Alhamisi, 9 Machi 2017

WAKAZI MKOANI IRINGA WASHAURIWA KUNUNUA HISA



Posted by Esta Malibiche on MARCH 9,2017 IN NEWS


Na Esta Malibiche
Iringa.
Wakazi mkoani hapa wameshauriwa kujenga utamaduni wa kununua hisa kutoka katika makapuni mbalimbali ili kuwa  sehemu ya wanufaika wa faida zitokanazona biashara inayofanywa na makampumi hayo.
Akizungumza kwenye mkutano  ulioandaliwa na Kampuni  Chambe ya Wafanyabiashara wa Viwanda na Wakulima Pubalic Investment Campany (TCCIA PLC) mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Injiani Alois  Mwamanga alisema watu wengi waliopiga hatua kimaendeleo  duniani ni wale walionunua hisa katika kampuni mbalimbali.
Alisema hapoa nchini elimu ya watu juu ya umuhimu wa kununua hisa ni ndogo na ndioa sababu kampuni hiyo imepita katika mikoa mbalimbali ikiwamo Iringa kuhamasisha watu kununua hisa.
“Suala la kununua hisa kwa hapa nchini ni geni,watu wetu hawana utamaduni huo lakini ukweli ni kwamba hii ni fursa pekee ya mtanzania wa kawaaida kuwekeza kwenye uchumi”alisema Mwamanga na kuongeza:
“Hatua hii itawawezesha wananchi kupata gawio takribani kila mwaka nah ii itawezesha wananchi wengi kuondokana na umasikini  unaokabili taifa kwa sasa.
Alitolea mfano watalii wanaotka nchi z aulaya kuja kutembelea nchini kuwa wengi wao wamewekeza katika kununua hisa kwenye kampuni mbalimbali na hutumia fedha zitokanazo na gawio kufanya safari katika nchi mbalimbali.
Mwamanga alisema zipo faida za kudumu kwa mtu anayenunua hisa kwakuwa anapata fursa ya kupata gawio litokanalo na faida iliyopatikana kwenye kampuni hiyo kila mwaka jambo ambalo linaweza kuwafanya waaondokani na umasikini.
Alisesma lengo la kukutana na wafanyabiashara pamoja na wakazi wa mkoa wa Iringa ni kuwahamasisha ili kujenga utamaduni wa kununua hisa  zikiwamo hisa 112.5 milioni  zinazouzwa na Kampuni ya TCCIA PLC.
Kwa upande wake Judith Ndawi  ambaye alishiriki mkutano huo alisema ni muhimu wsatu kununua hisa ili kukabiliana na changamoto z auchumi wa sasa.
 “Mimi ninamfano mme wangu amewekeza kwenye Kampuni ya Bahaco lakini kila mmoja anapata mgao,tupo sisi na watoto wetu wane katika familia na wote tunapata mgao katika Akaunti zetu mimi nimefarijika sana ninawashauri wananchi wengine kununua hisa”alisema Ndawi.
Afisa Mtendaji wa TCCIA Mkoa wa Iringa James Sizya alisema mkutano huo  uliandaliwa na TCCIA PLC lengo likiwa kutoa elimu ya umuhimu wa wananchi kununua hisa katika kampuni hiyo na kampuni mbalimbali ili kuwa sehemu ya uwekezaji katika kampuni mbalimbali.
Aliwataka wananchi hao kujitokez akununua hisa hizo kwa kuwaa lengo la kampuni hiyo ni kuwajenga wananchi kiuchumi na kuwawezesha kumdu gharama za maisha ya sasa na baadae.

0 maoni:

Chapisha Maoni