Ijumaa, 8 Juni 2018

ALBERT CHALAMILA;NITAWANYANG'ANYA KADI WANACCM WANAOKIUKA KANUNI NA TARATIBU ZA CHAMA

Posted by Esta Malibiche on MEI 8,2018
Mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Iringa Albert Chalamila akizungumza na wajumbe wa Halmashauri kuu ccm Wilaya ya Iinga.Kulia kwake ni katibu wa ccm Mkoa wa Iringa Christopher Magala na kushoto kwake ni Mwenyekiti wa ccm Iringa vijijini.PICHA NA ESTA MALIBICHE.

CHAMA cha Mapinduzi ccm Mkoani Iringa kimetahadharisha kuwafuta uanachama, wanachama  wake watakaobainika kuanza kujipitisha kwenye majimbo na kata kwa lengo la kuomba uongozi huku wabunge na madiwani wa maeneo yao wakiwa madarakani.

Hayo yamesemwa jana na Mwenyekiti cha chama cha Mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa Albert Chalamila  wakati akizungumza na  wajumbe wa Halamshauri kuu ccm Wilaya ya Iringa vijijini,katika ziara yake ya kwanza toka kuchaguliwa kwake.

Katika ziara hiyo aliambatana na mjumbe wa Halmashauri kuu  CCM Taifa viti 15 Tanzania bara Teresia Mtewele pamoja na Sekretarieti ya Mkoa.

Baada ya kukutana na halmashauri kuu ya CCM ya wilaya ya Iringa,Chalamila anatarajia  kukutana  na wajumbe wa Halamshauri kuu ccm wilaya ya Iringa Mjini hapo kesho.


Katibu wa chama cha mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa Christopher Magala  akizungumza na wajumbe wa Halamashauri kuu ccm wilaya ya Iringa,aliwataka makatibu kata kuziwasilisha fomu za taarifa za wanachama wapya kabla ya june 20 mwaka huu ili  kutekeleza  agizo lililotolewa  mwaka 2016.  .
Mnec wa ccm viti 15 tanzania bara Bi.Teresia Mtewele akizungumza na wajumbe wa Halmashauri kuu  ccm Wilaya ya Iringa, aliwasihi wajumbe kuunga mkono kwa vitendo juhudi zinazofanywa na Mwenyekiti cccm Taifa Rais Dk.John Magufulihuku akiwasihi kudumisha upendo ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi.

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi ccm Wilaya ya Iringa akizungumza na wajumnbe wa Halmashauri kuu ccm Wilya ya Iringa.
Makamu katibu wa chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa Bi.Agnes Kasela,akiwasalimia wajumbe wa Halmashauri kuu ccm Wilaya ya Iringa .

Awali Mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Iringa Albert Chalamila akivalishwa skafu mapema leo asubuhi  mara baada ya kuwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Iringa mjini tayari kuanza ziara yake wilayani humo.

Katibu wa jumuiya ya wazazi Mkoa wa Iringa,akiwa na katibu wa UVCCM Mkoa wa Iringa James Mgego.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Iringa Dodo Sambu akiwa na Katibu Mwenezi CCM wilaya ya Iringa.
Wajumbe wa Halmashauri kuu ccm Wilaya ya Iringa wakimsikiliza Mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Iringa Albert Chalamila.
Wajumbe wa Halmashauri kuu ccm Wilaya ya Iringa wakimsikiliza Katibu wa Chama cha Mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa Christopher Magala.
Wajumbe wa Halmashauri kuu ccm Wilaya ya Iringa,wakiwa kwenye kikao.

































0 maoni:

Chapisha Maoni