Jumatatu, 22 Januari 2018

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA KHERI JAMES AWAFUNDA WASOMI

libicheon JAN 22,2018 IN SIASA

Mwenyekiti wa Uvccm Taifa Kheri James akizungumza   na   Uvccm wanaosoma katika vyuo mbalimbali mkoani Iringa jana.



Na Esta Malibiche,
Iringa.
Mwenyekiti wa Uvccm Taifa Kheri James amewataka vijana wasomi Nchini kutumia Elimu waliyonayo kuisaidia Serikali    katika mambo mbalimbali , siyo kusubiri yaharibike ndipo waanze koukikosoa katika Mitandao ya kijamii.

Kauli hiyo ameitoa  jana wakati akizungumza  katika Mkutano maaluma wa Idara ya Vyuo na vyuo vikuu Mkoani Iringa, aliwataka wasomi kutumia Elimu yao kuleta Maendeleo Nchini.

 "" Wasomi tunatakiwa tuwe chachu ya maendeleo kwa kulisaidia Taifa letu.Tusisubiri mambo  yaharibike ndipo tuanze kukosoa na kulalamika,bali tushirikiane na Serikali kuhamasisha maendeleo Nchini kwa Maslahi mapana ya Taifa letu. "" Alisema Kheri.

Aidha katika mkutano huo maalum,Mwenyekiti wa Uvccm Taifa alipokea wanachama wapya 400   na kuwakabidhi kadi ya chama cha Mapinduzi  ,kati yao 45 wakitoka vyama vya upinzani.

Pia Mwenyekiti wa Uvccm Taifa alikabidhi kiasi cha Tsh.1 Mill. kwa viongozi wa Idara ya vyuo na vyuo vikuu Mkoa wa Iringa kwa ajili yamkutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili,n,huku akimuomba Mnec wa Mkoa wa Iringa Salim Asas aweze kuwasaidia.  

Awali akisoma taarifa ya kazi  za  Uvccm Mkoa wa Iringa,ktika ofisi za Uvccm Mkoa,Katibu wa Umoja wa Vijana ccm Mkoa wa Iringa,James Mgego alisema  wanaendelea kufanya uhakiki wa mali zote za  jumuiya pamojanna  na miradi  yote iliyopo katika mkoa wa Iringahuku wakitekeleza agizo la  Mwenyekiti wa ccm Taifa Rias John Magufuli.

"" Ndugu Mwenyekiti,Uvccm Mko wa Iringa  imefanya uhakiki wa Mali zote za jumuiya ndani ya Mkoa kuanzia matawi, Kata, Wilaya  na Mkoa  kwa ujumla""Alisema Mgeg



umna mrali zifuatazoShamba la Igumbilo Ekari 210 leny hati namba 43_Mbylr mali ya mako makuu,Nyumba ya umoja wa vijana  ambayo iko Igumbilo yenya hati na. 434_MBYLR ,Kiwanja cha Mwembetogwa  chenye hati na.215029/4,ambacho ndipo mradi wa vibanda vy32 vya Uvccm Mkoa wa Iringa vilipo,Vyumba viwili v katika jengo la Ccm Mkoa,Eneo la Chuo cha Ihemi_malimya makao makuu,,Pikipiki 1,Compyuta 2,Magari2, Printer1,Terevisheni moja,King'amuzi 1Sofa set 1,Vyerehani 4, Kabati la Chuma1, Kabati la mbao1, Meza kubwa 4, ,Viti 7, Mashati ya chipukizi 50,Suruali za Chipukizi 42, pamoja na Kofia za Chipukizi 34"Alisema Mgego"

 Akizungumzia hali ya  kisiasa  kwa vijana ndani ya mkoa wa Iringa alisema katika kuhakikisha vijana wanakuwa na kukomaa kisiasa wamejipanga ipasanpvyo  kuwafikia  vijana wote na kutoa  masomo na semina  mbalimbali zikiwemo za ujasiliamali na madarsa ya itikadi.

Mgego alisema  kuwa, Mkoa wa Iringa kwa sasa hali ya kisiasa ni nzuri  kutokana na utendaji mzuri wa Serikali ya  awamu ya tano inayoongozaa na Rais Dakt.John Magufuli ,wanaccm na wananchi kwa ujumla  wamerudisha  imani kubwa  kwa Serikali na Chama cha Mapinduzi.


"Kutokana na utendaji huo wa Mh.Rais wetu kipenzi cha watanzania, mkoa wetu wa Iringa madiwani na wanachama wa vyama vya upinzani wameweza kujiunga  na chama cha Mapinduzi ,ambapo amdiwani watano wa kata  kutoka Chadema ,walijihudhuru nafasi zao na  kujiunga ca CCM pamojamna madiwani watatu wa viti maalum nao wamejiunga na ccm"" Alisema Mgego.

Kwa upande wake Katibu wa Idara ya Vyuo na Vyuo vikuu Mkoa wa Iringa,Shabath Kapingaakisoma Risala ya Idara ya Vyuo na Vyuo vikuu alisema  idara ya vyuo ina matawi matatu  ya vyuo vikuu ambayo ni  Chuo kikuu Mkwawa,Chuo kikuu Ruah na Chuo kikuu Iringa pia kuna matawi ambayo yamefunguliwa katika Chuo  cha ualimu Kleruu.
Kapinga alisema katika kuhakikisha  ustawi wa chama ndani ya vyuo na vyuo vikuu unaendelea  na k(wa kitovu cha siasa  borazenye tija  kwa manufaa ya chama na Uvccm wanaendelea kuhakikisha wanafunzi wanapata  mafunzo ya itikadi ambapo mwaka 2017  katibu wa Halmashauri kuu ya Taifa uhusiano wa kitaifa Canal Lubinga alitoa mafunzo  ambayo yamekuwa na matokeo chanya  kwa mwaka wa uchaguzi 2017.,hivyo Serikali zote  za wanafunzi  zinaongozwa na  vijana wa chama cha Mapinduzi .

"Pamoja na mafanikio hayo,tunchangamoto  ya ukosefu wa ofisi kwenye matawi ,Uhaba wa  fedha  za kuweza  kutembela  matawi ya mbali ya vyuo ya wilaya  za nje ya  Iringa mjini na kutoa hamasa"" Alisema Kapingu


 Katibu wa Chama cha Malpinduzi CCM Mkoa wa Iringa,Christopher Magala akizungumza   na   Uvccm wanaosoma katika vyuo mbalimbali mkoani Iringa jana.


Mnec Mkoa wa Iringa Salim Asas akizungumza   na   Uvccm wanaosoma katika vyuo mbalimbali mkoani Iringa jana


Katibu wa Idara ya Vyuo na vyuo vikuuu Mkoa wa Iringa Shabath Kapingu akisoma Risala ya Idara ya Vyuo na Vyuo vikuu mkoa wa Iringa kwa Mwenyekiti wa Uvccm Taifa Kheri James.
































0 maoni:

Chapisha Maoni