Alhamisi, 7 Juni 2018

MWENYEKITI CCM MKOA WA IRINGA ALBERT CHALAMILA AFANYA ZIARA WILAYANI MUFINDI NA KUZUNGUMZA NA WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU CCM WILAYA.

Posted by Esta Malibiche on JUNE 7,2018 IN SIASA

Mwenyekiti wa chama chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa Albert Chalamila akizungumza na Wajumbe[Hapo pichani]  wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Mufindi.Kulia kwake ni Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa Christopher Magala,kushoto kwake ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mufindi Daudi  Yasini.PICHA NA ESTA MALIBICHE.


MWENYEKTITI wa Chama cha Mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa Albert Chalamila amewataka wajumbe wa Halmashauri kuu ccm wilaya ya Mufindi kuhakikisha wanafanya  ziara katika maeneo yao ili kutambua changamoto zinazowakabili wananchi ususani wanachama   na kuzipatia ufumbuzi.



Akizungumza leo na wajumbe wa Halmashauri kuu CCM Wilaya ya Mufindi Mkoani hapa, aliwasihi wajumbe kuendeleza utamaduni wa kuwatembelea wananchi ili kuibua kero zinazowakabili na kuzifanyia kazi kwa mujibu wa matakwa ya Irani ya Uchaguzi ya CCM ya  mwaka 2015/2020.


Chalamila  aliwataka kuzitendea haki dhamana za uongozi walizonazo katika medali za kisiasa ili   kuhakikisha CCM inazidi kuwa Chama bora na imara.Pia alitumia fursa hiyo kuvunja rasmi makundi yaliyopo ambayo yalitokana uchaguzi wa ndani ya chama na jumuiya zake.


Alisema kuwa kumekuwa na mifano mingi  ya kukosa majimbo na kata kutokana na kuwa na makundi ndani ya chama na jumuiya zakE,hivyo kwa uongozi wake hatakubali kuona majimbo na kata zinachukuliwa na upinzani kutokana na makundi au uzembe wa kiongozi Fulani.

"Nachukua fursa hii kuvunja makundi yote  ambayo yalikuwepo katika uchaguzi uliopita ndani ya chama, sisi sote tu wamoja na tunaunganishwa na itikadi ya chama cha mapinduzi tunapaswa kuungana kukijenga chama chenye sera , taratibu na misingi ya maadili.Alisema Chalamila
Mwenyekiti  huyo aliwataka wajumbe  hao,kuhakikisha wanaweka mikakati  ya ushindi katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wa kuhakikisha wanazirudisha ndani ya ccm  kata  2 zilizochukuliwa na Chadema katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 wilayani humo.
Aidha alikemea tabia ya baadhi ya wajumbe kuingilia utendaji wa wabunge na madiwani,ambappo aliwatakaa waache wabunge  wafanye kazi kwa uhuru mpaka watakapomaliza kipindi chao cha uongozi.
‘Ninawaomba  tuwache wabunge  wafanye kazi kwa uhuru.Kuna wajumbe mmeanza kuwatembeza wagombea wapya  majimboni kabla ya muda wake,kwa kufanya hivyo mnawafanya wabunge washindwe kutatua changamoto zinazowakanbili wananchi. 

Katika ziara hiyo Mwenyekiti  Albert Chalamila aliambatana na Mjumbe wa Halamshauri kuu ccm Tanzania bara Tresia Mtewele pamoja  na Sekretarieti ya ccm Mkoa   
Mwenyekiti wa chama chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa Albert Chalamila akizungumza na Wajumbe[Hapo pichani]  wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Mufindi.Kulia kwake ni Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa Christopher Magala,kushoto kwake ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mufindi Daudi  Yasini.PICHA NA ESTA MALIBICHE.
Katibu wa chama chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa Christophea Magala  akizungumza na Wajumbe[Hapo pichani]  wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Mufindi.Kulia kwake ni makamu Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa,ambae mhasibu  kushoto kwake ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Albert Chalamila .PICHA NA ESTAMALIBICHE.

Katibu wa chama cha mapinduzi ccm Wilaya ya Mufindi akizungumza
Wajumbe wa Halmashauri kuu CCM Wilaya ya Mufindi wakiwa kat katika kiao.
 









 





















 Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa Albert Chalamila akikabidhi Tisheti  zilizotolewa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ccm Taifa ambae pia ni Mnec wa Mkoa wa Iringa Salim Asas,Jumla ya tisheti 3600 zimekabidhiwa.

































0 maoni:

Chapisha Maoni