Jumatatu, 27 Machi 2017

KAMATI YA BUNGE YA HESABU NA SERIKALI ZA MITAA[ LAAC ]YATOA AGIZO KWA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

Posted by Esta Malibiche on MARCH 27,2017 IN NEWS



Kamati ya Kudumu ya Bunge Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC)imewaagiza watendaji wa Manispaa ya Iringa kuhakikisha wanasimamia miradi ya Maendeleo ili iweze kukamilika kwa wakati na  kwa kiwango cha ubora unaotakiwa.
  

Kauli hiyo imetokea baada ya Kamati hiyo kutetembelea miradi mbalimbali iliyopo  Manispaa ya Iringa ukiwemo mradi wa maji, barabara na machinjio ya kisasa,ambapo mradi huo umechukua muda mrefu zaidi ya miaka kumi bila kukamilika,hali iliyoishangaza kamati hiyo na hatimae kutoa agizo kwa manispaa.

Akizungumza wakati wa majumuisho ya ziara ya siku moja ya kamati hiyo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Iringa Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Abdallah Chikota alitoa maelekezo kwa Manispaa  kusimamia miradi na kuhakikisha inatekelezwa kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa.


 Akizungumzia uboreshaji wa Miundombinu ya barabara alisema kuwa Manispaa ya Iringa imeelekeza nguvu kubwa katikati ya mji na kusahau barabara za pembezo ambazo zitasaidai kutoa huduma kwa wananchi.

 Chikota alisema kuwa barabara hizo hazina viwango vinavyotakiwa  pamoja na kukamilika ujenzi wake,ikiwemo alama za barabarani na vivuko vya watembelea kwa miguu,hali inayosababisha kutokuwa rafiki kwa mwananchi.

Kamati ya Kudumu ya Bunge za Hesabu za Serikali za Mitaa ilitembelea barabara za Mkimbizi- kihesa Sokoni-Chuo kikuu cha Iringa na Ngome na kukuta barabara hizo hazina vivuko ambavyo vinaweza kwa kuwarahisishia wananchi kufika kwa urahisa katika makazi yao.

Mradi wa ujenzi wa barabara unajumuisha vipande vitatu vya barabara za Mkimbizi TBA (1.10km), Kihesa Sokoni-University of Iringa (zamani Tumaini University (0.70km) na Ngome–Mwang’ingo (0.45km) uliyobuniwa ili kuinua kiwango cha barabara hizi kutoka changarawe hadi kiwango cha lami.



‘’’’Kuna tofauti kubwa kati ya wananchi waishio pembezoni na katikakti. Barabara za pembezoni mwa mji hazina kiwamgo vya ubora…,” alisema Chikota.

Awali kitoa taarifa kwa kamati hiyo, Mhandishi wa Ujenzi wa Manispaa ya Iringa, Mashaka Luhamba alisema kuwa mradi huo ulianza kutekeleza tarehe 1/11/2013 na uilikamilika tarehe 18/09/2014.Alisema kazi hiyo ilitekelezwa na Mkandarasi G’S Contractors kwa mkataba wa gharama ya 1,088,505,000/-.

Luhamba alisema kuwa kazi hiyo ililenga na pia kupunguza kero kwa wananchi wa eneo la mkimbizi ambalo halina barabara ya uhakika na lina wakazi wengi.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alisema amepokea maagizo hayo kutoka kamati ya kudumu ya bunge za hesabu za serikali za mitaa (LAAC)na kuahidi kuyafanya kazi mapendekezo hayo.

Wamoja alisema kuwa kupitia sekretarieti ya mkoa atahakikisha wanasimia utekelekezaji wa maagizoyote yalitotolewa na kamati hiyo kwa manispaa ya Iringa na kuhakikisha yanatekelezwa ipasavyo.

 Halmashauri ya Manispaa ilifanya matengenezo ya barabara hizi kwa kiwango cha lami kwa kutumia fedha za mfuko wa barabara (Road Fund) kwa bajeti ya mwaka 2013/2014 ambazo zilivuka mwaka.



 





 
 


 
 


 
 




 






 


0 maoni:

Chapisha Maoni