Malibiche on DEC 2,2017 IN SIASA
Deogratiuas Ndejembi mkuu wa wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma akizungumza na wajumbe wa umoja wa uvccm mkoa wa Iringa katika mkutano mkuu wa 9 wa uvccm mkoa,akitangaza matokeo ya wasshindi wa ngazi mbalimbali ikiwemo ya uenyekiti wa uvccm mkoa wa iringa,aliwasihi washindi  kuwa wazalendo kwa kutanguliza maslai ya chama na jumuiya ya vijana mbele pamoja na kukipigania chama ili kiendelee kushika hatamu.PICHA ZOTE NA ESTA  MALIBICHE.
Na Esta Malibiche
Iringa
UMOJA wa vijana ccm mkoa wa Iringa umeandika historia mpya kumpata Mwenyekiti wa jumuiya hiyo mara baada ya kukaa takribani miaka 4 bila Mwenyekiti wa Uvccm mkoa.

Akitangaza matokeo ya kura za Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa katika mkutano mkuu wa 9,Msimamizi mkuu wa uchaguzi Deogratius Ndejembi ,ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma,aliwasihi washindi wa umoja wa vijana ccm walioshinda katika ngazi mbalimbali za jumuiya hiyo i kuwa wazalendo kwa kutanguliza maslai ya chama na jumuiya ya vijana mbele pamoja na kukipigania chama ili kiendelee kushika hatamu.

Ndejembi alisema hakuna Taifa linalosonga mbele kimaendeleo pasipo kumtegemea kijana,hivyo aliwataka kuweka maslai ya chama mbele na wasikubali kutumika na watu kwa maslai yao binafsi hivyo kukivuruga chama na jumuiya ya Vijana.

"Kura zilizopigwa ni 294,halali 193 iliyoharibika ni kura 1.Amoni..kapata kura 7,Jafari kikoti kapata kura 45 na Kenani Kihongosi kapata kura 235.Hivyo basi kutokana na matokeo haya ninamtangaza Kenani Kihongosi kuwa ndiye Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa wa Iringa.Uchaguzi umeisha kikichobaki ni kumpa ushirikiano,tuwe na sauti moja  juu ya maslai mapana ya jumuiya na chama"" Alisema Ndejembi.

Kwa upande wa Msimamizi msaidizi ambae pia ni Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalah aliwataka wawe viongozi wenye kuleta mabadiliko katika jumuiya,kujiepusha na makundi ambayo yanaweza kuwagawa vijana.

‘Msikubali kubezwa na vyama vya upinzani,tembeeni kifua mbele kwa kufanya kazi kwa bidii ili kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mwenyekiti wetu wa ccm Taifa Rais Magufuli’’Alisema Asiah na kuongeza kuwa

 ‘’Uongozi wa jumuiya ya vijana siyo ajira bali ni uzalendovijana  moja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Iringa umempata mwenyekiti mpya bwana Kenani Kihongosi alichaguliwa kwa kura nyingi za kishindo na kurudisha matumaini mapya ya kuanza safari ya kuijenga CCM mpya kwa vijana wa mkoa huu wa Iringa’’Alisema Asia

Nae katibu wa jumuiya ya umoja wa vijana ccm mkoa wa Iringa,Jemsi Mgego akitoa pongezi kwa washindi walioshinda katika ngazi mbalimbali za uongozi wa umoja huo alisema kazi kubwa ya uvccm ni kuwapika vijana  kwa imani na itikadi ya ccm,na kwa mtu yeyote atakae hubiri utengano na kuleta mpasuko ndani ya umoja wa vijana wa ccm basi hastahili kuwa kiongozi na kuwa mwanaccm.
""Huu sasa ni wakati wakujenga jumuiya imara na madhubuti ikiwa nipamoja na  kuvujna makundi ya uchaguzi na kuwa kitu kimoja  ili kuiletea hedhima jumuiya hii iliyopotoea  kwa miaka minne bila juwa na Mwenyekiti wa uvccm mkoa wa Iringa"" Alisema Mgego na kuingeza kuwa

""Mbele yetu tuna kazi kubwa ya kulikomboa jimbo la Iringa mjini,tukishirikiana kwa pamoja kama tulivyoshirikiana katika uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya kitwiru hakika tutafanikiwa na hatimae jimbo kurudi katika mikono ya chama cha Mapinduzi"" Alisema Mgego

Akiwashukuru kwa kumchagua kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya umoja wa Vijana ccm MKOA WA Iringa,Kenani Kihongosi alisema kuwa atahakikisha jumuiya zote za umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi zinarudi na kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na kuhakikisha wanapata wanachama wapya ambao itakuja kuwa nguzo ya chama hicho hapo baadae.

“Ninawashukuru wajumbe kwa kuniona kuwa ninafaa,ni miaka mine tumekaa kwa unyonge bila kuwa na Mwenyekiti,ninawaomba tushirikiane kwa pamoja katika kufanya kazi na kuhakikisha kila kitu kinaenda kama kilivyokusubiwa na kuhakikisha chama kinapata matokeo chanya kutoka kwetu vijana hivyo naomba mniunge mkono kuhikikisha tunakuwa wamoja” alisema Kihongosi

Kihongosi aliwataka vijana kufanya kazi na kuhakikisha wanaendelea kumuunga mkono Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuijenga CCM na Tanzania mpya.


“Sisi ndio vijana ambao tunatakiwa kuonyesha mfano kwa kufanya kazi na kuonyesha wapinzani wa mkoa wa Iringa kuwa sasa kuna UVCCM ambavyo inania ya kuhaikisha inaumaliza upinzani uliopo hapa mkoana na CCM ikachukua jimbo la Iringa Mjini” alisema Kihongosi
Deogratiua Ndujembi mkuu wa wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma akizungumza na wajumbe wa umoja wa uvccm mkoa wa Iringa katika mkutano mkuu wa 9 wa uvccm mkoa, alisema hakuna Taifa linalosonga mbele kimaendeleo pasipo kumtegemea kijana,hivyo aliwataka kuweka maslai ya chama mbele na wasikubali kutumika na watu kwa maslai yao binafsi hivyo kukivuruga chama na jumuiya ya Vijana.
Msimamizi msaidizi ambae pia ni Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalah akizungumza alisema kuwa Uongozi wa jumuiya ya vijana siyo ajira bali ni uzalendovijana  moja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Iringa umempata mwenyekiti mpya bwana Kenani Kihongosi alichaguliwa kwa kura nyingi za kishindo na kurudisha matumaini mapya ya kuanza safari ya kuijenga CCM mpya kwa vijana wa mkoa  wa Iringa.

Msimamizi msaidizi ambae pia ni Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalah akizungumza aliwataka viongozi waliochaguliwa kuwa wenye kuleta mabadiliko katika jumuiya,kujiepusha na makundi ambayo yanaweza kuwagawa vijana.
Katibu wa chama cha mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa Christopher Magala,akizungumza alisema,sasa ni wakati wakujenga jumuiya imara na madhubuti ikiwa nipamoja na  kuvujna makundi ya uchaguzi na kuwa kitu kimoja  ili kuiletea hedhima jumuiya hii iliyopotoea  kwa miaka minne bila juwa na Mwenyekiti wa uvccm mkoa wa Iringa.

katibu wa jumuiya ya umoja wa vijana ccm mkoa wa Iringa,Jemsi Mgego akitoa pongezi kwa washindi walioshinda katika ngazi mbalimbali za uongozi wa umoja huo alisema kazi kubwa ya uvccm ni kuwapika vijana  kwa imani na itikadi ya ccm,na kwa mtu yeyote atakae hubiri utengano na kuleta mpasuko ndani ya umoja wa vijana wa ccm basi hastahili kuwa kiongozi na kuwa mwanaccm.

Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa vijana ccm Mkoa wa Iringa,Kenani Kihongosi aliyechaguliwa  kwa kura 235 kati ya kura 294 kuiongoza jumuiya hiyo.










 




0 maoni:

Chapisha Maoni