Jumanne, 23 Januari 2018

KHERI JAMES ATOA AGIZO KWA HALMASHAURI MKOANI IRINGA KUWATENGEA ENEO RASMI VIJANA KABLA HAWAJAWAFUKUZA KATIKA MAENEO YASIYO RASMI.

Posted by Esta Malibiche On JAN 24,2018  IN SIASA



Mwenyekiti wa Uvccm Taifa Keri James akizungumza  na  wanajumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Chama na jumuiya zake  katika kikao kilichofanyika Manispaa ya Iringa katika ukumbi wa Hall Faer  
Na Esta Malibiche
Iringa.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM Taifa Kheri James amezitaka Halmashauri za Mkoa wa Iringa kuhakikisha zinatenga eneo maalum  na rafiki kwa ajili ya vijana wajasiliamali kabla hawajawafukuza katika maeneo yasiyo rasmi wanayofanyia kazi.

Agizo hilo amelitoa  jana wakati akizungumza na umoja wa vijana CCM Mkoa wa Iringa,wanachama  wa Chama cha Mapinduzi na jumuiya  zake,ambapo lisema kuwa  ni jambo la kusikitisha kuona vijana wanaondolewa  tena kwa kupigwa katika maeneo wanayofanyia kazi zao pasipo kuambiwa wanatakiwa waende wapi,hivyo kila "Halmashauri ihakikishe imetenga eneo kwa ajili ya vijana na kama  eneo halijatengwa basi marufuku kuwafukuza nawawaache waendelee na biashara zao.

" Viongozi wa Chama ,Jumuiya na Serikali kwa ujumla  hakikisheni mnawatengea vijana eneo lao rasmi la kufanyia kazi kabla hamjawafukuza katika maeneo  yasiyo rasmi wanayofanyia kazi zao kwa ajiki yq kujiingizia kipato   hivyo kuongeza pato la Taifa na kukuza uchumi."Alisema Kheri na kuongeza kuwa
.Si sahihi na haikubaliki kumwambia kijana   atoke katika eneo analofanyia biashara  kabla  haujamtengea  eneo rafiki haitakubalika.Kama mnataka kuwatoa basi  hakikisheni mmewapa eneo  lao la kufanyia   kazi zao kinyume na hapo ni matumizi mabaya ya madaraka."Alisema Kheri"

Aidha  aliwataka viongozi wa Uvccm  ngazi zote   kutenga muda maalum kwa ajili yakupokea maoni  kutoka kwa vijana na wanachama ili waweze kuyatatua kwa wakati. 
"Nendeni mkawafikie wanachama na kupokea maoni yao  na siyo kukaa ofisini tu, lazima tujue kuwa Uvccm ni  sauti inayosikikika kwasababu kuna vijana wana mawazo na maoni juu ya Serikali yao lakini hawana pa kusemea.Wafikieni,bodaboda,vijana wajasiliamali,Mama nitilie,vijana wa Vijiweni na wengineo"" Alisiaitiza Kheri

 Hata hivyo aliwasihi   viongozi  wa Uvccm katika ngazi zote  kutoa ushirikiano  kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi  ikiwa nipamoja na kutambua mipaka yao ya kufanyia kazi  na kuheshimiana  iili kuepuka migogoro isiyo ya lazima na inayoweza kuhepukika.


Kwa upande wake katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Mgala alisema hakuna kiongozi ndani ya Chama na  na Serikali kaa asiyepitia na kupikwa na Uvccm,hivyo ni jukumu la Vijana kuienzi kwa vitendo na si kwa mamneo tu.
"Uvccm ni tanuru la kuoka viongozi, mbalimbali ndani ya Chama na Serikali yake ambalo limewekewa  namna ya kuongoza  ukiwa kiongozi utokana na mafundisho  tunayoyapata  Uvccm .


Nae Mnec wa Mkoa wa Iringa Salim Asas akizungumza  aliwataka Vijana kuchangamkia fursa zinazotokana na Chama cha Mapinduzi CCM.
"Fursa  za Vijana  zipo ndani ya CCM sababu ndiyo inayotawala  na ndiyo yenye Serikali.Hakuna kijana atakaepata fursa nje ya CCM ,hivyo tuache ushabiki usio na  tija kwa jamii na Taifa kwa ujumla"" 
Alisema Asasas na kuongeza  kuwa 
"Tuwapuuze watu wanaotugawa vijana nawatanzania kwa ujumla,tusiwashabikie wale wote wasiopenda maendeleo ya Nchi yetu ambao kutwa kuchwa wanaitukana Serikali  na viongozi wa Chama,watu kama hawa  ni wa kupuuzwa"" Alisema Asas
Ninawaomba tumuombee Mh.Rais wetu kipenzi cha watanzania,Dakta John Magufuli,tumuunge mkono kwa kazi kubwa anayoifanya ya kutetea mali za watanzania ili tuaweze kunufaika nazo.

Kenani Kihongosi ni Mwenyekiti wa Jumuiyabya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,akizungumza alisema,Vijana ni chachu ya  Chama cha Mapinduzi,hivyo wanatakiwa kuisaidia CCM   nanSerikali yake ili iendelee  kutawala.

"Tuisemee vizuri Serikali inayoongozwa na Chama cha Mapinduzi kwa yote yanayofanywa, tuwe mstari wa mbele kuyatangaza kwa wananchi ili wajue nini kinatekelezwa na Irani ya chama cha Mapinduzi.
Aidha alisisitiza wananchi wamuunge mkono  Mwenyekiti  wa Chama cha Mapinduzi Taifa,Rais Dakta John Magufuli  kwa kazi kubwa anayoifanya  kwa maslai mapana ya Taifa.




Mwenyekiti wa Uvccm Taifa Keri James akizungumza  na  wanajumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Chama na jumuiya zake  katika kikao kilichofanyika Manispaa ya Iringa katika ukumbi wa Hall Faer  
Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Mgala akizungumza.


 Kada wa Chama cha Mapinduzi CCMambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa Asia Abdalah akizungumza.


Mwenyekiti  wa Uvccm Taifa Kheri James akionyesha hati maalum ya pongezi kwa kazi nzuri anayoifanya katika jumuiya hiyo toka alipoingingia madarakani iliyotolewa na Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Iringa.


Mioni mwa wqnachama  wapya wqliorejesha kadi za Chadema na kujiunga na Chama cha Mmapinduzi CCM.
Mwanachama Mpya miongoni mwa 448 waliojiunga na Chama cha MapinduI CCM akipokea kadi tayari kwa kiapo.
Wanachama wapya 448  waliojiunga na Chama cha Mapinduzi CCM,wakila kiapo mara baada ya kupokea kadi  na wengine kurejesha kadi za Chadema.



  Mwenyekiti wa uvccm Taifa  alikutana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza na kufanya mazungumzo Ofisini kwake,ambapo Mkuu wa Mkoa aliipongeza Jumuiya ya Umoja wa Vijana CCM kwakuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya awamu  ya tano chini ya uongozi wake Rais John Magufuli kwa kuyasemea mazuri yote yanayofanywa na Serikali.
Masenza alimpongeza Mwenyekiti wa Uvccm Taifa Kheri James kwa  kazi nzuri anayoifanya toka aingie madarakani na kuahidi kutoa ushirikiano wa dhati kwa umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa.



Mwenyekiti wa Uvccm Taifa Kheri Jemes alitembelea na kukagua chuo cha  Mafunzo ya makada Ihemi n kuzungumza na watumishi wa chuo hicho.

Katika mazungumzo yao alisema Chama cha Mapinduzi kitaendelea kutimiza ndoto za wazee ambao ni  Asisi wa Chama  kwa kuifanya Ihemi kuwa kimbilio la vijana kimafunzo, Taaluma na Uchumi wa Jumuiya.
Mwenyekiti waa Uvccm Taifa Kheri Jemes alitembelea na kukagua chuo cha  Mafunzo ya makada Ihemi na  kuzungumza na watumishi wa chuo hicho.

Katika mazungumzo yao alisema Chama cha Mapinduzi kitaendelea kutimiza ndoto za wazee wa Chama  kwa kuifanya Ihemi kuwa kimbilio la vijana kimafunzo, Taaluma na Uchumimna wa Jumuiya.
Mwenyekiti waa Uvccm Taifa Kheri Jemes alitembelea na kukagua chuo cha  Mafunzo ya makada Ihemi kuzungumza na watumishi wa chuo hicho.
Katika mazungumzo yao alisema Chama cha Mapinduzi kitaendelea kutimiza ndoto za wazee  wa Chama  kwa kuifanya Ihemi kuwa kimbilio la vijana kimafunzo, Taaluma na Uchumimna wa Jumuiya.






0 maoni:

Chapisha Maoni