Kwa Habari za kitaifa na kimataifa

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za michezo na burudani

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za afya

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za Kilimo

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za uchumi na biashara

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za elimu

Tembelea Kali ya habari

Jumatatu, 27 Februari 2017

RC MRISHO GAMBO ATEMBELEA NYUMBANI KWA HAYATI EDWARD SOKOINE

Posted by Esta Malibiche on FEB 27,2017 IN NEWS


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo,Akisalimiana na Mjane wa Hayati Sokoine.
Kutoka Kulia ni Diwani wa Monduli juu akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli na pia ni Diwani wa Monduli Mjini Mh:Issack Joseph,akisalimiana na Mjane wa Hayati Sokoine .
Mh: Gambo akiwa ameambatana na Mjane wa Sokoine Pamoja na watumishi mbalimbali wa Serikali,Wakitoa Heshima kwenye kaburi la Hayati Sokoine.  
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mh: Mrisho Gambo akipanda mti wa kumbukumbu nyumbani kwa Hayati Sokoine.Picha na Msumbanews.com

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo wikiendi hii alipata nafasi ya kutembelea nyumbani kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani Hayati Edward Moringe Sokoine huko Monduli juu Wilayani Monduli. 

Mh.Gambo alipata wasaaa wa kuzungumza na wajane wa kiongozi huyo mkubwa wa Kitaifa aliyefariki kwa ajali ya gari mwaka 1984 eneo la Dumila huko Mkoani Morogoro, Mkuu wa mkoa alipata wasaa wakuzungumza na familia hiyo pamoja na wakazi majirani wanaozunguka familia hiyo na kusema maneno machache ambapo Alisema 

"Kutembelea maeneo haya ambapo zipo kumbukumbu za mashujaa wetu waliolipigania Taifa letu kwa uzalendo mkuu, inatusaidia sisi viongozi vijana kuzirudia hadhiri zetu za uongozi ili tuweze kuwatumikia wananchi wanyonge kwa Uadilifu na uwajibikaji,ili kuacha alama katika nafasi tulizopewa na kuwatumikia wananchi kama walivyofanya wazee wetu hawa."

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO DKT.ASHATU KIJAJI AFUNGUA TAWI JIPYA LA FIRST NATIONAL BANK JIJINI ARUSHA


Posted by Esta Malibiche on FEB 27,2017 
Afisa Mtendaji Mkuu wa First National Bank, Dave Aitken akiongea na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji wakati wa uzinduzi wa tawi la benki hiyo jijini Arusha mwishoni mwa wiki. 

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji akikata utepe kuzindua rasmi tawi la benki ya FNB Tanzania la Arusha huku akiambatana na Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqqaro (wa kwanza kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa FNB, Dave Aitken(wa pili kushoto) na Meya wa Jiji la Arusha, Mh. Calist Bukhai (kulia). 
Meneja wa Tawi la FNB Arusha, Genevieve Massawe akimueleza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dr. Ashatu Kijaji jinsi mashine ya kisasa ya kuweka fedha (cash deposit) na kutoa fedha. Mashine hiyo ya kisasa inamuwezesha mtumiaji kuweka fedha zake benki muda wa masaa 24 imewekwa kwenye tawi hilo jipya ili kuwawezesha wananchi kuweka akiba fedha zao muda wowote ule. 
Mshauri wa Huduma kwa Wateja na Mauzo wa FNB Tawi la Arusha, Cecyline Ayo akimueleza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo wakati wa uziduzi wa FNB Tawi la Arusha mwishoni mwa wiki. 
Afisa Mtendaji Mkuu wa First National Bank, Dave Aitken akimrekebishia kipaza sati Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji wakati wa uzinduzi rasmi wa tawi la FNB Tanzania la Arusha mwishoni mwa wiki. 

-- First National Bank (FNB) Tanzania imeendelea kupanua wigo wake kitaifa kwa kufungua tawi jipya eneo la PPF Plaza jijini Arusha kwa lengo la kuhudumia ongezeko la idadi ya wateja katika mkoa huo.

 Akizungumza wakati wa ufunguzi, Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Dave Aitken alisema uzinduzi wa tawi la FNB Arusha umelenga kukidhi ongezeko kubwa la wateja na mahitaji ya huduma za kibenki na kifedha katika kanda ya kaskazini. 

“ Uzinduzi wa tawi la Arusha ni sehemu ya mkakati wa uwekezaji endelevu uliolenga kuhakikisha maeneo mengi ya nchi yanapata huduma bora za kifedha. Pia ni kwa maslahi ya ukuaji wa haraka wa mkoa wa Arusha ambao una mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa Tanzania” Aitken alisema tawi la Arusha ni la kumi miongoni mwa mtandao wa matawi ya FNB Tanzania ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa kupanua mitandao ya matawi kwa kusudi la kuyafikia maeneo mengi ya nchini.

 “First National Bank (FNB), daima tunafikiria njia ambazo zinaweza kutoa huduma za kibenki kwa urahisi kwa wateja wetu. Tawi letu la Arusha litasaidia kuwapatia huduma zote za kibenki wananchi wa mkoa wa Arusha na wanaoishi maeneo jirani kwani maeneo haya yote yamedhiirika kuwa na biashara mbalimbali zinazokua kwa kasi,” alisema Aitken. 

Akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi rasmi wa tawi hilo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji alisema mkoa wa Arusha una uwezo mkubwa wa kiuchumi na ukuaji katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kudhihirisha kuwa mji unakuwa kwa kasi. 

“Tunakaribisha uwepo wa FNB Tanzania Arusha na tunatazamia kuwasaidia kuimarisha huduma zenu hapa na mikoa mengine,” Alisema Naibu Waziri. Alisema pamoja na utajiri mkubwa wa maliasili na utalii, mkoa wa Arusha umechangia sana katika kukuza uchumi wa Tanzania kupitia sekta nyingine za uzalishaji mali na biashara. 

“Arusha ina fursa na hazina kubwa ya rasilimali jambo ambalo limechangia ukuaji wa haraka wa biashara katika sekta zote muhimu za kiuchumi. Ni matumaini yetu uwepo wa FNB katika mji huu utachangia katika kuleta maendeleo ya biashara kupitia ubunifu wa huduma za kibenki,” Kijaji alisema. 

Vile vile Kijaji ameitaka sekta ya fedha nchini zimetakiwa kutoa mikopo inayosaidia wananchi kukuza mitaji yao ambayo kwa sehemu kubwa itawawezesha katika uzalishaji mali na kuongeza pato lao na nchi kwa ujumla. Amesema kuwa serikali haiwezi kufanikiwa kutekeleza sera na mipango yake kwa ufanisi bila kuwepo sekta binafsi hususani sekta ya fedha hivyo kama serikali inathamini sana mchango wa benki hiyo ya FNB ambayo kwa kiasi kikubwa itasaidia wananchi wa Arusha. 

Tawi la Arusha lililopo jengo la PPF Plaza linakuja na bidhaa na huduma mbalimbali zilizobuniwa mahususi kwa ajili ya kuwaongezea tija wateja wa kawaida na wafanyabiashara katika eneo hili la kanda ya kaskazini.

Jumapili, 26 Februari 2017

MATUKIO KATIKA PICHA ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU YA KUPEWA UPADRE SHEMASI RAYMOND SANGU KATIKA PAROKIA YA NJIRO JIMBO LA ARUSHA

Posted by Esta Malibiche on FEB 27,2017 IN NEWS

Mhashamu baba askofu mkuu wa jimbo kuu katoliki la Arusha Josephat Lebulu akitoa daraja takatifu la upadre  kwa  Shemasi Raymond Sangu,iliyofanyika  Parokia ya Njiro, jimbo katoliki la Arusha
 Mhashamu baba askofu mkuu wa jimbo kuu katoliki la Arusha Josephat Lebulu akitoa daraja takatifu la upadre  kwa  Shemasi Raymond Sangu,iliyofanyika  Parokia ya Njiro, jimbo katoliki la Arusha

 Mhashamu baba askofu mkuu wa jimbo kuu katoliki la Arusha Josephat Lebulu akitoa daraja takatifu la upadre  kwa  Shemasi Raymond Sangu,iliyofanyika  Parokia ya Njiro, jimbo katoliki la Arusha
 Shemasi Raymond Sangu akiwa amelala kifudifudi
Shemasi Raymond Sangu akiwa amelala kifudifudi

   Mhasham baba askofu mkuu wa jimbo kuu katoliki la Arusha Josephat Lebulu akitoa homilia yake [maubili]katika adhimisho la misa takatifu ya   upadre  wa  Shemasi Raymond Sangu,iliyofanyika  Parokia ya Njiro, jimbo katoliki la Arusha.
Ibada ya misa takatifu ikiendelea
  Waumini wakishiriki ibada ya misa takatifu ya upadre ya shemasi Raymond Sangu,iliyofanyika  Parokia ya Njiro, jimbo katoliki la Arusha.
 Waumini wakishiriki ibada ya misa takatifu ya upadre ya shemasi Raymond Sangu,iliyofanyika  Parokia ya Njiro, jimbo katoliki la Arusha.
 Watoto wa utoto mtakatifi[kipapa] wakishiriki ibada ya misa takatifu ya upadre ya shemasi Raymond Sangu,iliyofanyika  Parokia ya Njiro, jimbo katoliki la Arusha




MAGAZETI YA LEO FEBRUARY 27,2017

Posted by Esta Malibiche on FEB 27,2017 IN NEWS