Alhamisi, 2 Machi 2017

WAZIRI WA AFYA AZINDUA RIPOTI YA HALI YA NDOA ZA UTOTONI

Posted by Esta Malibiche on MARCH 2,2017 IN NEWS

HER1
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Ummy Mwalimu  akiwa tayari kwa uzinduzi wa Ripoti ya hali ya ndoa za utotoni Nchini.
HER2
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Ummy Mwalimu  akionesha Ripoti ya hali ya ndoa za utotoni Nchini.
HER3
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Ummy Mwalimu  akionesha Ripoti ya hali ya ndoa za utotoni Nchini.
HER4
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Ummy Mwalimu  akiwa na viongozi wa dini katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua  Ripoti ya hali ya ndoa za utotoni Nchini
……………………………………………………………………..
Na Anthony Ishengoma
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Ally Mwalimu ameagiza walimu wakuu wote wa shule za msingi chini kutekeleza marekebisho ya sheria ya elimu ya mwaka 2016 kwa vitendo kwa kuwataka kuwasilisha taarifa za wasichana waliopata mimba shuleni kwa kila kamishina wa elimu kama ilivyo agizo la sheria hiyo.
Aidha amewaagiza watendaji wa Wizara yake kufuatilia taarifa za wanafunzi wakike walioacha shule kutoka kwa kila Afisa Maendeleo wa Jamii katika ngazi ya Wilaya kuwapatia mrejesho wa kina kuhusu agizo lake kwa walimu wakuu kama hatua muhimu ya kutekeleza agizo la sheria ya elimu kama ilivyofanyiwa marekebisho na bunge mwaka 2016.
Amesema hayo katika hotuba yake ya ufunguzi wa ripoti ya hali ya mimba za utotoni hapa nchini iliyofanyika kote nchini chini ya mtandao wa mashirika yasiyo kuwa ya kiserikali ikiongozwa na shirika la Jukwaa la Utu wa Mtoto Tanzania, ufunguzi huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Waziri Ummy amewambia wajumbe walioshiriki ufunguzi huo kuwa kwa kuwa mabadiliko ya sheria ya ndoa hususani kifungu namba kumi na tatu cha sheria ya ndoa ya mwaka 1971 hayajafanyika ni bora kwenda mbele zaidi kutekeleza sheria ya elimu kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2016 ili kutekeleza kwa vitendo hatua za kupinga ndoa za utotoni.
Amesema kuwa sheria ya ndoa ya mwaka 1971 kimsingi inahalalisha uwepo wa vitendo vya ndoa za utotoni na kuahidi kuwa ataendelea kupigania marekebisho katika ndoa hiyo mara baada yakuwasiliana na waziri wa sheria na mambo ya katiba.
Katika kuhakikisha Serikali na Mashirika yasiyo ya kiserikali yanapambana na tatizo la ndoa za utotoni ameyataka mashirika hayo kuweka nguvu zake katika maeneo ya vijijini kwani ofisi nyingi za mashirika hayo zimejikita maeneo ya mjini hasa katika jiji la Dar es Salaam.
Aidha amehaidi kuwa serikali itaboresha mazingira ya mtoto wa kike kusoma ikiwemo ujenzi bora wa vyoo pamoja na uendelezaji wa sera rafiki na sheria kwa mtoto wa kike kujipatia elimu bila vikwazo ikiwemo elimu ya Afya na uzazi ili mtoto wa kike aweze kutambua thamani yake katika jamii na taifa kwa ujumla.
Ufunguzi huo umefanyika wakati serikali na mashirika ya yasiyo ya kiserikali wakiendelea kuadhimisha siku ya kimataifa ya wanawake ambayo kilele chake ni Machi 8, mawaka huu.

0 maoni:

Chapisha Maoni