Jumatatu, 27 Machi 2017

HAMLASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA YAWAKABIDHI VIJANA NA WANAWAKE HUNDI YENYE THAMANI YA MILL.70,000,000

Posted by Esta Malibiche on MARCH 27,2017 IN NEWS


HALMASHAURI ya Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa imetoa mkopo kwa vikundi 35 vya wanawake na vijana ikiwa ni utekeleza wa agizo la serikali la kutenga asilimia kumi (10%) ya mapato ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vijana na wanawake.

Akikabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 70,000,000/- kwa vikundi hivyo katika awamu ya pili ya kipindi cha mwaka 2016/2017, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa, Alex Kimbe amewataka kinamama na vijana kutumia fedha hizo kwa shughuli zilizokusudiwa ili ziweze kuleta manufaa na kuwatoa katika lindi la umasikini.

Kimbe alisema kuwa jumla ya vikundi 35 toka katika kata zote 18 za Manispaa ya Iringa vimepokea mikopo, ambapo vikundi 16 vya vijana vimepokea jumla ya shilingi milioni 32,000,000/- na shilingi milioni 38,000,000/- zimetolewa kwa vikundi 19 vya wanawake.

Alisema mkopo huo umetolewa kwa awamu ya pili, ambapo kwa awamu ya kwanza kipindi cha mwaka 2016/2017 Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ilitoa kiasi cha shilingi milioni 70,147,000/- kutoka mapato ya ndani kwa vikundi 35 vya wanawake na vijana.

Aidha, jumla ya 647,000/- zilitumika kwa ajili ya kuwajengea uwezo viongozi wa vikundi vilivyokopeshwa, ambapo vikundi 18 vya vijana na vikundi 17 vya wanawake vilinufaika.

Kwa upande wake Kaimu Ofisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Iringa, Eliah Kasanga alisema kuwa ofisi yake kwa kushirikiana na watendaji wa kata wameendelea kufanya ufautiaji kwa vikundi vilivyokopeshwa, na mpaka Januari, 2017 jumla ya 39,788,000/- zimerejeshwa na ufualiaji unaendelea.

Kasanga alisema  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imekuwa ikitekeleza agizo la serikali la kutenga asilimia kumi ya mapato ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake na vijana.

Alisema agizo hilo lilianza kutekelezwa kuanzia mwaka 2012 kwa kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake tu na kufikia mwaka 2013 mikopo hiyo ilianza kutolewa kwa vikundi vya vijana pia.

'''Kuanzia mwaka 2012/2013 mpaka 2016/2017 kiasi cha shilingi 175,100,000/- zimenufaisha walengwa 1,243 wa vikundi vya wanawake na vijanaalisema Kasanga'''

Nae Mratibu wa Mikopo ya Vijana Manispaa ya Iringa, Maria Sangana alisema mfuko huo umekuwa ukikabiriwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na vikundi kutorejesha fedha walizokopeshwa kwa wakati.

Sangana alisema kuwa hali hii imekuwa ikichelewesha utoaji wa mikopo kwa vikundi vingine na kuongeza kuwa baadhi ya vikundi kutotumia fedha kwa shughuli walizopanga wakati wa kuomba mkopo.

Alisema kuwa baadhi ya vikundi vinakabiliwa na mikopo mengine mingi toka taasisi zingine za fedha na kuongeza kuwa kuna upotoshaji unaendelea mitaani kuwa fedha inayotolewa na serikali ni msaada.


''Katika kukabiliana na changamoto hizo ofisi ya maendeleo ya jamii katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imeeandaa mfumo wa ufuatilaji wa marejesho ya fedha za mfuko huo, pamoja na kuendelea kutoa elimu ya stadi za kazi na ujasiliamali kwa kivundi vya ujasiliamali'''Alisema Sangana.

0 maoni:

Chapisha Maoni