Kwa Habari za kitaifa na kimataifa

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za michezo na burudani

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za afya

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za Kilimo

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za uchumi na biashara

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za elimu

Tembelea Kali ya habari

Jumatano, 31 Januari 2018

ROTARY CLUB OF IRINGA YAPANDA MITI 134 YA MATUNDA KATIKA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA IRINGA

Posted by Esta Malibiche on JAN 31,2018 IN NEWS
Rais wa Rotary Club of Iringa Miraji Vanginothi akiongoza zoezi la upandaji miti katika shule ya wasicahna ya Iringa (Iringa Girls) liliandaliwa na Kikundi cha Rotary Club tawi la Iringa kazi hiyo ikishirikisha wanafunzi wa kidato  cha tano na sita na uongozi wa shule siku ya jumamosi, ambapo zaidi ya miti ya matunda 134 ilipandwa. (Picha na Friday Simbaya)
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya wasicahna ya Iringa (Iringa Girls) wakishiriki zoezi la upandaji miti katika shule hiyo liliandaliwa na Kikundi cha Rotary Club tawi la Iringa kazi hiyo ikishirikisha wanafunzi wa kidato  cha tano na sita na uongozi wa shule siku ya jumamosi. (Picha na Friday Simbaya)


Rotary Club of Iringa imepanda miti ya matunda zaidi ya 134 katika ya wasichana ya iringa (Iringa Girls Secondary School) ikiwa mkakati kabambe wakupanda miti katika shule mbalimbali mkoani hapa. 

Zoezi la upandaji miti katika shule hiyo iliongozwa na rais wa rotary club of iringa Miraji Vanginothi kwa kushirikiana na MKUU wa Wilaya Iringa Richard Kasesela. 

MKUU wa Wilaya Iringa Richard Kasesela amesema kama watu watajenga utamaduni wa kuwaangalia na kuwasaidia watu wengine wataishi kwa furaha katika maisha yao. 

Kasesela ametoa kauli hiyo jana wakati alipokuwa akizungumza kwenye hafla ya upandaji miti katika shule ya Sekondari ya wasichana ya Iringa (Iringa Girls). 

Zoezi la upandaji miti katika shule hiyo liliandaliwa na Kikundi cha Rotary Club tawi la Iringa kazi hiyo ikishirikisha wanafunzi wa kidato cha tano nasita na uongozi wa shule. 

"Ngoja niseme mambo mawili,kwanza ukiwa Rotarian ni kumuungalia mwenzako,hilo ndo jambo la Msingi,ni jumuiya ya kimatifa na kikibwa ni kujitolea"alisema Kasesela. 

Kasesela aliwataka wanafunzi wa shule hiyo pamoja na vijana kujenga utamaduni wa kufanya jambo kwa lengo la kusaidia wengine na kwamba kwa kufanya hivyo watakuwa wamejijengea uwezo wa kutenda mema. 

"Hata leo tunapanda miti ,hii miti si kw aajili yetu ni kw aajili ya watu wengine,ndio sababu mi mara nyingi ninasema nivema kila unalofanya ufanye kwa ajili ya mwingine: 

:Umezaliwa na mtu mwingine,umepokelewa na mtu mwingine,utalelewa na mtu mwingine,utaolewa na mtu mwingine na utazikwa na mtu mwingine hivyo kila mtu akifanya kwa ajili ya mtu mwingine nchi yetu na dunia kwa ujumla itabaki kuwa na amani"alisema. 

Awali akizungumza katika zoezi hilo Rais wa Rotary Club Tawi la Iringa Miraji Vanginothi aliwashukuru watu waliojitolkea kupanda naa miti katika eneo la shule hiyo na kuutaka uongozi w ashule na wanafunzi kuitunza kwa faida yao na kizazi kijacho. 

"Tumepanda miti jukumu lenu ni kuhakikisha mnaitunza kwa aajili ya kizazi kijacho,miti niu kwa ajili ya kutunza mazingira miti ni kw aajili ya maatunda"alisema Vanginothi. 

Kwa upande wake Mkuu wa shule ya hiyo Blandina Nkondola alishukuru Rotary Club tawi la Iringa kwa uamuzi w akupanda miti katika shule hiyo na kuahidi kuitunza. 

"Tunawashukuru sana kwa msaada wenu wa kijamii,tumefurahishwa na uamzui wenu wa kizalenda wwenye lengo al kutunz amazingira yetu na tuwahakikishei tu kwua tutaitunza hii miti"alisema,Nkondola.

MADIWANI MAFINGA WATAKA UCHUNGUZI MANUNUZI HEWA SEKONDARI YA IHUMO

Posted by Esta Malibiche on JAN 31,2018 IN NEWS






BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga limeagiza mamlaka zinazohusika kufanya uchunguzi wa matumizi hewa ya fedha  zilizotolewa kwa ajili ujenzi wa nyumba ya mwalimu katika shule ya msingi Ihumo na atakayebainika achukuliwe hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kusimamishwa kazi.
Jumla ya Sh 2,650,000 zikiwemo Sh Milioni 2 zilizotolewa na halmashauri hiyo na Sh 650,000 zilizotoka kwenye Mfuko wa Jimbo la Mafinga Mjini, ziliingizwa katika akaunti ya shule hiyo mapema mwaka jana na matumizi yake yakafanywa kati ya mwezi Mei na Julai.
Akisoma taarifa ya mkaguzi wa ndani wa halmashauri hiyo kwenye baraza hilo juzi, diwani wa kata ya Saohill, Denis Kutemile alisema katika kipindi hicho kulikuwepo na awamu mbili ya manunuzi ya sementi na vifaa vingine vya ujenzi kwa ajili ya nyumba hiyo.
Kutumile alisema kwa kupitia risiti ya kwanza ya manunuzi hewa inaonesha jumla ya Sh 840,000 zilitumika kununua mifuko 70 ya sementi lakini katika hali ya kushangaza ilikutwa mifuko 13 tu katika stoo ya shule hiyo.
“Baada ya manunuzi hayo yalifanywa manunuzi mengine hewa ya vifaa vya ujenzi ambayo kwa kupitia risiti yake yanaonesha jumla ya Sh 650,000 zilitumika,” alisema na kutoa hoja ya kuliomba baraza hilo liamuru uchunguzi ufanyike na muhusika wa matumizi hayo hewa asimamishwe kazi.
Akipigilia msumari hoja hiyo, mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Charles Makoga alisema matumizi hayo hewa yamesababisha pia ujenzi wa nyumba hiyo usimame na akaziomba mamlaka zinazohusika zifanye uchunguzi huo haraka kwani umeathiri maendeleo ya sekta hiyo katika shule hiyo.
Wakati huo huo, baraza hilo limeagiza hatua kali zichukuliwe kwa watoa huduma wa zahanati ya Bumilahinga wanaotuhumiwa kutowasilisha kunakohusika zaidi ya Sh Milioni 2 zilizochangwa na wananchi wa kijiji hicho mwaka jana waliochangia huduma za matibabu kwa hiari kwa njia ya kadi (Tiba kwa Kadi-TIKA).
Mwenyekiti wa halmashauri hiyo alisema hiyo ni mara ya pili kwa watoa huduma wa zahanati hiyo kufanya hivyo, mara ya kwanza ikiwa ni mwaka 2016 na hivyo kusababisha walengwa kukosa huduma walizotarajia kuzipata katika kituo hicho.
“Tika ni shida katika zahanati ya Bumilahinga, watu wanachanga fedha lakini zinakaa mifukoni mwa watu na kusababisha wananchi wakose huduma za afya. Tunadhani wahusika wanatumia fedha hizo kufanyia mambo yao na kuzirudisha baada ya ukaguzi kufanyika. Baraza linataka wahusika wachukuliwe hatu kali,” alisema.
Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Rajabu Gogwa aliahidi kufuatilia utekelezaji wa maagizo hayo na lingine linaloitaka halmashauri hiyo kujitangaza kupitia vyombo mbalimbali vya habari.
Katika hatua nyingine halmashauri hiyo imeahidi kushirikiana na wadau wake wote kuendeleza mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi (VVU) yanayoendelea kuathiri nguvu kazi yao.

Makoga alisema halmashauri yake ni moja kati ya halmashauri za mkoa wa Iringa yenye kasi kubwa ya maambukizi hayo jambo linalotishia ustawi wa watu na maendeleo ya halmashauri hiyo.

MBUNGE KABATI ATOA MSAADA WA MIFUKO 25 YA SARUJI KATIKA KANISA LA FREE PENTECOST CHURCH OF TANZANIA

Posted by Esta Malibiche ON JAN 31,2018 IN NEWS

 Mbunge wa viti maalum mkoa wa iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akimkabidhi mchungaji
wa kanisa hilo la Free Pentecost Church of Tanzania Francis Okero huku akiwa sambamba na katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Iringa
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akiwa na viongozi mbalimbali  wa chama cha mapinduzi wilaya ya Iringa pamoja na madiwani wa chama hicho.
 Hili ndio kanisa la la Free Pentecost Church of Tanzania ambalo mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati amekabidhi mifuko ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali.

Na Fredy Mgunda,Iringa.

MBUNGE wa viti maalum mkoa wa iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati ametoa msaada wa mifuko ishirini na tano (25) katika kanisa la Free Pentecost Church of Tanzania lililopo kata ya Isakalilo kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa kanisa jipya ili kuendelea kutoa huduma bora ya neon la mungu.

Akizungumza wakati wa ibada iliyofanyika katika kanisani hilo Kabati alisema kuwa ni heri kujibembeleza kwa mwenye mungu kuliko kujipendekeza kwa binadamu mwenzako hivyo ni bora kuchangia shughuli za kihoro kuliko shughuli za kidunia.

“Mimi nimejitoa kuchangia shughuli zote zinazo muhusu mungu hivyo naomba mnishirikishe nami nitakuja bila kusita kwa kuwa ndio kazi yangu hata iliyonifanikisha mimi kuwa mbunge” alisema Kabati

Kabati alisema kuwa aliwaahidi kuwapa mifuko ishirini na tano ya saruji hivyo ametimiza ahadi hiyo kwa kuwapa mifuko ya saruji yote aliyoiadi hivyo amefanikiwa kutekeleza na kuwaomba wananchi wananchi wengine kuchangia maendeleo ya kanisani.

“Alikuja diwani hapa kwa niaba yangu na kuahidi mifuko hiyo ambayo ni sawa na tani moja hivyo nimeamua kutimiza kuwa lengo langu nikiahidi kitu lazima nitimize malengo yangu ya kuitoa ahadi hiyo” alisema Kabati

Aidha Kabati aliwata wananchi na viongozi mbalimbali kuendelea kuchangia shughuli za kimaendeleo kwa jamii na taasisi ambazo hazina uwezo wa kufikia mafanikio yanayotakiwa kwa ajili ya kutatua kero zinazorudisha nyuma maendeleo.

Kabati amesema kuwa wananchi na viongozi wanatakiwa kumtegemea mungu ili kuweza kufanikisha malengo wanayotarajia.

Katika hatua nyingine Kabati amewataka wazazi kuwapeleka shule watoto wao ili wakapate elimu ambayo ndiyo itakuwa dira ya maisha yao ya baadae.

Kwa uoande wake mchungaji wa kanisa hilo la Free Pentecost Church of Tanzania Francis Okero alisema kuwa walikuja viongozi wengi na kutoa ahadi nyingi lakini hakuna hata mmoja aliyetimiza ahadi yake zaidi ya mbunge Ritta Kabati.

"Nilialika wageni wengi wakala na kutoa ahadi nyingi kwa mbwembwe nyingi lakini kilichotokea hadi sana viongozi wote hakuna aliyetimiza malengo hayo hivyo nichukue furasa kushukuru" alisema Okero

Mchungaji Okero alimshukuru mbunge huyo kwa kutimiza ahadi yake ambayo itatusaidia katika ujenzi wa kanisa letu


MTULIA AZIDI KUITEKA KINONDONI ,SERA ZAKE ZAWA GUMZO

Posted by Esta Malibiche on JAN 31,2018 IN SIASA

Mgombea Ubunge katika jimbo la Kinondoni kupitia tiketi ya CCM Maulid Said Mtulia akinadi sera zake jukwaani na  kuomba kura kwa wapiga kura wa Kata ya Ndugumbi.

Image may contain: one or more people, people on stage, crowd and outdoor
Mgombea Ubunge katika jimbo la Kinondoni kupitia tiketi ya CCM Maulid Said Mtulia akinadi sera zake jukwaani na  kuomba kura kwa wapiga kura wa Kata ya Ndugumbi.
Mgombea wa ubunge jimbo la Kinondoni kupitia cha cha Mapinduzi ccm Maulid Mtulia akijinadi katika kampeni leo hii alisema  kuwa aliamua kujiondoa Cuf akiwa na akili tiamamu na wala hakushawishiwa na mtu, wala hakununuliwa kama  vyama vya upinzani wanavyodai.
'Kama Mtulia angekuwa amenunuliwa asingepewa tena dhamana ya kugombea Ubunge " - Mtulia na kuongeza kuwa
"Ningekaaje kwenye chama ambacho Mwenyekiti na Katibu hawaelewani, nimejitoa ili niwe na uhuru wa kuwatumikia wana Kinondoni." - Mtulia
Alisema  kuwa alijiuzuru Cuf  ili kuwaokoa Wananchi wa jimbo la Kinondoni na si vinginevyo
"Kuhama chama ili kujiunga na chama chenye maendeleo, huo ni usaliti?" - Mtulia na kuongeza kuwa
"Nilitoa hela yake mfukoni kujenga visima vya maji; Mtulia aliyefungua kesi mahakamani kuzuia bomoa bomoa; ndio Mtulia yule aliyeomba maghorofa ya Magomeni Watu waliojitokeza nyumba zao wakae bure" - Mtulia
"Mtulia mimi ni yule yule mkinichagua nitahakikisha naendelea kuwaletea maendeleo nikishirikiana na viongozi wenzangu na Rais wangu mpendwa Di. Magufuli " - Mtulia
"Ninaomba tena ridhaa ili nihakikishe nawaletea maendeleo wana Kinondoni kutokana na kugombea kwenye chama chenye ilani ya uchaguzi iliyoshikan dola" - Mtulia
"Naomba dhamana ya kugombea ili nikashirikiane na wenzangu kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM 2015 - 2020" - Mtulia
"Kazi yangu mkinichagua ni kwenda kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM na si porojo wala usanii" - Mtulia
"Ukichagua Mtulia umechagua maendeleo; ukimchagua Mtulia umejenga daraja kati ya Wananchi na Serikali" - Mtulia

Jumapili, 28 Januari 2018

KIKAO CHA BARAZA KUU LA JUMUIYA YA WAZAZI TANZANIA CHANFANYIKA LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Posted by Esta Malibiche ON JAN 28,2018 IN SIASA
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk. Edmund Mdolwa akizungumza wakati wa kikao cha kwanza cha Baraza Kuu la Jumuiya hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. Kikao hicho pamoja na mambo mengine kilitarajiwa kuchagua Wajumbe wa Baraza la Utekelezaji
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk. Edmund Mdolwa akizungumza wakati wa kikao cha kwanza cha Baraza Kuu la Jumuiya hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. Kikao hicho pamoja na mambo mengine kilitarajiwa kuchagua Wajumbe wa Baraza la Utekelezaji
 Kikao kikiendelea
 Wajumbe ukumbini
 Wajumbe ukumbini

 Hali ya ukumbini
 Wajumbe ukumbini
 Wajumbe ukumbini
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Dk Edmund Mndolwa akiteta jambo na naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya Tanzania Bara kushauriana jambo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Zanzibar Abdallah Haj haidar  na kushoto ni Katibu wa NEC Oganaizesheni Pereila Ame Silima
 Wajumbe ukumbini 
 Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya wazazi Tanzanaia  Zanzibar najma Giga na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Bara Burhan Ruta wakijadili jambo kwenye kikao hicho
Wajumbe ukumbini. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

Jumamosi, 27 Januari 2018

CCM YAZINDUA KAMPENI ZA UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE KINONDONI KWA KISHINDO

Posted by Esta Malibiche on JAN 28,2018 IN SIASA

 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mwigulu Nchemba (kushoto), akimnadi kwa wananchi mgombea ubunge Jimbo la Kinondoni, Maulid Mtulia wakati wa uzinduzi wa Kampeni za uchaguzi mdogo kwenye viwanja vya Biafra, Dar es Salaam Jumamosi. 
PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA

 Wafuasi wa CCM wakishangilia wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo.

 TOT wakitumbuiza wakati wa mkutano huo


 Ni furaha meza kuu
 Bendi ya Vijana Jazz ikitumbuiza

 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM,, Stephen Wassira AKISALIMIANA NAMtulia





 Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kimara Chadema,  akirudisha kadi ya chama hicho na kujiunga na CCM
 Waliokuwa upinzani wakijiunga na CCM
Mtulia akiitambulisha familia yake
leo. 
Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa kampeni za chama cha CCM, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mwigulu Nchemba akizungumza mbele ya umati wa watu waliofika kuhudhuria uzinduzi wa Kampeni za uchaguzi mdogo kwenye viwanja vya Biafra, jijini Dar es Salaam leo. 
Mgombea Ubunge jimbo la Kinondoni Maulid Mtulia akizungumza mambo mbalimbali mbele ya Wanachama wa chama hicho na Wananchi kwa ujumla mara baada kutambulishwa na kuitwa jukwaani kumwaga sera zake za kuomba kura wakati wa uzinduzi wa Kampeni za uchaguzi mdogo kwenye viwanja vya Biafra, Dar es Salaam leo.
Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kimara Chadema, Ngudu Pascal Manota akiwasalimia wananchi wa Kinondoni jioni ya leo alipokuwa akitambulishwa kwao na kurudisha kadi ya chama hicho na kujiunga na CCM,pichani kati ni Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa kampeni za chama cha CCM, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mwigulu Nchemba na kulia kwake ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM,Stephen Wasira

Wananchi na wafuasi wa chama cha CCM wakishangilia wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo,katika viwanja vya Biafra Kinondoni jana jioni 

KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU ATEMBELEA GHALA LA KUHIFADHI VIFAA VYA MAAFA DODOMA

Posted by Esta Malibiche on JAN 28,2018 IN NEWS

????????????????????????????????????
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Msaidizi (Mipango na Tafiti) Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Bashiru Taratibu alipotembelea Moja ya Ghala la kuhifadhi Vifaa vya Maafa lililopo Dodoma Januari 26, 2018.
????????????????????????????????????
Mkurugenzi Msaidizi (Mipango na Tafiti) Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Bashiru Taratibu akitoa maelezo kuhusu ghala la kuhifadhi vifaa vya maafa kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora alipotembelea kuangalia hali ya ghala hilo.
????????????????????????????????????
Afisa Ugavi Hospitali ya Mkoa wa Dodoma Bw. James Mashaka akionesha moja ya kifaa cha kuhifadhi maji wakati wa maafa (Collapse can jelly) kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora alipotembelea Ghala la kuhifadhi vifaa vya Maafa.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora akifuatilia maelezo ya ghala la kuhifadhia vifaa vya maafa   kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi (Mipango na Tafiti) Idara ya Uratibu wa Maafa Bw. Bashiru Taratibu alipotembelea kukagua hali ya ghala hilo.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora akifuatilia baadhi ya taarifa zinazohusu ghala la kuhifadhi vifaa vya maafa lililopo Dodoma.
????????????????????????????????????
Muonekano wa moja ya Ghala la kuhifadhi Vifaa vinavyotumika wakati wa Maafa lililopo Dodoma.

CHAMA CHA MAPINDUZI CCM KINONDONI CHAANDIKA HISTORIA MPYA UZINDUZI WA KAMPENI YA UBUNGE

Posted by Esta Malibiche on JAN 28,2018 IN SIASA


Baadhi ya wananchi na wafuasi wa chama cha CCM wakishangilia wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo,katika viwanja vya Biafra Kinondoni jioni ya leo.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mwigulu Nchemba (kushoto), akimnadi kwa wananchi mgombea ubunge Jimbo la Kinondoni, Maulid Mtulia wakati wa uzinduzi wa Kampeni za uchaguzi mdogo viwanja vya Biafra, Dar es Salaam leo. 
Mgombea Ubunge jimbo la Kinondoni Maulid Mtulia akiwasalimia wananchi mara baada kutambulishwa na kuitwa jukwaani kumwaga sera zake za kuomba kura wakati wa uzinduzi wa Kampeni za uchaguzi mdogo kwenye viwanja vya Biafra, Dar es Salaam leo. 
Mgombea Ubunge jimbo la Kinondoni Maulid Mtulia akizungumza mambo mbalimbali mbele ya Wanachama wa chama hicho na Wananchi kwa ujumla mara baada kutambulishwa na kuitwa jukwaani kumwaga sera zake za kuomba kura wakati wa uzinduzi wa Kampeni za uchaguzi mdogo kwenye viwanja vya Biafra, Dar es Salaam leo.
Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kimara Chadema, Ngudu Pascal Manota akiwasalimia wananchi wa Kinondoni jioni ya leo alipokuwa akitambulishwa kwao na kurudisha kadi ya chama hicho na kujiunga na CCM,pichani kati ni Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa kampeni za chama cha CCM, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mwigulu Nchemba na kulia kwake ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM,Stephen Wasira
Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kimara Chadema, Ngudu Pascal Manota akirudisha kadi ya chama hicho na kujiunga na CCM,Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa kampeni za chama cha CCM, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mwigulu Nchemba akiitazama kadi hiyo kwa makini
Aliyekuwa mjumbe wa bodi ya wadhamini wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Muslim Hassaanal ambaye hivi karibuni alihamia CCM,akimwombea kura za ushindi Mgombea Ubunge wa jimbo la Kinondoni ,Maulid Mtulia wakati wa uzinduzi wa Kampeni za uchaguzi mdogo kwenye viwanja vya Biafra, Dar es Salaam leo. 
Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa kampeni za chama cha CCM, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mwigulu Nchemba akizungumza mbele ya umati wa watu waliofika kuhudhuria uzinduzi wa Kampeni za uchaguzi mdogo kwenye viwanja vya Biafra, jijini Dar es Salaam leo. 
Baadhi ya wananchi na wafuasi wa chama cha CCM wakisikiliza kwa makini yaliyokuwa yakijiri kwenye jukwaa la uzinduzi wa kampeni Uchaguzi mdogo wa Ubunge katika jimbo la Kinondoni,mapema leo jijini Dar.PICHA NA MICHUZI JR.