Kwa Habari za kitaifa na kimataifa

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za michezo na burudani

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za afya

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za Kilimo

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za uchumi na biashara

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za elimu

Tembelea Kali ya habari

Jumatatu, 27 Machi 2017

KIWANDA CHA SARUJI MOSHI CHAFUNGWA KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA

Posted by Esta Malibiche on MARCH 27,2017 IN NEWS

UCHA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Rombo Bi. Agness Hokororo mara baada ya kuwasili wilayani hapo kwa ziara ya kikazi.
UCHA 1
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba alipotembelea kiwanda cha saruji cha Moshi. Kiwanda hicho kimefungiwa baada ya kutotekeleza maagizo waliyopewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). Katikati ni Mwakilishi wa Kiwanda hicho Bi. Sophia na kushoto ni Dkt. Menan Jangu kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Kanda ya Kaskazini.
UCHA 2
Mtambo wa kudhibiti vumbi katika kiwanda cha saruji cha Moshi ambao haufanyi kazi ipasavyo, kumekua na malalamiko kutoka kwa wananchi juu ya uchavuzi wa hewa ufanywao na kiwanda hicho. Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC Kanda ya Kaskazini ilitoa maelekezo ambayo hayakutekelezwa kikamilifu,  hivyo kiwanda hicho kimefungwa hii leo.
……………
Na Lulu Mussa,Moshi
Ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba hii leo ametembelea Mkoani Kilimanjaro katika Wilaya ya Rombo. Akiwa Wilayani hapo Waziri Makamba ametembelea Kiwanda cha Saruji cha Moshi kufuatia malalamiko ya wananchi juu ya uchafuzi wa hewa itokanayo na vumbi katika shughuli za uzalishaji.
Akitoa maelezo wa awali, Mkuu wa Wilaya ya Rombo Bi. Agness Hokororo amesema kuwa Kiwanda hicho kimeendesha shughuli za uzalishaji wa sementi kwa kutofuata sheria ya mazingira ya mwaka 2004 ikiwa ni pamoja na kutokuwa na mfumo mzuri wa kudhibiti uchafuzi wa vumbi kiwandani hapo.
kwa upande mwingine Dkt. Menan Jangu Mratibu wa Mazingira kutoka Baraza la Taifa la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Kanda ya Kaskazini amesema kuwa Ofisi yake awali ilitembelea kiwanda hicho na kutoa muongozo na taratibu zinazotokiwa kufuatwa kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004.
“Tuliwaelekeza kufanya yafuatayo, kujenga fensi kuzunguka eneo lote la kiwanda, kujenga “pevements” na kuweka mashine maalumu ya kuzuia vumbi kusambaa kwa wingi angani, vitu ambavyo havijafanyiwa kazi.” Alisisitiza Dkt. Jangu
Mwakilishi wa Kiwanda hicho raia wa China aliyefahamika kwa jina moja tu Bi. Sophia, amesema kuwa suala la kuzungusha uzio eneo lote litatekelezwa pindi hati miliki ya ardhi ya eneo hilo itakapopatikana.
Waziri Makamba aliagiza NEMC kukifunga kiwanda hicho mpaka mapendekezo yaliyotolewa na Baraza yatakapokamilika. “Kiwanda hiki kisitishe shughuli za uzalishaji mpaka pale vigezo vya Sheria ya Mazingira vitakapokamili”
Katika hatua nyingine Waziri Makamba ametembelea Ziwa Chala na kuwataka wadau wa mazingira kuongeza jitihada katika kulihifadhi  kwa kuwa ni muhimu kwa ikolojia na historia yake. ” Kina cha ziwa hili kinashuka kwa kasi kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi na sisi kama Serikali tutahakikisha tunawekeza nguvu zetu katika kunusuru kina cha ziwa hili kisiendelee kushuka” Alisisitiza Makamba.
Waziri Makamba ameahidi kuzungumza na Serikali ya Kenya ili kuwa na mikakati ya pamoja ya kuhifadhi ziwa hilo kwa kukuwa lipo pande zote za nchi hizi. Ziwa Chala ni chanzo kikubwa cha utalii na limetokana na mlipuko wa Volcano likiwa halitoi wala kuingiza maji kutoka vyanzo mbalimbali.
Waziri Makamba amemaliza ziara yake Mkoani Kilimanjaro na hii leo amewasili Mkoani Arusha.

PROF. MBARAWA: NEEMA YAJA WAFANYABIASHARA KANDA YA ZIWA

Posted by Esta Malibiche ON MARCH 27,2017 IN NEWS

JEMA
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati), akielekea kukagua Bandari ya Kemondo mkoani Kagera ili kujionea utendaji kazi wake.  Kulia ni Meneja wa Bandari Kanda ya Ziwa, Bw. Abel Moyo.
JEMA 1
Meneja wa Bandari Kanda ya Ziwa, Bw. Abel Moyo, akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (Wa pili kushoto), njia ya reli katika bandari ya Kemondo mkoani Kagera, ambayo itaruhusu mizigo itakayokuja kwenye mabehewa kwa njia ya meli iweze kupakuliwa na kupelekwa kuhifadhiwa kwenye maghala.
JEMA 2
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akikagua sehemu ya maegesho ya meli katika Bandari ya Kemondo, mkoani Kagera. Bandari hiyo ina upana wa mita 100.
JEMA 3
Muonekano wa gati ya meli katika Bandari ya Kemondo, mkoani Kagera.
JEMA 4
Kaimu Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), mkoani Kagera Eng. Zephrine Bahyona, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa nne kulia), alipokuwa akikagua Kivuko cha Kyanyabasa kinachotoa huduma katika mto Kyanyabasa, mkoani Kagera.
JEMA 5
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa Kaimu Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), mkoani Kagera Eng. Zephrine Bahyona, alipotembelea na kukagua kivuko cha Kyanyabasa kinachotoa huduma katika mto Kyanyabasa, mkoani Kagera.
JEMA 6
Muonekeano wa kivuko cha Kyanyabasa kinachotoa huduma katika mto Kyanyabasa, mkoani Kagera. Kivuko hicho kina uwezo wa kubeba watu sitini au magari mawili madogo kwa wakati mmoja.
………………..
Imeelezwa kuwa kukamilika kwa ukarabati wa meli ya MV Umoja kutarudisha huduma ya usafirishaji wa mizigo katika kanda ya ziwa kupitia bandari ya Kemondo  iliyopo mkoani Kagera.
Kauli  hiyo imetolewa na  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, wakati akikagua Bandari hiyo kuangalia maendeleo yake, na kuitaka Mamlaka ya Bandari Nchini (TPA), Shirika la Reli Nchini (TRL), na Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL),  kuanza kuandaa Mfumo mmoja wa kutoa Stakabadhi ili kuwarahisishia wateja wake huduma za usafirishaji wa mizigo.
Aidha, Waziri Mbarawa ameitaka TRL kukarabati njia za reli bandarini hapo haraka iwezekanavyo ili kuruhusu mizigo itakayokuja ikiwa kwenye mabehewa kwa njia ya meli iweze kupakuliwa pindi Meli hiyo itaposhusha.
“Serikali imefanya ukarabati wa meli ya MV Umoja ambayo itabeba mizigo ikiwa kwenye mabehewa na reli hii inahitaji ukarabati mapema ipasavyo nawaagiza TRL kufanya ukarabati wa reli ili kusiwepo usumbufu wowote wakati wa kushusha na kupakia mizigo hiyo” , amesema Profesa Mbarawa.
Ameiagiza Mamlaka hiyo kuanza kutafuta tena wateja ambao kwa muda mrefu walikuwa wamepotea kutokana na  bandari hiyo kusuasua kutoa huduma zake kwa muda mrefu.
Kwa upande wake Meneja wa TPA Kanda ya Ziwa Bw. Abel Moyo, amemuahidi Waziri huyo  kutekeleza agizo lake kwa kushirikiana na TRL pamoja na MSCL na kuwahakikishia wafanyabiashara wa kanda ya ziwa  kuwa na matumaini mpya ya kupata usafiri bora na wa uhakika.
Katika hatua nyengine, Waziri Mbarawa ametembelea na kukagua Kivuko cha Kyanyabasa kinachotoa huduma katika mto Kyanyabasa na kumtaka Kaimu Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) mkoani humo, Eng. Zephrine Bahyona,  kutoa huduma bora sambamba na kukusanya mapato ili kuweza kutatua changamoto ndogondogo zinazowakabili.
Naye, Kaimu Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) mkoani humo Eng. Zephrine Bahyona, amezitaja baadhi ya changamoto zinazoathiri utendaji mzuri wa kivuko hicho kuwa ni kukatika kwa magugu maji na hivyo kupelekea kusombwa kwa kivuko.
Waziri Profesa Mbarawa pia amekagua barabara ya Uyovu- Bwanga yenye urefu wa kilometa 45 mkoani Geita na kuridhishwa na kasi ya Mkandarasi wa ujenzi wa barabara hiyo ambapo ujenzi wake kwa sasa umefika asilimia 56.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WIzara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

BALOZI WA MOROCCO NCHINI TANZANIA AKUTANA NA WAZIRI WA ARDHI KUHUSU MASUALA YA ARDHI

Posted bu Esta Malibiche on MARCH 27,2017 IN NEWS

ORO
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa William Lukuvi akiwa na Balozi wa Morocco Nchini Tanzania Mhe. Abdelilah Benryane wakati alipo mtembelea ofisini kwake.
ORO 1
Balozi wa Morocco Nchini Tanzania Mhe. Abdelilah Benryane akimueleza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa William Lukuvi jinsi Nchi yake ilivyofanikiwa katika kukabiliana na makazi holela kwa kiasi kikubwa.

KAMATI YA BUNGE YA HESABU NA SERIKALI ZA MITAA[ LAAC ]YATOA AGIZO KWA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

Posted by Esta Malibiche on MARCH 27,2017 IN NEWS



Kamati ya Kudumu ya Bunge Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC)imewaagiza watendaji wa Manispaa ya Iringa kuhakikisha wanasimamia miradi ya Maendeleo ili iweze kukamilika kwa wakati na  kwa kiwango cha ubora unaotakiwa.
  

Kauli hiyo imetokea baada ya Kamati hiyo kutetembelea miradi mbalimbali iliyopo  Manispaa ya Iringa ukiwemo mradi wa maji, barabara na machinjio ya kisasa,ambapo mradi huo umechukua muda mrefu zaidi ya miaka kumi bila kukamilika,hali iliyoishangaza kamati hiyo na hatimae kutoa agizo kwa manispaa.

Akizungumza wakati wa majumuisho ya ziara ya siku moja ya kamati hiyo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Iringa Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Abdallah Chikota alitoa maelekezo kwa Manispaa  kusimamia miradi na kuhakikisha inatekelezwa kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa.


 Akizungumzia uboreshaji wa Miundombinu ya barabara alisema kuwa Manispaa ya Iringa imeelekeza nguvu kubwa katikati ya mji na kusahau barabara za pembezo ambazo zitasaidai kutoa huduma kwa wananchi.

 Chikota alisema kuwa barabara hizo hazina viwango vinavyotakiwa  pamoja na kukamilika ujenzi wake,ikiwemo alama za barabarani na vivuko vya watembelea kwa miguu,hali inayosababisha kutokuwa rafiki kwa mwananchi.

Kamati ya Kudumu ya Bunge za Hesabu za Serikali za Mitaa ilitembelea barabara za Mkimbizi- kihesa Sokoni-Chuo kikuu cha Iringa na Ngome na kukuta barabara hizo hazina vivuko ambavyo vinaweza kwa kuwarahisishia wananchi kufika kwa urahisa katika makazi yao.

Mradi wa ujenzi wa barabara unajumuisha vipande vitatu vya barabara za Mkimbizi TBA (1.10km), Kihesa Sokoni-University of Iringa (zamani Tumaini University (0.70km) na Ngome–Mwang’ingo (0.45km) uliyobuniwa ili kuinua kiwango cha barabara hizi kutoka changarawe hadi kiwango cha lami.



‘’’’Kuna tofauti kubwa kati ya wananchi waishio pembezoni na katikakti. Barabara za pembezoni mwa mji hazina kiwamgo vya ubora…,” alisema Chikota.

Awali kitoa taarifa kwa kamati hiyo, Mhandishi wa Ujenzi wa Manispaa ya Iringa, Mashaka Luhamba alisema kuwa mradi huo ulianza kutekeleza tarehe 1/11/2013 na uilikamilika tarehe 18/09/2014.Alisema kazi hiyo ilitekelezwa na Mkandarasi G’S Contractors kwa mkataba wa gharama ya 1,088,505,000/-.

Luhamba alisema kuwa kazi hiyo ililenga na pia kupunguza kero kwa wananchi wa eneo la mkimbizi ambalo halina barabara ya uhakika na lina wakazi wengi.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alisema amepokea maagizo hayo kutoka kamati ya kudumu ya bunge za hesabu za serikali za mitaa (LAAC)na kuahidi kuyafanya kazi mapendekezo hayo.

Wamoja alisema kuwa kupitia sekretarieti ya mkoa atahakikisha wanasimia utekelekezaji wa maagizoyote yalitotolewa na kamati hiyo kwa manispaa ya Iringa na kuhakikisha yanatekelezwa ipasavyo.

 Halmashauri ya Manispaa ilifanya matengenezo ya barabara hizi kwa kiwango cha lami kwa kutumia fedha za mfuko wa barabara (Road Fund) kwa bajeti ya mwaka 2013/2014 ambazo zilivuka mwaka.



 





 
 


 
 


 
 




 






 


WAHUDUMA 80 KATIKA SEKTA YA UTALII WAPATA MAFUNZO IRINGA

Posted by Esta Malibiche on MARCH 27,2017 IN NEWS



MKUU wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amewataka watoa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii kanda ya kusini kuboresha huduma zao ili kukidhi haja soko la utalii katika ukanda huu.

Mafunzo hayo yanayotolewa na wizara ya Maliasili na utalii kwa kushirikiana na Mradi wa Kuboresha Mtandao wa Maeneo Yaliyohifadhiwa Kusini mwa Tanzania (SPANEST), yanafanyika kwa muda wa siku tatu Iringa.


Aliyasema hayo jana kwenye mafunzo ya siku tatu kwa watoa huduma wa sekta ya ukarimu na utalii,na kuhudhuriwa na  watoa huduma zaidi ya 80 wanaofanya biashara inayohudumia watalii mkoani Iringa.


Masenza alisema kuwa ili kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi za taifa za kusini watoa huduma kwa kushirikiana na sekta binafsi hawanabudi kuinua viwango vya utowaji wa huduma.

Alisema kuwa serikali ipo katika machakato wa kuboresha miundombinu za barabara na viwanja vya ndege ili kurahisha watalii kufika katika hifadhi pamoja na vivutio vilivyopo katka ukanda wa kusini.

‘’Takwimu za mwaka 2015 zinaonesha kuwa watalii wengi zaidi walitembelea mbuga za kanda za kaskazini kuliko kanda ya kusini, kwa hiyo mafunzo hayo yatakuwa chachu ya kuboresha utoaji wa huduma katika kanda ya kusini.Hivyo basi Wizara ya Maliasili na Utalii ipo katika mchakato wa kutunga kanuni zitakazowazuia wafanyakazi wa hoteli wasio na vyeti vinavyotambulika na serikali kutoa huduma katika sekta ya utalii’’Alisema Masenza

Alisema kuwa kanuni hiyo ambayo msingi wake unalenga kuendeleza na kuboresha huduma katika ya sekta hiyo, utahusisha pia kuvibana vyuo vya hoteli na utalii ili vitoe mafunzo yanayokidhi viwango kwa manufaa ya Taifa.

“Baada ya kutungwa na kuanza kutumika kwa kanuni hizo, waajiri katika sekta hiyo watalazimika kuwaajiri wafanyakazi wenye sifa ambao wamesajiliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii,” alisema Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utalii, alisema Masenza.


 Kwa upande wake Mratibu wa SPANEST, Godwell Ole Meing’ataki alisema changamoto hizo zimesababisha huduma duni katika maeneo ya mapokezi, chakula, vinywaji na malazi, na hivyo kuleta malalamiko makubwa sana kwa wageni.


Meing’ataki alisema SPANEST inamatarajio makubwa mara mafunzo yatakapomalizika washiriki wataweza kutambua wajibu wao ili wageni waingiapo waweze kuwahudumiwa vizuri.

“Sekta ya utalii ina changamoto nyingi, lakini eneo hili la huduma ni muhimu kwasababu linaweza kusaidia kumrudisha mgeni tena na tena na kumfanya awe balozi kwa watu wengine,” alisema Meing’ataki .

Aliongeza kuwa katika sekta ya utalii haitoshi  kuwa na hoteli kubwa tu kama itakuwa haina huduma bora kwa wageni wake.
 Awali,Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Fikira Kissimba alisema licha ya ukanda wa nyanda za juu kusini kuwa na vivutio vingi vya utalii, idadi ya watalii wanaovitembelea ni ndogo na moja ya sababu yake ni uduni wa huduma katika sekta hiyo ya utalii.


Kissimba aliishukuru wizara ya maliasili na utalii na SPANEST kwa kutoa mafunzo hayo, Kissimba alisema yatakuwa chachu katika kukuza na kuendeleza utalii kusini mwa Tanzania kwa kutoa huduma bora kwa watalii.

Aliwataka wahudumu katika sekta hiyo waache tabia ya uvivu, kufanyakazi kwa mazoea na wawe wepesi kujifunza ili kuboresha huduma zao.

HAMLASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA YAWAKABIDHI VIJANA NA WANAWAKE HUNDI YENYE THAMANI YA MILL.70,000,000

Posted by Esta Malibiche on MARCH 27,2017 IN NEWS


HALMASHAURI ya Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa imetoa mkopo kwa vikundi 35 vya wanawake na vijana ikiwa ni utekeleza wa agizo la serikali la kutenga asilimia kumi (10%) ya mapato ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vijana na wanawake.

Akikabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 70,000,000/- kwa vikundi hivyo katika awamu ya pili ya kipindi cha mwaka 2016/2017, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa, Alex Kimbe amewataka kinamama na vijana kutumia fedha hizo kwa shughuli zilizokusudiwa ili ziweze kuleta manufaa na kuwatoa katika lindi la umasikini.

Kimbe alisema kuwa jumla ya vikundi 35 toka katika kata zote 18 za Manispaa ya Iringa vimepokea mikopo, ambapo vikundi 16 vya vijana vimepokea jumla ya shilingi milioni 32,000,000/- na shilingi milioni 38,000,000/- zimetolewa kwa vikundi 19 vya wanawake.

Alisema mkopo huo umetolewa kwa awamu ya pili, ambapo kwa awamu ya kwanza kipindi cha mwaka 2016/2017 Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ilitoa kiasi cha shilingi milioni 70,147,000/- kutoka mapato ya ndani kwa vikundi 35 vya wanawake na vijana.

Aidha, jumla ya 647,000/- zilitumika kwa ajili ya kuwajengea uwezo viongozi wa vikundi vilivyokopeshwa, ambapo vikundi 18 vya vijana na vikundi 17 vya wanawake vilinufaika.

Kwa upande wake Kaimu Ofisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Iringa, Eliah Kasanga alisema kuwa ofisi yake kwa kushirikiana na watendaji wa kata wameendelea kufanya ufautiaji kwa vikundi vilivyokopeshwa, na mpaka Januari, 2017 jumla ya 39,788,000/- zimerejeshwa na ufualiaji unaendelea.

Kasanga alisema  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imekuwa ikitekeleza agizo la serikali la kutenga asilimia kumi ya mapato ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake na vijana.

Alisema agizo hilo lilianza kutekelezwa kuanzia mwaka 2012 kwa kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake tu na kufikia mwaka 2013 mikopo hiyo ilianza kutolewa kwa vikundi vya vijana pia.

'''Kuanzia mwaka 2012/2013 mpaka 2016/2017 kiasi cha shilingi 175,100,000/- zimenufaisha walengwa 1,243 wa vikundi vya wanawake na vijanaalisema Kasanga'''

Nae Mratibu wa Mikopo ya Vijana Manispaa ya Iringa, Maria Sangana alisema mfuko huo umekuwa ukikabiriwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na vikundi kutorejesha fedha walizokopeshwa kwa wakati.

Sangana alisema kuwa hali hii imekuwa ikichelewesha utoaji wa mikopo kwa vikundi vingine na kuongeza kuwa baadhi ya vikundi kutotumia fedha kwa shughuli walizopanga wakati wa kuomba mkopo.

Alisema kuwa baadhi ya vikundi vinakabiliwa na mikopo mengine mingi toka taasisi zingine za fedha na kuongeza kuwa kuna upotoshaji unaendelea mitaani kuwa fedha inayotolewa na serikali ni msaada.


''Katika kukabiliana na changamoto hizo ofisi ya maendeleo ya jamii katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imeeandaa mfumo wa ufuatilaji wa marejesho ya fedha za mfuko huo, pamoja na kuendelea kutoa elimu ya stadi za kazi na ujasiliamali kwa kivundi vya ujasiliamali'''Alisema Sangana.

PPF YAKABIDHI VIFAA TIBA KATIKA KITUO CHA AFYA LONGIDO

Posted by Esta Malibiche on MARCH 27,2017 IN NEWS

TPP
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu),
Mhe. Jenista Mhagama,(watatu kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho
Gambo,(wanne kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William
Erio, (watano kushoto), Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI (anayeshughulikia Afya),
Dkt. Zainabu Chaula,(kulia), Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mhe. Daniel Chongolo,
(wapili kushoto), na viongozi wengine, wakiangalia kitanda cha kujifungulia
wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba vilivyotolewa na PPF.
 Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu),
Mhe. Jenista Mhagama,(watatu kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw. William
Erio, (wapili kushoto), Viongozi wa Mkoa wa Arusha na Wilaya ya Longido,
wakitembelea wodi ya wagonjwa ya Kituo cha Afya Longido, ambapo ni moja kati ya
vituo vilivyonufaika na msaada huo wa vifaa tiba kama sehemu ya mchango  wa PPF kwenye Jamii.
.